Biblia inasema nini juu ya kushirikiana katika ngono kabla kuoana?

0
7K
Pamoja na matendo mengine ya uchafu, kufanya kitendo cha mapenzi kabla kuoana kumekatazwa katika maandiko (matendo 15:20; warumi 1:29; wakorintho wa kwanza 5:1; 6:13, 7:2; 10;8; wakorintho wa pili 12:21; wagalatia 5:19; waefeso 5:3; wakolosai 3:5; wathesalonike 4:3; yuda7). Biblia inasisitiza kuepuka kitendo hicho kabla ya ndoa.hii ina maana ya kuwa ni dhambi kama ya uzinifu kwa kuwa hujaunganishwa na unayefanya naye kitendo hicho. Mapenzi baina ya mume na mke waliooana ndiyo mapenzi yanayokubalika mbele za Mungu (waebrania 13:4).
 
Kushirikiana katika ngono kabla ndoa kumeenea sana kwa sababu nyingi. Mapenzi yanastarehesha. Mungu aliyaumba hivyo. Anawataka wanaume na wanawake wafurahie kitendo cha ngono (ndani ya ndoa). Hata hivyo, lengo la msingi la ngono si starehe bali kuzaana tukaongezeke. Hivyo tunazuiwa kufanya kitendo cha ngono kabla ndoa ili tusijipatie watoto tusiowatarajia. Kama jambo hili lingezingatiwa, magonjwa ya zinaa na wamama wasioolewa na kuavya mimba na kadhalika kungepungua. Kujizuia kunaokoa maisha, kunalinda watoto wachanga na kuleta ladha halisi ya ngono pamoja na heshima kwa Mungu.
Pesquisar
Categorias
Leia Mais
Injili Ya Yesu Kristo
MWANANGU, YULE MAMA HAKUMALIZA VIZURI SAFARI YAKE
Mwanangu yule mama hakumaliza vizuri safari yake! Hivi ndivyo Mchungaji wangu, alivyoanza...
Por GOSPEL PREACHER 2021-11-23 12:39:49 0 5K
MAHUSIANO KIBIBLIA
UNA HOFU YA KUTOKUOLEWA, AU KUACHIKA? SOMA HII ITAKUSAIDIA
Kama wewe ni mwanamke na bado hujaolewa, na sasa kitu kama hofu ndani yako ya kutokuolewa...
Por GOSPEL PREACHER 2021-11-07 23:29:46 0 6K
PSALMS
Verse by verse explanation of Psalm 5
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 42 questions at the...
Por THE HOLY BIBLE 2022-04-04 23:02:55 0 5K
1 CHRONICLES
Verse by verse explanation of 1 Chronicles 3
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 35 questions at the...
Por THE HOLY BIBLE 2022-03-20 04:32:03 0 5K
MAHUSIANO KIBIBLIA
NAFASI YA MWANAMKE KIBIBLIA
Mwanzo 1:27 ‘Mungu akaumba mtu kwa mfano wake,kwa mfano wa Mungu alimwumba,mwanaume na...
Por GOSPEL PREACHER 2021-12-16 12:14:49 0 6K