Biblia inasema nini juu ya kushirikiana katika ngono kabla kuoana?

0
7K
Pamoja na matendo mengine ya uchafu, kufanya kitendo cha mapenzi kabla kuoana kumekatazwa katika maandiko (matendo 15:20; warumi 1:29; wakorintho wa kwanza 5:1; 6:13, 7:2; 10;8; wakorintho wa pili 12:21; wagalatia 5:19; waefeso 5:3; wakolosai 3:5; wathesalonike 4:3; yuda7). Biblia inasisitiza kuepuka kitendo hicho kabla ya ndoa.hii ina maana ya kuwa ni dhambi kama ya uzinifu kwa kuwa hujaunganishwa na unayefanya naye kitendo hicho. Mapenzi baina ya mume na mke waliooana ndiyo mapenzi yanayokubalika mbele za Mungu (waebrania 13:4).
 
Kushirikiana katika ngono kabla ndoa kumeenea sana kwa sababu nyingi. Mapenzi yanastarehesha. Mungu aliyaumba hivyo. Anawataka wanaume na wanawake wafurahie kitendo cha ngono (ndani ya ndoa). Hata hivyo, lengo la msingi la ngono si starehe bali kuzaana tukaongezeke. Hivyo tunazuiwa kufanya kitendo cha ngono kabla ndoa ili tusijipatie watoto tusiowatarajia. Kama jambo hili lingezingatiwa, magonjwa ya zinaa na wamama wasioolewa na kuavya mimba na kadhalika kungepungua. Kujizuia kunaokoa maisha, kunalinda watoto wachanga na kuleta ladha halisi ya ngono pamoja na heshima kwa Mungu.
Search
Categories
Read More
OTHERS
NANI ANAPOTOSHA WATU ILI WAENDE JEHANNAM, ALLAH AU SHETANI?
Ndugu wasomaji. Kwa mara nyingine tena, tunaziona sifa za Shetani ndani ya Allah wa dini ya...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 08:29:02 0 4K
DEUTERONOMY
Verse by verse explanation of Deuteronomy 11
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 31 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-01-25 06:01:25 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
Je! Mkristo anaweza pagagwa na Mapepo?
Bibilia kwa ukamilifu haitaji kama Mkristo anaweza shikwa na pepo. Ingagwa, kwa vile Mkristo...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 04:05:56 0 5K
SPIRITUAL EDUCATION
BWANA YUAJA TUWE TAYARI
BWANA YUAJA TUWENI TAYARI
By Martin Laizer 2024-01-06 16:59:17 0 4K
NDOA KIBIBLIA
MWANAUME: SIO MKE WAKO NI WEWE
Mchungaji wangu Emmanuel Nhyama Manwele ambaye ni mwalimu wangu wa kwanza wa ndoa na maswala...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-08 00:15:02 0 6K