Mtu ambaye amemwamini Yesu lakini akafa bila kubatizwa je! atenda mbinguni?

0
5Кб

JIBU: Inategemea kama hapo kabla alishausikia ukweli au la, kwa mfano kama mtu alishaufahamu ukweli tangu zamani, na hataki kufanya hivyo au anapinga, huyo mtu atahukumiwa…Lakini kama huyo mtu ndio mara yake ya kwanza kuamini na kwa bahati mbaya akafa kabla ya kubatizwa, ataokolewa atafananishwa na yule mhalifu pale msalabani aliyekufa na Bwana.

Lakini Wapo watu baada ya kuujua ukweli, hawataki kuufanya uteule wao na wito wao imara kulingana na 2Petro 1: 10 “Kwa hiyo ndugu, jitahidini zaidi kufanya imara kuitwa kwenu na uteule wenu; maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe.”

Kadhalika biblia inasema pia katika

Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana. “

Soma tena hapa..

Yakobo 4:17 “Basi yeye ajuaye kutenda mema, wala hayatendi, kwake huyo ni dhambi”.

Hivyo masuala ya rohoni ni ya kuyatimiza kwa kuogopa na kutetemeka, na sio ya kuyachukulia tu kijuu juu.. Tunapoujua ukweli na mapenzi ya Mungu tunapaswa kuyafanya.

Wafilipi 2:12”…. utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka”.

Ubarikiwe.

Поиск
Категории
Больше
NUMBERS
Verse by verse explanation of Numbers 11
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 37 questions at the...
От THE HOLY BIBLE 2022-01-24 14:34:59 0 5Кб
LEVITICUS
Verse by verse explanation of Leviticus 19
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 95 questions at the...
От THE HOLY BIBLE 2022-01-24 10:22:54 0 6Кб
OTHERS
Ni kwa nini uzao wa ubikira ni wa maana?
 Funzo la uzao wa ubikira ni la maana sana (Isaya 7:14 Mathayo 1:23; Luka 1:27,34). Kwanza,...
От MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 09:41:23 0 5Кб
GENESIS
Verse by verse explanation of Genesis 30
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 48 questions at the...
От THE HOLY BIBLE 2022-01-21 06:56:28 0 6Кб
OTHERS
FREEMASONS NA ILLUMINANT
Hiki ni kitabu chenye siri nzito za Freemasons na Illuminanti. Utangulizi.Ni mpango wa Shetani...
От GOSPEL PREACHER 2022-01-12 01:10:54 0 12Кб