Mtu ambaye amemwamini Yesu lakini akafa bila kubatizwa je! atenda mbinguni?

0
5χλμ.

JIBU: Inategemea kama hapo kabla alishausikia ukweli au la, kwa mfano kama mtu alishaufahamu ukweli tangu zamani, na hataki kufanya hivyo au anapinga, huyo mtu atahukumiwa…Lakini kama huyo mtu ndio mara yake ya kwanza kuamini na kwa bahati mbaya akafa kabla ya kubatizwa, ataokolewa atafananishwa na yule mhalifu pale msalabani aliyekufa na Bwana.

Lakini Wapo watu baada ya kuujua ukweli, hawataki kuufanya uteule wao na wito wao imara kulingana na 2Petro 1: 10 “Kwa hiyo ndugu, jitahidini zaidi kufanya imara kuitwa kwenu na uteule wenu; maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe.”

Kadhalika biblia inasema pia katika

Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana. “

Soma tena hapa..

Yakobo 4:17 “Basi yeye ajuaye kutenda mema, wala hayatendi, kwake huyo ni dhambi”.

Hivyo masuala ya rohoni ni ya kuyatimiza kwa kuogopa na kutetemeka, na sio ya kuyachukulia tu kijuu juu.. Tunapoujua ukweli na mapenzi ya Mungu tunapaswa kuyafanya.

Wafilipi 2:12”…. utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka”.

Ubarikiwe.

Αναζήτηση
Κατηγορίες
Διαβάζω περισσότερα
Religion
HOW TO BECOME A CHRISTIAN?
This question is very important, and not all human beings know its answer. But it is very simple...
από GOSPEL PREACHER 2021-08-25 10:01:32 0 6χλμ.
OTHERS
NIFANYE NINI ILI KUSHINDA TAMAA ZA MWILI?
JE, NINAWEZA KUISHINDA DHAMBI? Sasa je, tunaweza kweli kuishi humu duniani bila dhambi?  ...
από MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 22:18:48 0 6χλμ.
OTHERS
VIOJA VYA MUHAMMAD: ETI MAITI YA KIISLAMU INA UFAHAMU. NA INAJUA NANI ANAIBEBA
Kasema Mtume (S.a.w)“Hakika maiti anajua nani anaembeba, na nani anaemuosha, na nani...
από MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-25 11:40:54 0 5χλμ.
ESTHER
ESTA SURA YA 8, 9 & 10
Jina la YESU KRISTO BWANA wetu lisifiwe. Karibu kwenye mwendelezo wa kitabu cha Esta, leo...
από GOSPEL PREACHER 2022-01-20 02:55:34 0 7χλμ.
Religion
"DUNIA SIO TUFE KAMA MPIRA" JE UMBO LA DUNIA BI LIPI?
Usibitisho wa kibiblia kuhusu umbo la duniaWatu wengi wakizaliwa ukimuuliza kabla hajapata elimu...
από UUMBAJI CREATION 2022-07-19 00:55:51 1 10χλμ.