Mtu ambaye amemwamini Yesu lakini akafa bila kubatizwa je! atenda mbinguni?

0
5χλμ.

JIBU: Inategemea kama hapo kabla alishausikia ukweli au la, kwa mfano kama mtu alishaufahamu ukweli tangu zamani, na hataki kufanya hivyo au anapinga, huyo mtu atahukumiwa…Lakini kama huyo mtu ndio mara yake ya kwanza kuamini na kwa bahati mbaya akafa kabla ya kubatizwa, ataokolewa atafananishwa na yule mhalifu pale msalabani aliyekufa na Bwana.

Lakini Wapo watu baada ya kuujua ukweli, hawataki kuufanya uteule wao na wito wao imara kulingana na 2Petro 1: 10 “Kwa hiyo ndugu, jitahidini zaidi kufanya imara kuitwa kwenu na uteule wenu; maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe.”

Kadhalika biblia inasema pia katika

Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana. “

Soma tena hapa..

Yakobo 4:17 “Basi yeye ajuaye kutenda mema, wala hayatendi, kwake huyo ni dhambi”.

Hivyo masuala ya rohoni ni ya kuyatimiza kwa kuogopa na kutetemeka, na sio ya kuyachukulia tu kijuu juu.. Tunapoujua ukweli na mapenzi ya Mungu tunapaswa kuyafanya.

Wafilipi 2:12”…. utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka”.

Ubarikiwe.

Αναζήτηση
Κατηγορίες
Διαβάζω περισσότερα
REVELATION
UFUNUO 13
Tukisoma kitabu cha Ufunuo mlango wa 13 tunaona kuna wanyama wawili wanaozungumziwa pale; wa...
από GOSPEL PREACHER 2021-10-30 11:43:02 0 6χλμ.
Networking
How to find the best marketplace growth strategies
After you have seeded your marketplace with a stable initial user base, it's time to start...
από Business Academy 2022-09-17 04:03:44 0 10χλμ.
NUMBERS
Verse by verse explanation of Numbers 11
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 37 questions at the...
από THE HOLY BIBLE 2022-01-24 14:34:59 0 5χλμ.
Injili Ya Yesu Kristo
HAWA NI WATU WALIOMDHIHAKI MUNGU NA KUPATWA NA SHIDA
1. JOHN LENNON (MUIMBAJI) Wakati alipokuwa akihojiwa na mwandishi wa habari wa gazeti la American...
από GOSPEL PREACHER 2022-02-21 22:11:40 0 5χλμ.
OTHERS
SAA YA WOKOVU NI SASA!
NINI MAANA YA KUOKOKA? KUOKOKA ni lugha ya kawaida kabisa, yenye maana ya; kunusurika,...
από MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 05:57:57 0 5χλμ.