Mtu ambaye amemwamini Yesu lakini akafa bila kubatizwa je! atenda mbinguni?

0
5كيلو بايت

JIBU: Inategemea kama hapo kabla alishausikia ukweli au la, kwa mfano kama mtu alishaufahamu ukweli tangu zamani, na hataki kufanya hivyo au anapinga, huyo mtu atahukumiwa…Lakini kama huyo mtu ndio mara yake ya kwanza kuamini na kwa bahati mbaya akafa kabla ya kubatizwa, ataokolewa atafananishwa na yule mhalifu pale msalabani aliyekufa na Bwana.

Lakini Wapo watu baada ya kuujua ukweli, hawataki kuufanya uteule wao na wito wao imara kulingana na 2Petro 1: 10 “Kwa hiyo ndugu, jitahidini zaidi kufanya imara kuitwa kwenu na uteule wenu; maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe.”

Kadhalika biblia inasema pia katika

Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana. “

Soma tena hapa..

Yakobo 4:17 “Basi yeye ajuaye kutenda mema, wala hayatendi, kwake huyo ni dhambi”.

Hivyo masuala ya rohoni ni ya kuyatimiza kwa kuogopa na kutetemeka, na sio ya kuyachukulia tu kijuu juu.. Tunapoujua ukweli na mapenzi ya Mungu tunapaswa kuyafanya.

Wafilipi 2:12”…. utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka”.

Ubarikiwe.

البحث
الأقسام
إقرأ المزيد
OTHERS
UTATA KATIKA KORAN: ADAM ALIUMBWAJE?
Binadamu aliumbwa kutoka nini? Tone la Damu? Maji? Udongo? Vumbi?Jamani huu nao ni Msiba Mkubwa...
بواسطة MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 08:20:59 0 5كيلو بايت
OTHERS
How an Atheist Found God
A personal account from an atheist who was convinced no god exists, and what facts led to God....
بواسطة MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 09:43:58 0 6كيلو بايت
Injili Ya Yesu Kristo
Why did Jesus have to die?
When we ask a question such as this, we must be careful that we are not calling God into...
بواسطة MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 10:39:49 0 5كيلو بايت
NDOA KIBIBLIA
NDOA NA ROHO YA SIKU ZA MWISHO
Siku Za Mwisho:Siku za Mwisho ni siku zilizotajwa katika Biblia kuwa ni siku zote baada ya Yesu...
بواسطة GOSPEL PREACHER 2021-11-07 22:31:00 0 5كيلو بايت
JUDGES
Book of Judges Explained
Title: The book bears the fitting name “Judges,” which refers to unique leaders...
بواسطة THE HOLY BIBLE 2022-01-25 08:58:35 0 6كيلو بايت