Mtu ambaye amemwamini Yesu lakini akafa bila kubatizwa je! atenda mbinguni?

0
5كيلو بايت

JIBU: Inategemea kama hapo kabla alishausikia ukweli au la, kwa mfano kama mtu alishaufahamu ukweli tangu zamani, na hataki kufanya hivyo au anapinga, huyo mtu atahukumiwa…Lakini kama huyo mtu ndio mara yake ya kwanza kuamini na kwa bahati mbaya akafa kabla ya kubatizwa, ataokolewa atafananishwa na yule mhalifu pale msalabani aliyekufa na Bwana.

Lakini Wapo watu baada ya kuujua ukweli, hawataki kuufanya uteule wao na wito wao imara kulingana na 2Petro 1: 10 “Kwa hiyo ndugu, jitahidini zaidi kufanya imara kuitwa kwenu na uteule wenu; maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe.”

Kadhalika biblia inasema pia katika

Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana. “

Soma tena hapa..

Yakobo 4:17 “Basi yeye ajuaye kutenda mema, wala hayatendi, kwake huyo ni dhambi”.

Hivyo masuala ya rohoni ni ya kuyatimiza kwa kuogopa na kutetemeka, na sio ya kuyachukulia tu kijuu juu.. Tunapoujua ukweli na mapenzi ya Mungu tunapaswa kuyafanya.

Wafilipi 2:12”…. utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka”.

Ubarikiwe.

البحث
الأقسام
إقرأ المزيد
1 CHRONICLES
Verse by verse explanation of 1 Chronicles 21
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 32 questions at the...
بواسطة THE HOLY BIBLE 2022-03-20 05:08:28 0 6كيلو بايت
OTHERS
VLOOKUP function
Use VLOOKUP when you need to find things in a table or a range by row. For example, look up a...
بواسطة PROSPER HABONA 2024-01-01 20:56:17 0 4كيلو بايت
Injili Ya Yesu Kristo
THE TRUTH ABOUT RIGHTEOUSNESS FOUND IN FAITH
Today, brethren, I would like to talk specifically about justification. How are we counted? By...
بواسطة PROSPER HABONA 2022-01-17 01:18:01 0 7كيلو بايت
MASTERS
MASTERS
List of all subjects for the students who are taking masters courses.
بواسطة PROSHABO ONLINE SCHOOLS 2021-10-09 10:55:41 0 6كيلو بايت
MAHUSIANO KIBIBLIA
SEHEMU YA 3: MISINGI YA KIIMANI KATIKA MAHUSIANO YA UCHUMBA HADI NDOA
Bwana asifiwe!! Unaweza kusoma SEHEMU YA 1, SEHEMU YA 2, SEHEMU YA 4 au SEHEMU YA 5 ya somo hili,...
بواسطة GOSPEL PREACHER 2021-11-06 11:43:23 0 5كيلو بايت