Mtu ambaye amemwamini Yesu lakini akafa bila kubatizwa je! atenda mbinguni?

0
5كيلو بايت

JIBU: Inategemea kama hapo kabla alishausikia ukweli au la, kwa mfano kama mtu alishaufahamu ukweli tangu zamani, na hataki kufanya hivyo au anapinga, huyo mtu atahukumiwa…Lakini kama huyo mtu ndio mara yake ya kwanza kuamini na kwa bahati mbaya akafa kabla ya kubatizwa, ataokolewa atafananishwa na yule mhalifu pale msalabani aliyekufa na Bwana.

Lakini Wapo watu baada ya kuujua ukweli, hawataki kuufanya uteule wao na wito wao imara kulingana na 2Petro 1: 10 “Kwa hiyo ndugu, jitahidini zaidi kufanya imara kuitwa kwenu na uteule wenu; maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe.”

Kadhalika biblia inasema pia katika

Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana. “

Soma tena hapa..

Yakobo 4:17 “Basi yeye ajuaye kutenda mema, wala hayatendi, kwake huyo ni dhambi”.

Hivyo masuala ya rohoni ni ya kuyatimiza kwa kuogopa na kutetemeka, na sio ya kuyachukulia tu kijuu juu.. Tunapoujua ukweli na mapenzi ya Mungu tunapaswa kuyafanya.

Wafilipi 2:12”…. utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka”.

Ubarikiwe.

البحث
الأقسام
إقرأ المزيد
EZRA
Verse by verse explanation of Ezra 8
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 24 questions at the...
بواسطة THE HOLY BIBLE 2022-04-02 06:23:21 0 6كيلو بايت
GENESIS
Verse by verse explanation of Genesis 36
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 20 questions at the...
بواسطة THE HOLY BIBLE 2022-01-21 09:07:07 0 5كيلو بايت
JOSHUA
Verse by verse explanation of Joshua 8
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 29 questions at the...
بواسطة THE HOLY BIBLE 2022-01-25 07:29:00 0 5كيلو بايت
NEHEMIAH
Verse by verse explanation of Nehemiah 11
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 30 questions at the...
بواسطة THE HOLY BIBLE 2022-04-02 12:35:09 0 5كيلو بايت
Injili Ya Yesu Kristo
YESU ATAKUPONYA.
Bwana Yesu asifiwe… Kwa ufupi, “Hata walipokosa nafasi ya kumpeleka ndani kwa ajili...
بواسطة GOSPEL PREACHER 2022-03-30 04:53:31 0 5كيلو بايت