Mtu ambaye amemwamini Yesu lakini akafa bila kubatizwa je! atenda mbinguni?

0
5K

JIBU: Inategemea kama hapo kabla alishausikia ukweli au la, kwa mfano kama mtu alishaufahamu ukweli tangu zamani, na hataki kufanya hivyo au anapinga, huyo mtu atahukumiwa…Lakini kama huyo mtu ndio mara yake ya kwanza kuamini na kwa bahati mbaya akafa kabla ya kubatizwa, ataokolewa atafananishwa na yule mhalifu pale msalabani aliyekufa na Bwana.

Lakini Wapo watu baada ya kuujua ukweli, hawataki kuufanya uteule wao na wito wao imara kulingana na 2Petro 1: 10 “Kwa hiyo ndugu, jitahidini zaidi kufanya imara kuitwa kwenu na uteule wenu; maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe.”

Kadhalika biblia inasema pia katika

Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana. “

Soma tena hapa..

Yakobo 4:17 “Basi yeye ajuaye kutenda mema, wala hayatendi, kwake huyo ni dhambi”.

Hivyo masuala ya rohoni ni ya kuyatimiza kwa kuogopa na kutetemeka, na sio ya kuyachukulia tu kijuu juu.. Tunapoujua ukweli na mapenzi ya Mungu tunapaswa kuyafanya.

Wafilipi 2:12”…. utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka”.

Ubarikiwe.

Search
Categories
Read More
Injili Ya Yesu Kristo
Yesu ni nani?
Yesu wa Nazareti ni nani kwako? Maisha yako hapa duniani na ya milele yanaguswa na jibu lako kwa...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 05:27:05 0 5K
MASWALI & MAJIBU
Je! Bikira Maria Ni MALKIA WA MBINGUNI?
JIBU: Neno Malkia wa mbinguni limeonekana mara mbili katika biblia Sehemu ya kwanza ni...
By GOSPEL PREACHER 2022-06-13 09:42:45 0 7K
BIBLICAL FINANCIAL EDUCATION
10 Financial Principles That Are Biblical
Some people mash cans, crunch bottles or shred newspapers and magazines to further the cause of...
By BIBLICAL FINANCES 2021-12-29 15:13:24 0 12K
EXODUS
Verse by verse explanation of Exodus 10
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 58 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-01-22 11:23:54 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
Biblia inasema nini juu ya kunywa pombe? Je, ni dhambi kwa mkristo kunywa pombe?
Maandiko yana ilani nyingi juu ya kunywa kileo (mambo ya walawi 10:9; hesabu6:3; kumbukumbu la...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 04:07:04 0 6K