Mtu ambaye amemwamini Yesu lakini akafa bila kubatizwa je! atenda mbinguni?

0
5K

JIBU: Inategemea kama hapo kabla alishausikia ukweli au la, kwa mfano kama mtu alishaufahamu ukweli tangu zamani, na hataki kufanya hivyo au anapinga, huyo mtu atahukumiwa…Lakini kama huyo mtu ndio mara yake ya kwanza kuamini na kwa bahati mbaya akafa kabla ya kubatizwa, ataokolewa atafananishwa na yule mhalifu pale msalabani aliyekufa na Bwana.

Lakini Wapo watu baada ya kuujua ukweli, hawataki kuufanya uteule wao na wito wao imara kulingana na 2Petro 1: 10 “Kwa hiyo ndugu, jitahidini zaidi kufanya imara kuitwa kwenu na uteule wenu; maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe.”

Kadhalika biblia inasema pia katika

Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana. “

Soma tena hapa..

Yakobo 4:17 “Basi yeye ajuaye kutenda mema, wala hayatendi, kwake huyo ni dhambi”.

Hivyo masuala ya rohoni ni ya kuyatimiza kwa kuogopa na kutetemeka, na sio ya kuyachukulia tu kijuu juu.. Tunapoujua ukweli na mapenzi ya Mungu tunapaswa kuyafanya.

Wafilipi 2:12”…. utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka”.

Ubarikiwe.

Search
Categories
Read More
JOSHUA
Verse by verse explanation of Joshua 3
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 22 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-01-25 07:16:08 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
ALIVYOOKOKA SHEIKH ALHAJI RASHID ABUBAKAR WA MSIKITI WA MTAA WA MWANZA ILALA DAR ES SALAAM
1. AKIRI KULA NYAMA ZA WATU2. AKIRI KUNYWA DAMU ZA WATU3. AKIRI KUMEZA MAJINI 3604. ASEMA UISLAM...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 21:24:13 0 8K
SPIRITUAL EDUCATION
If Jesus is God, then who did He pray to?
This is a very common question and the answer is found in understanding...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 06:03:16 0 6K
MAHUSIANO KIBIBLIA
Biblia inasema nini juu ya kushirikiana katika ngono kabla kuoana?
Pamoja na matendo mengine ya uchafu, kufanya kitendo cha mapenzi kabla kuoana kumekatazwa katika...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 04:08:31 0 7K
Injili Ya Yesu Kristo
Je, Nina wezaje kupokea msamaha wa dhambi toka kwa Mungu?
Matendo ya Mitume 13:38 yasema, “Basi naijulikane kwenu, ndugu zangu ya kuwa kwa huyo...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 09:42:55 0 5K