Mtu ambaye amemwamini Yesu lakini akafa bila kubatizwa je! atenda mbinguni?

0
5KB

JIBU: Inategemea kama hapo kabla alishausikia ukweli au la, kwa mfano kama mtu alishaufahamu ukweli tangu zamani, na hataki kufanya hivyo au anapinga, huyo mtu atahukumiwa…Lakini kama huyo mtu ndio mara yake ya kwanza kuamini na kwa bahati mbaya akafa kabla ya kubatizwa, ataokolewa atafananishwa na yule mhalifu pale msalabani aliyekufa na Bwana.

Lakini Wapo watu baada ya kuujua ukweli, hawataki kuufanya uteule wao na wito wao imara kulingana na 2Petro 1: 10 “Kwa hiyo ndugu, jitahidini zaidi kufanya imara kuitwa kwenu na uteule wenu; maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe.”

Kadhalika biblia inasema pia katika

Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana. “

Soma tena hapa..

Yakobo 4:17 “Basi yeye ajuaye kutenda mema, wala hayatendi, kwake huyo ni dhambi”.

Hivyo masuala ya rohoni ni ya kuyatimiza kwa kuogopa na kutetemeka, na sio ya kuyachukulia tu kijuu juu.. Tunapoujua ukweli na mapenzi ya Mungu tunapaswa kuyafanya.

Wafilipi 2:12”…. utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka”.

Ubarikiwe.

Pesquisar
Categorias
Leia mais
SPIRITUAL EDUCATION
SOMO:BWANA AMETUPA MOTO DUNIANI LUKA 12:49
SOMO:BWANA AMETUPA MOTO DUNIANI LUKA 12:49.
Por Martin Laizer 2023-11-10 08:43:36 0 9KB
MASWALI & MAJIBU
Je! Dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu ni ipi?
SWALI : Dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu ni ipi? JIBU: Tukisoma; Mathayo 12:25-32 ”...
Por GOSPEL PREACHER 2022-06-13 00:19:41 0 6KB
OTHERS
MUHAMMAD ALIKUWA NA WAKE ZAIDI YA 20
Huu ni MSIBA mkubwa sana. Ifuatayo ni orodha ya wake wa Muhammad iliyoandaliwa na mwanazuoni wa...
Por MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 22:48:32 0 5KB
1 SAMUEL
Verse by verse explanation of 1 Samuel 10
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 40 questions at the...
Por THE HOLY BIBLE 2022-01-26 03:35:03 0 5KB
Networking
How to validate your marketplace idea before building the platform
Recognizing a good marketplace idea or a viable business model is difficult. If you...
Por Business Academy 2022-09-17 03:23:20 0 7KB