Mtu ambaye amemwamini Yesu lakini akafa bila kubatizwa je! atenda mbinguni?

0
5KB

JIBU: Inategemea kama hapo kabla alishausikia ukweli au la, kwa mfano kama mtu alishaufahamu ukweli tangu zamani, na hataki kufanya hivyo au anapinga, huyo mtu atahukumiwa…Lakini kama huyo mtu ndio mara yake ya kwanza kuamini na kwa bahati mbaya akafa kabla ya kubatizwa, ataokolewa atafananishwa na yule mhalifu pale msalabani aliyekufa na Bwana.

Lakini Wapo watu baada ya kuujua ukweli, hawataki kuufanya uteule wao na wito wao imara kulingana na 2Petro 1: 10 “Kwa hiyo ndugu, jitahidini zaidi kufanya imara kuitwa kwenu na uteule wenu; maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe.”

Kadhalika biblia inasema pia katika

Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana. “

Soma tena hapa..

Yakobo 4:17 “Basi yeye ajuaye kutenda mema, wala hayatendi, kwake huyo ni dhambi”.

Hivyo masuala ya rohoni ni ya kuyatimiza kwa kuogopa na kutetemeka, na sio ya kuyachukulia tu kijuu juu.. Tunapoujua ukweli na mapenzi ya Mungu tunapaswa kuyafanya.

Wafilipi 2:12”…. utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka”.

Ubarikiwe.

Rechercher
Catégories
Lire la suite
Injili Ya Yesu Kristo
HAKUNA MTU ALIYEMWONA MUNGU
Neno la Uzima kutoka kwa  Askofu Zachary Kakobe        ...
Par GOSPEL PREACHER 2022-01-12 01:38:03 0 6KB
Injili Ya Yesu Kristo
NAMNA IMANI INAVYOWEZA KUFANYIKA MSAADA KATIKA MAISHA YAKO.
 Siku zote neno la Mungu linasema katika 2Petro 5:7 kwamba siku zote Mungu anajishughulisha...
Par GOSPEL PREACHER 2021-11-23 12:44:24 0 5KB
Injili Ya Yesu Kristo
ROHO MTAKATIFU NI MUNGU
Ndugu msomaji,Watu wengi hawafahamu kuhusu Roho Mtakatifu. Roho Mtakatifu Ni Nani?Baadhi ya watu...
Par MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 05:21:47 0 5KB
1 KINGS
Verse by verse explanation of 1 Kings 10
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 30 questions at the...
Par THE HOLY BIBLE 2022-02-05 13:05:59 0 6KB
JOB
Verse by verse explanation of Job 27
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 22 questions at the...
Par THE HOLY BIBLE 2022-04-03 04:03:51 0 5KB