Mtu ambaye amemwamini Yesu lakini akafa bila kubatizwa je! atenda mbinguni?

0
5KB

JIBU: Inategemea kama hapo kabla alishausikia ukweli au la, kwa mfano kama mtu alishaufahamu ukweli tangu zamani, na hataki kufanya hivyo au anapinga, huyo mtu atahukumiwa…Lakini kama huyo mtu ndio mara yake ya kwanza kuamini na kwa bahati mbaya akafa kabla ya kubatizwa, ataokolewa atafananishwa na yule mhalifu pale msalabani aliyekufa na Bwana.

Lakini Wapo watu baada ya kuujua ukweli, hawataki kuufanya uteule wao na wito wao imara kulingana na 2Petro 1: 10 “Kwa hiyo ndugu, jitahidini zaidi kufanya imara kuitwa kwenu na uteule wenu; maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe.”

Kadhalika biblia inasema pia katika

Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana. “

Soma tena hapa..

Yakobo 4:17 “Basi yeye ajuaye kutenda mema, wala hayatendi, kwake huyo ni dhambi”.

Hivyo masuala ya rohoni ni ya kuyatimiza kwa kuogopa na kutetemeka, na sio ya kuyachukulia tu kijuu juu.. Tunapoujua ukweli na mapenzi ya Mungu tunapaswa kuyafanya.

Wafilipi 2:12”…. utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka”.

Ubarikiwe.

Suche
Kategorien
Mehr lesen
ESTHER
Verse by verse explanation of Esther 8
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 30 questions at the...
Von THE HOLY BIBLE 2022-04-02 13:03:00 0 6KB
Religion
USIFUATE MAMBO YAKO TU!!
Ipo faida  ya kufuata mambo yako na kutojishughulisha na mambo ya wengine!.. Lakini pia ipo...
Von GOSPEL PREACHER 2021-10-09 23:17:01 2 6KB
SPIRITUAL EDUCATION
AGANO LA AMANI ISAYA 54:10,EZEKIEL 34:25
PASIPO AGONO LA AMANI YA KRISTO HAPANA MAFANIKIO
Von Martin Laizer 2023-09-25 15:12:47 0 11KB
OTHERS
JE, YESU ALITUMWA KWA ISRAEL PEKE YAKE?
Waislamu “wanahubiri” kuwa Yesu  hakuja kwa ajili ya ulimwengu wote bali...
Von MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 05:11:00 0 5KB
OTHERS
KORAN INADAI KUWA YESU ALIZEEKEA HAPA DUNIANI.
VIOJA NDANI YA KORAN.KORAN INADAI KUWA YESU ALIZEEKEA HAPA DUNIANI.Leo tunajifunza Vioja vya...
Von MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 08:19:11 0 5KB