Mtu ambaye amemwamini Yesu lakini akafa bila kubatizwa je! atenda mbinguni?

0
5K

JIBU: Inategemea kama hapo kabla alishausikia ukweli au la, kwa mfano kama mtu alishaufahamu ukweli tangu zamani, na hataki kufanya hivyo au anapinga, huyo mtu atahukumiwa…Lakini kama huyo mtu ndio mara yake ya kwanza kuamini na kwa bahati mbaya akafa kabla ya kubatizwa, ataokolewa atafananishwa na yule mhalifu pale msalabani aliyekufa na Bwana.

Lakini Wapo watu baada ya kuujua ukweli, hawataki kuufanya uteule wao na wito wao imara kulingana na 2Petro 1: 10 “Kwa hiyo ndugu, jitahidini zaidi kufanya imara kuitwa kwenu na uteule wenu; maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe.”

Kadhalika biblia inasema pia katika

Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana. “

Soma tena hapa..

Yakobo 4:17 “Basi yeye ajuaye kutenda mema, wala hayatendi, kwake huyo ni dhambi”.

Hivyo masuala ya rohoni ni ya kuyatimiza kwa kuogopa na kutetemeka, na sio ya kuyachukulia tu kijuu juu.. Tunapoujua ukweli na mapenzi ya Mungu tunapaswa kuyafanya.

Wafilipi 2:12”…. utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka”.

Ubarikiwe.

Site içinde arama yapın
Kategoriler
Read More
Other
BOOK OF GENESIS
Book of Genesis Explained Genesis is the book of beginnings. It records the beginning of time,...
By PROSHABO NETWORK 2021-10-02 23:29:25 0 8K
MASWALI & MAJIBU
Je! Inawezekana mtu akawa anafanya miujiza na bado asinyakuliwe?
SWALI: Naomba kuelewa kwanini mtu atoe pepo, aombee wagonjwa wapone, asikie sauti ya Mungu...
By GOSPEL PREACHER 2022-06-12 23:16:05 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
UNAJIFUNZA NINI KUPITIA HUDUMA YA ANANIA NA BARNABA KWA PAULO?
Nakusalimu katika jina la Bwana, mpenzi msomaji.   Katika nyanja hii, leo nimeona ni vema...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-23 12:24:28 0 5K
SPIRITUAL EDUCATION
NGURUMO SABA
Katika kufunguliwa kwa mihuri saba, kwenye kile kitabu cha ufunuo, tunaona kuwa muhuri wa saba...
By GOSPEL PREACHER 2021-10-30 11:00:50 0 5K
OTHERS
Kwa nini imani ya Kikristo ni bora zaidi ya Kiislamu?
1. Utangulizi Kuamini juu ya Mungu Mmoja, ni imani katika Uwepo wa Utendaji wa Mungu mmoja [1]....
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 06:28:18 0 5K