Mtu ambaye amemwamini Yesu lakini akafa bila kubatizwa je! atenda mbinguni?

0
4K

JIBU: Inategemea kama hapo kabla alishausikia ukweli au la, kwa mfano kama mtu alishaufahamu ukweli tangu zamani, na hataki kufanya hivyo au anapinga, huyo mtu atahukumiwa…Lakini kama huyo mtu ndio mara yake ya kwanza kuamini na kwa bahati mbaya akafa kabla ya kubatizwa, ataokolewa atafananishwa na yule mhalifu pale msalabani aliyekufa na Bwana.

Lakini Wapo watu baada ya kuujua ukweli, hawataki kuufanya uteule wao na wito wao imara kulingana na 2Petro 1: 10 “Kwa hiyo ndugu, jitahidini zaidi kufanya imara kuitwa kwenu na uteule wenu; maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe.”

Kadhalika biblia inasema pia katika

Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana. “

Soma tena hapa..

Yakobo 4:17 “Basi yeye ajuaye kutenda mema, wala hayatendi, kwake huyo ni dhambi”.

Hivyo masuala ya rohoni ni ya kuyatimiza kwa kuogopa na kutetemeka, na sio ya kuyachukulia tu kijuu juu.. Tunapoujua ukweli na mapenzi ya Mungu tunapaswa kuyafanya.

Wafilipi 2:12”…. utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka”.

Ubarikiwe.

Site içinde arama yapın
Kategoriler
Read More
MAHUSIANO KIBIBLIA
HATUA 7 ZA KUMALIZA UGOMVI NA MWENZAKO
“Ndugu yako akikukosa, enenda ukamwonye, wewe na yeye peke yenu; akikusikia,...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-06 10:57:06 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
TAJI KWA WATAKATIFU NA HARUSI YA MWANAKONDOO
Neno la Uzima kutoka kwa  Askofu Zachary Kakobe        ...
By GOSPEL PREACHER 2022-01-12 00:35:38 2 5K
OTHERS
Je, Walio-okoka Wanaweza Kwenda Jehanamu?
Kama Paulo anavyoandika, Mungu hutuadhibu “ili isitupase adhabu pamoja na dunia”...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 10:04:22 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
DALILI ZA KUMJUA MTUMISHI/NABII WA UONGO.
Ndugu msomaji na mwanadamu uliyeumbwa kwa mfano wa sura ya MUNGU na siyo ya shetani, MUNGU huyu...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-19 05:52:58 0 6K
Injili Ya Yesu Kristo
DINI YA KIISLAM ILIANZISHWA SIKU YA JUMATATU MWEZI WA 17, SAWA SAWA NA TAREHE 27 DESEMBA MKWA 610 B.K.
KUMBE UISLAM NI DINI YA KUTENGEZA TU, TENA CHANGA SANA NA HAIKUWEPO KABLA YA MUHAMMAD  ...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 22:13:31 0 5K