Mtu ambaye amemwamini Yesu lakini akafa bila kubatizwa je! atenda mbinguni?

0
5K

JIBU: Inategemea kama hapo kabla alishausikia ukweli au la, kwa mfano kama mtu alishaufahamu ukweli tangu zamani, na hataki kufanya hivyo au anapinga, huyo mtu atahukumiwa…Lakini kama huyo mtu ndio mara yake ya kwanza kuamini na kwa bahati mbaya akafa kabla ya kubatizwa, ataokolewa atafananishwa na yule mhalifu pale msalabani aliyekufa na Bwana.

Lakini Wapo watu baada ya kuujua ukweli, hawataki kuufanya uteule wao na wito wao imara kulingana na 2Petro 1: 10 “Kwa hiyo ndugu, jitahidini zaidi kufanya imara kuitwa kwenu na uteule wenu; maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe.”

Kadhalika biblia inasema pia katika

Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana. “

Soma tena hapa..

Yakobo 4:17 “Basi yeye ajuaye kutenda mema, wala hayatendi, kwake huyo ni dhambi”.

Hivyo masuala ya rohoni ni ya kuyatimiza kwa kuogopa na kutetemeka, na sio ya kuyachukulia tu kijuu juu.. Tunapoujua ukweli na mapenzi ya Mungu tunapaswa kuyafanya.

Wafilipi 2:12”…. utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka”.

Ubarikiwe.

Pesquisar
Categorias
Leia Mais
Injili Ya Yesu Kristo
MFANO WA MPANZI NA MBEGU
  LUKA 5;8-5 "Mpanzi alitoka kwenda kupanda mbegu zake; naye alipokuwa akizipanda, nyingine...
Por GOSPEL PREACHER 2022-01-15 22:24:38 0 6K
JOB
Verse by verse explanation of Job 39
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 24 questions at the...
Por THE HOLY BIBLE 2022-04-03 04:22:03 0 6K
Injili Ya Yesu Kristo
UNYENYEKEVU.
Bwana Yesu asifiwe... Kwa ufupi. ” Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni...
Por GOSPEL PREACHER 2022-03-30 04:54:56 0 5K
1 CHRONICLES
Verse by verse explanation of 1 Chronicles 23
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 25 questions at the...
Por THE HOLY BIBLE 2022-03-20 05:15:13 0 6K
JUDGES
Verse by verse explanation of Judges 13
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 39 questions at the...
Por THE HOLY BIBLE 2022-01-25 11:07:08 0 6K