Mtu ambaye amemwamini Yesu lakini akafa bila kubatizwa je! atenda mbinguni?

0
5K

JIBU: Inategemea kama hapo kabla alishausikia ukweli au la, kwa mfano kama mtu alishaufahamu ukweli tangu zamani, na hataki kufanya hivyo au anapinga, huyo mtu atahukumiwa…Lakini kama huyo mtu ndio mara yake ya kwanza kuamini na kwa bahati mbaya akafa kabla ya kubatizwa, ataokolewa atafananishwa na yule mhalifu pale msalabani aliyekufa na Bwana.

Lakini Wapo watu baada ya kuujua ukweli, hawataki kuufanya uteule wao na wito wao imara kulingana na 2Petro 1: 10 “Kwa hiyo ndugu, jitahidini zaidi kufanya imara kuitwa kwenu na uteule wenu; maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe.”

Kadhalika biblia inasema pia katika

Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana. “

Soma tena hapa..

Yakobo 4:17 “Basi yeye ajuaye kutenda mema, wala hayatendi, kwake huyo ni dhambi”.

Hivyo masuala ya rohoni ni ya kuyatimiza kwa kuogopa na kutetemeka, na sio ya kuyachukulia tu kijuu juu.. Tunapoujua ukweli na mapenzi ya Mungu tunapaswa kuyafanya.

Wafilipi 2:12”…. utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka”.

Ubarikiwe.

Pesquisar
Categorias
Leia Mais
OTHERS
Is the Jehovah’s Witness religion Christian?
The Jehovah’s Witness (aka Watchtower Bible and Tract Society) religion is not...
Por MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-29 06:19:46 0 8K
SPIRITUAL EDUCATION
The Holy Spirit's Comfort, Guidance and Help
In John, chapter 14, verses 15 to 17, Jesus said: "If ye love me, keep my commandments. And I...
Por MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 18:37:56 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
FAHAMU KUHUSU JINA LA FARAO
Kwa ufupi… Bwana Yesu asifiwe… Je unafahamu nini kuhusu jina hili la farao? Basi...
Por GOSPEL PREACHER 2022-03-30 05:04:49 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
Na sisi je tufanye nini?
Luka 3:2-14 “wakati wa ukuhani mkuu wa Anasi na Kayafa, neno la Mungu lilimfikia...
Por GOSPEL PREACHER 2022-03-31 14:37:54 0 6K
Injili Ya Yesu Kristo
NI NINI MAANA YA “ROHO”?
Hebu tuzungumzie jinsi Biblia inavyotumia neno “roho.” Watu fulani hufikiri kwamba...
Por MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 19:51:05 0 7K