Mtu ambaye amemwamini Yesu lakini akafa bila kubatizwa je! atenda mbinguni?

0
5K

JIBU: Inategemea kama hapo kabla alishausikia ukweli au la, kwa mfano kama mtu alishaufahamu ukweli tangu zamani, na hataki kufanya hivyo au anapinga, huyo mtu atahukumiwa…Lakini kama huyo mtu ndio mara yake ya kwanza kuamini na kwa bahati mbaya akafa kabla ya kubatizwa, ataokolewa atafananishwa na yule mhalifu pale msalabani aliyekufa na Bwana.

Lakini Wapo watu baada ya kuujua ukweli, hawataki kuufanya uteule wao na wito wao imara kulingana na 2Petro 1: 10 “Kwa hiyo ndugu, jitahidini zaidi kufanya imara kuitwa kwenu na uteule wenu; maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe.”

Kadhalika biblia inasema pia katika

Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana. “

Soma tena hapa..

Yakobo 4:17 “Basi yeye ajuaye kutenda mema, wala hayatendi, kwake huyo ni dhambi”.

Hivyo masuala ya rohoni ni ya kuyatimiza kwa kuogopa na kutetemeka, na sio ya kuyachukulia tu kijuu juu.. Tunapoujua ukweli na mapenzi ya Mungu tunapaswa kuyafanya.

Wafilipi 2:12”…. utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka”.

Ubarikiwe.

Cerca
Categorie
Leggi tutto
OTHERS
SAA YA WOKOVU NI SASA!
NINI MAANA YA KUOKOKA? KUOKOKA ni lugha ya kawaida kabisa, yenye maana ya; kunusurika,...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 05:57:57 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
Ngazi ya Yakobo
Mwanzo 28:10-19 “Yakobo akatoka Beer-sheba, kwenda Harani. Akafika mahali fulani...
By GOSPEL PREACHER 2022-03-31 14:40:12 0 6K
SPIRITUAL EDUCATION
Epuka Fundisho la Uongo kuwa "Mara Baada ya Kuokolewa, Umeokolewa Daima"
Mafundisho machache ya uwongo ni hatari zaidi kuliko madai ya Calvin ya “usalama wa...
By PROSPER HABONA 2022-01-15 11:47:40 0 8K
NUMBERS
Verse by verse explanation of Numbers 5
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 32 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-01-24 14:15:41 0 5K
1 SAMUEL
Verse by verse explanation of 1 Samuel 19
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 30 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-01-26 03:53:56 0 5K