Mtu ambaye amemwamini Yesu lakini akafa bila kubatizwa je! atenda mbinguni?

0
5K

JIBU: Inategemea kama hapo kabla alishausikia ukweli au la, kwa mfano kama mtu alishaufahamu ukweli tangu zamani, na hataki kufanya hivyo au anapinga, huyo mtu atahukumiwa…Lakini kama huyo mtu ndio mara yake ya kwanza kuamini na kwa bahati mbaya akafa kabla ya kubatizwa, ataokolewa atafananishwa na yule mhalifu pale msalabani aliyekufa na Bwana.

Lakini Wapo watu baada ya kuujua ukweli, hawataki kuufanya uteule wao na wito wao imara kulingana na 2Petro 1: 10 “Kwa hiyo ndugu, jitahidini zaidi kufanya imara kuitwa kwenu na uteule wenu; maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe.”

Kadhalika biblia inasema pia katika

Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana. “

Soma tena hapa..

Yakobo 4:17 “Basi yeye ajuaye kutenda mema, wala hayatendi, kwake huyo ni dhambi”.

Hivyo masuala ya rohoni ni ya kuyatimiza kwa kuogopa na kutetemeka, na sio ya kuyachukulia tu kijuu juu.. Tunapoujua ukweli na mapenzi ya Mungu tunapaswa kuyafanya.

Wafilipi 2:12”…. utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka”.

Ubarikiwe.

Cerca
Categorie
Leggi tutto
UCHUMBA KIBIBLIA
DALILI ZA MCHUMBA ASIYEKUPENDA, ALIYEKUACHA BILA KUKWAMBIA
Mahusiano ya uchumba yamekuwa na changamoto nyingi sana zisizoisha.Moja ya changamoto kubwa...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-07 22:50:19 0 6K
JOSHUA
Verse by verse explanation of Joshua 8
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 29 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-01-25 07:29:00 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
UMEJIAANDAJE KWA TUKIO LA UNYAKUO? (Sehemu ya 1)
Nakusalimu kwa jina la Yesu! Ili uweze kuelewa somo hili mpenzi msomaji nakushauri tafuta muda...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-23 13:07:03 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
UKWELI KUHUSU HAKI IPATIKANAYO KWA IMANI
BWANA YESU ASIFIWE!! Mpendwa Roho Mtakatifu ameweka Nyakati hizi tunazoishi ni nyakati/siku za...
By PROSPER HABONA 2022-01-16 14:17:28 0 5K
OTHERS
UTHIBITISHO 12 KUWA ALLAH SIO MUNGU
  Leo nitawapa Sababu 12 kwanini allah sio mungu. 1. ALLAH NI MUNGU ASIYE NA JINA...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 03:12:48 0 5K