JE, UNAWEZA KUOKOKA BILA YA KUPITIA YESU?

0
4K
Je naweza kuingia mbinguni bila kumkubali Yesu kama Bwana na Mwokozi wangu?
Jibu: Hapana, huwezi kwenda mbinguni kama unakataa kumkubali Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wako. Mambo manne ya kuzingatia kwenye jibu hili.
 
Haki: Mungu ni mwema, Mtakatifu, mwenye haki kwa watu wote (Waebrania 6:10). Mungu huwahukumu watu kwa kuzingatia ufahamu walio nao (Warumi 4:15; 5:13). Abraham hakujua jina la Yesu, lakini alimfuata Mungu na bado aliokolewa kupitia Yesu. (Yohana 8:56, Waebrania 9)
 
Njia moja tu: Hatuwezi kwenda mbinguni kwa kutegemea haki yetu wenyewe; tunahitaji rehema na neema za Mungu kupitia kwa Yesu. Yesu siyo tu njia ya kwendea kwa Mungu bali pia ni njia pekee ya kwendea kwa Mungu. (Yoh 14:6; 15:5; Matendo 4:12). Njia pekee ya kuifikia mbingu ya Mungu ni kupitia njia ya Mungu.
 
Ukimkataa Yesu kama Mwana wa Mungu utakuwa umeikataa mbingu: Hata kwa mtu anayeshika dini sana, Farisayo wa kiyahudi, Yesu alisema kuwa kama ukinikataa utakufa kwenye dhambi zako. (Yohana 8:24)
 
Mungu hutafuta: Mungu hapendi mtu yoyote aangamie (2 Petro 3:9), lakini kama Yeremia alivyowalilia watu wake (Yeremia 13:17; 14:17) na kama Yesu alivyoililia Yerusalem (Luka 19:41-44) na kama Petro alivyowasihi watu waliokuwa wanamsikiliza (Matendo 2:40), Mungu, huwatafuta watu wake kwa haja hiyo hiyo.
 
Ni mimi Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.
Shalom.
Site içinde arama yapın
Kategoriler
Read More
2 KINGS
Verse by verse explanation of 2 Kings 13
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 27 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-03-19 20:27:08 0 5K
NDOA KIBIBLIA
USIDANGANYIKE, MATUMIZI YA VIDEO ZA NGONO KWA WANANDOA NI DHAMBI
Shalom wapendwa, Leo katika kona yetu hii ya Mahusiano, uchumba na Ndoa napenda tuangalie juu ya...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-06 20:56:12 0 6K
DEUTERONOMY
Verse by verse explanation of Deuteronomy 17
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 30 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-01-25 06:11:57 0 5K
EXODUS
Verse by verse explanation of Exodus 35
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 22 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-01-23 05:38:20 0 6K
MASWALI & MAJIBU
Mitume Wote Waliopita Walikuwa Ni Watu Weupe Hata Manabii Wote Waliopita Hadi Ma-Papa Ni Ngozi Nyeupe. Ni Kweli Ngozi Nyeusi Ililaaniwa ?
JIBU: Hakuna ngozi yoyote iliyolaaniwa, watu wote kwa Mungu ni sawa, Mungu hana upendeleo...
By GOSPEL PREACHER 2022-06-13 08:37:18 0 5K