JE, UNAWEZA KUOKOKA BILA YA KUPITIA YESU?

0
5K
Je naweza kuingia mbinguni bila kumkubali Yesu kama Bwana na Mwokozi wangu?
Jibu: Hapana, huwezi kwenda mbinguni kama unakataa kumkubali Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wako. Mambo manne ya kuzingatia kwenye jibu hili.
 
Haki: Mungu ni mwema, Mtakatifu, mwenye haki kwa watu wote (Waebrania 6:10). Mungu huwahukumu watu kwa kuzingatia ufahamu walio nao (Warumi 4:15; 5:13). Abraham hakujua jina la Yesu, lakini alimfuata Mungu na bado aliokolewa kupitia Yesu. (Yohana 8:56, Waebrania 9)
 
Njia moja tu: Hatuwezi kwenda mbinguni kwa kutegemea haki yetu wenyewe; tunahitaji rehema na neema za Mungu kupitia kwa Yesu. Yesu siyo tu njia ya kwendea kwa Mungu bali pia ni njia pekee ya kwendea kwa Mungu. (Yoh 14:6; 15:5; Matendo 4:12). Njia pekee ya kuifikia mbingu ya Mungu ni kupitia njia ya Mungu.
 
Ukimkataa Yesu kama Mwana wa Mungu utakuwa umeikataa mbingu: Hata kwa mtu anayeshika dini sana, Farisayo wa kiyahudi, Yesu alisema kuwa kama ukinikataa utakufa kwenye dhambi zako. (Yohana 8:24)
 
Mungu hutafuta: Mungu hapendi mtu yoyote aangamie (2 Petro 3:9), lakini kama Yeremia alivyowalilia watu wake (Yeremia 13:17; 14:17) na kama Yesu alivyoililia Yerusalem (Luka 19:41-44) na kama Petro alivyowasihi watu waliokuwa wanamsikiliza (Matendo 2:40), Mungu, huwatafuta watu wake kwa haja hiyo hiyo.
 
Ni mimi Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.
Shalom.
Căutare
Categorii
Citeste mai mult
GENESIS
Verse by verse explanation of Genesis 35
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 37 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-01-21 09:01:12 0 5K
Networking
Marketplace pricing: How to define your ideal take rate
As a marketplace owner, pricing is one of the most important decisions you need to make. This is...
By Business Academy 2022-09-17 03:26:58 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
KWA NINI YESU ALIVUNJA SABATO?
Ndugu msomaji, Hebu tuangalie mifano kadhaa hapa:   MFANO WA KWANZAYesu alipomponya mtu...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 22:34:44 0 6K
SPIRITUAL EDUCATION
MAANA HALISI YA IBADA YA KWELI
MAANA HALISI YA IBADA KWA UJUMLA. EBR 10:25 Ibada ni tendo la heshima ya hali ya juu...
By Martin Laizer 2025-11-05 04:57:48 0 527
Networking
How to communicate your marketplace value proposition
People's attention spans have become shorter. With the rapid growth in the number of online...
By Business Academy 2022-09-17 03:45:17 0 9K