JE, UNAWEZA KUOKOKA BILA YA KUPITIA YESU?

0
5KB
Je naweza kuingia mbinguni bila kumkubali Yesu kama Bwana na Mwokozi wangu?
Jibu: Hapana, huwezi kwenda mbinguni kama unakataa kumkubali Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wako. Mambo manne ya kuzingatia kwenye jibu hili.
 
Haki: Mungu ni mwema, Mtakatifu, mwenye haki kwa watu wote (Waebrania 6:10). Mungu huwahukumu watu kwa kuzingatia ufahamu walio nao (Warumi 4:15; 5:13). Abraham hakujua jina la Yesu, lakini alimfuata Mungu na bado aliokolewa kupitia Yesu. (Yohana 8:56, Waebrania 9)
 
Njia moja tu: Hatuwezi kwenda mbinguni kwa kutegemea haki yetu wenyewe; tunahitaji rehema na neema za Mungu kupitia kwa Yesu. Yesu siyo tu njia ya kwendea kwa Mungu bali pia ni njia pekee ya kwendea kwa Mungu. (Yoh 14:6; 15:5; Matendo 4:12). Njia pekee ya kuifikia mbingu ya Mungu ni kupitia njia ya Mungu.
 
Ukimkataa Yesu kama Mwana wa Mungu utakuwa umeikataa mbingu: Hata kwa mtu anayeshika dini sana, Farisayo wa kiyahudi, Yesu alisema kuwa kama ukinikataa utakufa kwenye dhambi zako. (Yohana 8:24)
 
Mungu hutafuta: Mungu hapendi mtu yoyote aangamie (2 Petro 3:9), lakini kama Yeremia alivyowalilia watu wake (Yeremia 13:17; 14:17) na kama Yesu alivyoililia Yerusalem (Luka 19:41-44) na kama Petro alivyowasihi watu waliokuwa wanamsikiliza (Matendo 2:40), Mungu, huwatafuta watu wake kwa haja hiyo hiyo.
 
Ni mimi Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.
Shalom.
Pesquisar
Categorias
Leia mais
GENESIS
GENESIS 1 : VERSE BY VERSE EXPLANATION
Verses 1:1 – 2:3: This description of God creating heaven and earth is understood to be:...
Por MOCARECI CHURCH 2021-12-05 22:43:49 0 7KB
LEVITICUS
Verse by verse explanation of Leviticus 8
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 154 questions at the...
Por THE HOLY BIBLE 2022-01-24 09:38:44 0 5KB
1 SAMUEL
Verse by verse explanation of 1 Samuel 1
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 44 questions at the...
Por THE HOLY BIBLE 2022-01-26 03:10:53 0 5KB
Injili Ya Yesu Kristo
Je ni nini kitawapata watu wale hawajawai pata nafasi ya kusikia kuhusu Yesu?
Je ni nini kitawapata watu wale hawajawai pata nafasi ya kusikia kuhusu Yesu? Je Mungu...
Por MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 04:11:03 0 5KB
BIBLICAL FINANCIAL EDUCATION
test
Jeremiah Chapter 48 Verses 1-47: The Moabites were descendants of Lot who lived east of the...
Por PROSHABO NETWORK 2021-12-31 18:31:29 0 8KB