JE, UNAWEZA KUOKOKA BILA YA KUPITIA YESU?
Δημοσιευμένα 2021-12-24 21:01:24
0
4χλμ.
Je naweza kuingia mbinguni bila kumkubali Yesu kama Bwana na Mwokozi wangu?
Jibu: Hapana, huwezi kwenda mbinguni kama unakataa kumkubali Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wako. Mambo manne ya kuzingatia kwenye jibu hili.
Haki: Mungu ni mwema, Mtakatifu, mwenye haki kwa watu wote (Waebrania 6:10). Mungu huwahukumu watu kwa kuzingatia ufahamu walio nao (Warumi 4:15; 5:13). Abraham hakujua jina la Yesu, lakini alimfuata Mungu na bado aliokolewa kupitia Yesu. (Yohana 8:56, Waebrania 9)
Njia moja tu: Hatuwezi kwenda mbinguni kwa kutegemea haki yetu wenyewe; tunahitaji rehema na neema za Mungu kupitia kwa Yesu. Yesu siyo tu njia ya kwendea kwa Mungu bali pia ni njia pekee ya kwendea kwa Mungu. (Yoh 14:6; 15:5; Matendo 4:12). Njia pekee ya kuifikia mbingu ya Mungu ni kupitia njia ya Mungu.
Ukimkataa Yesu kama Mwana wa Mungu utakuwa umeikataa mbingu: Hata kwa mtu anayeshika dini sana, Farisayo wa kiyahudi, Yesu alisema kuwa kama ukinikataa utakufa kwenye dhambi zako. (Yohana 8:24)
Mungu hutafuta: Mungu hapendi mtu yoyote aangamie (2 Petro 3:9), lakini kama Yeremia alivyowalilia watu wake (Yeremia 13:17; 14:17) na kama Yesu alivyoililia Yerusalem (Luka 19:41-44) na kama Petro alivyowasihi watu waliokuwa wanamsikiliza (Matendo 2:40), Mungu, huwatafuta watu wake kwa haja hiyo hiyo.
Ni mimi Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.
Shalom.
Αναζήτηση
Κατηγορίες
- BIBLICAL FINANCIAL EDUCATION
- SPIRITUAL EDUCATION
- MASWALI & MAJIBU
- WORLD'S EDUCATION
- MAHUSIANO KIBIBLIA
- Injili Ya Yesu Kristo
- OTHERS
Διαβάζω περισσότερα
KORAN INADAI KUWA YESU ALIZEEKEA HAPA DUNIANI.
VIOJA NDANI YA KORAN.KORAN INADAI KUWA YESU ALIZEEKEA HAPA DUNIANI.Leo tunajifunza Vioja vya...
Verse by verse explanation of Genesis 27
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 56 questions at the...
KWA NINI MUNGU ANATAKA TUENENDE KWA ROHO?
Ukisoma katika warumi 8:14 Biblia inasema “kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa...
Je! Wayahudi Wote Wataokolewa Kulingana Na Warumi 11:26?
SWALI: Je! Wayahudi wote wataokolewa? maana biblia inasema katika;
Warumi 11:25...
Verse by verse explanation of Ezra 1
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 29 questions at the...