Nawezaje kujazwa na Roho Mtakatifu?
Posted 2021-12-23 11:04:02
0
5K
Kifungu cha maana katika kuelewa juu ya kujazwa na Roho Mtakatifu in Yohana 14:16, mahali ampapo Yesu anaahidi kukaa kwa Roho Mtakatifu kwa wakristo, na huyo atadumu si kwa muda. Ni kitu cha maana kutofautisha kati ya kukaa kwa Roho Mtakatifu na kujazwa na Roho Mtakatifu. Kudumu kwa Roho Mtakatifu aupo kwa baadhi ya wakristo, bali ni kwa Wakristo wote. Kuna sehemu nyingi katika Bibilia zinazo pongeza huu msimamo wetu. Kwanza, Roho Mtakatifu ni zawadi iliyopewa Wakristo wote katika Kristo Yesu bila kupagua, na hakuna sheria za kutimiza ila tu ni kuwa na imani katika Kristo Yesu (Yohona 7:37-39). Pili, Roho Mtakatifu unapokewa wakati wa kuokoka (Waefeso 1:13). Wagalatia 3:2 inasisitiza ukweli huu pia, kwa kusema kwamba kutiwa muhuri na kujazwa na Roho Mtakatifu ulitokea wakati wa kuokoka. Tatu, Roho Mtakatifu unakaa kwa Wakristo milele. Wakristo wamepewa Roho Mtakatifu kama mtaji ama tibitisho la utukufu wao katika siku zijazo katika Kristo (2 Wakorintho 1:22; Waefeso 4:30).
Hili ni linganisho la kujazwa kwa Roho Mtakatifu ambao Waefeso 5:18 yazungumzia. Kikamilifu ni lazima tuzame katika Roho Mtakatifu ili atumiliki na katika hali hiyo atujaze. Warumi 8:9 na Waefeso 1:13-14 za sema kwamba anakaa kwa kila Mkristo, lakini anaweza kuhusunishwa (4:30), na kazi yake ndani yetu unaweza poa (1Wathesalonike 5:19). Wakati tunaruhusu haya kutokea hatuwezi kuhisi kikamilifu Roho Mtakatifu ukifanya kazi na nguvu zake ndani yetu. Kujazwa na Roho Mtakatifu haimaanishi tendo la nche pekee; pia yamaanisha tendo la kimawazo ambalo latutia moyo kwa kila tendo tutendalo. Zaburi 19:14 yasema, “Maneno ya kinywa changu, Na mawazo ya moyo wangu, Yapate kibali mbele zako, Ee BWANA, Mwamba wangu, na mwokozi wnagu.”
Dhambi ndiyo huzuia kujazwa kwa Roho Mtakatifu, na kumtii Mungu ndio njia pekee Roho anaweza kutunzwa. Waefeso 5:18 yatwaamuru kwamba tujazwe na Roho Mtakatifu; bali si kwa kuomba ili tujazwe na Roho Mtakatifu ambayo itawezesha kukamilisha kujazwa kwa Roho. Ni utiifu wetu wa sheria za Mungu wawezesha Roho kufanya kazi kwa huru ndani yetu. Kwa sababu tumeadhirika kwa dhambi, ni vigumu kujazwa na Roho wakati wote. Wakati twatenda dhambi ni lazima tutubu papo hapo kwa Mungu na tufanye upya mkataba wa kujazwa na Roho and kuongozwa na Roho Mtakatifu.
Search
Categories
- BIBLICAL FINANCIAL EDUCATION
- SPIRITUAL EDUCATION
- MASWALI & MAJIBU
- WORLD'S EDUCATION
- MAHUSIANO KIBIBLIA
- Injili Ya Yesu Kristo
- OTHERS
Read More
Verse by verse explanation of Joshua 21
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 27 questions at the...
Verse by verse explanation of Deuteronomy 25
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 19 questions at the...
MUHAMMAD ALIKUWA NA DHAMBI KUBWA KIASI CHA KUOMBA MSAMAHA MARA MIA KWA SIKU
Dhambi kubwa
Katika "Sahih Muslim, Kitabu 35, 6522 Idadi" inasema kwamba Muhammad alikuwa...
Watakaodanganywa Baada Ya Miaka 1000,Watatoka Wapi?
Swali linaendelea….Angali tunajua ndani ya ule utawala kutajawa na watakatifu tu? sasa...
UKWELI KUHUSU DUNIA YETU.
Watu walio wengi wanajua dunia yetu ina umbo la sphere yaani ipo flattened kwa top, sio duara...