JE, UNAWEZA KUOKOKA BILA YA KUPITIA YESU?

0
5K
Je naweza kuingia mbinguni bila kumkubali Yesu kama Bwana na Mwokozi wangu?
Jibu: Hapana, huwezi kwenda mbinguni kama unakataa kumkubali Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wako. Mambo manne ya kuzingatia kwenye jibu hili.
 
Haki: Mungu ni mwema, Mtakatifu, mwenye haki kwa watu wote (Waebrania 6:10). Mungu huwahukumu watu kwa kuzingatia ufahamu walio nao (Warumi 4:15; 5:13). Abraham hakujua jina la Yesu, lakini alimfuata Mungu na bado aliokolewa kupitia Yesu. (Yohana 8:56, Waebrania 9)
 
Njia moja tu: Hatuwezi kwenda mbinguni kwa kutegemea haki yetu wenyewe; tunahitaji rehema na neema za Mungu kupitia kwa Yesu. Yesu siyo tu njia ya kwendea kwa Mungu bali pia ni njia pekee ya kwendea kwa Mungu. (Yoh 14:6; 15:5; Matendo 4:12). Njia pekee ya kuifikia mbingu ya Mungu ni kupitia njia ya Mungu.
 
Ukimkataa Yesu kama Mwana wa Mungu utakuwa umeikataa mbingu: Hata kwa mtu anayeshika dini sana, Farisayo wa kiyahudi, Yesu alisema kuwa kama ukinikataa utakufa kwenye dhambi zako. (Yohana 8:24)
 
Mungu hutafuta: Mungu hapendi mtu yoyote aangamie (2 Petro 3:9), lakini kama Yeremia alivyowalilia watu wake (Yeremia 13:17; 14:17) na kama Yesu alivyoililia Yerusalem (Luka 19:41-44) na kama Petro alivyowasihi watu waliokuwa wanamsikiliza (Matendo 2:40), Mungu, huwatafuta watu wake kwa haja hiyo hiyo.
 
Ni mimi Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.
Shalom.
Pesquisar
Categorias
Leia Mais
MASWALI & MAJIBU
Je! kuna dhambi kubwa na ndogo?
SWALI: Naomba kufahamu Je! Kuna dhambi kubwa na ndogo, na kama hakuna je! Mtu aliyeua na...
Por GOSPEL PREACHER 2022-06-13 00:12:35 0 5K
GENESIS
Verse by verse explanation of Genesis 6
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 53 questions at the...
Por THE HOLY BIBLE 2022-01-03 04:34:43 0 5K
2 CHRONICLES
Verse by verse explanation of 2 Chronicles 14
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 23 questions at the...
Por THE HOLY BIBLE 2022-04-02 01:26:52 0 5K
UCHUMBA KIBIBLIA
HASARA ZA KUFANYA TENDO LA NDOA KABLA YA NDOA.
Andiko la Msingi ni Mithali 5:1-20. Mungu ndiye aliyewaumba mtu mume na mtu mke, akawaweka...
Por GOSPEL PREACHER 2021-11-23 07:16:45 0 9K
LEVITICUS
Verse by verse explanation of Leviticus 14
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 87 questions at the...
Por THE HOLY BIBLE 2022-01-24 10:10:45 0 5K