JE, UNAWEZA KUOKOKA BILA YA KUPITIA YESU?
نشر بتاريخ 2021-12-24 21:01:24
0
4كيلو بايت
Je naweza kuingia mbinguni bila kumkubali Yesu kama Bwana na Mwokozi wangu?
Jibu: Hapana, huwezi kwenda mbinguni kama unakataa kumkubali Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wako. Mambo manne ya kuzingatia kwenye jibu hili.
Haki: Mungu ni mwema, Mtakatifu, mwenye haki kwa watu wote (Waebrania 6:10). Mungu huwahukumu watu kwa kuzingatia ufahamu walio nao (Warumi 4:15; 5:13). Abraham hakujua jina la Yesu, lakini alimfuata Mungu na bado aliokolewa kupitia Yesu. (Yohana 8:56, Waebrania 9)
Njia moja tu: Hatuwezi kwenda mbinguni kwa kutegemea haki yetu wenyewe; tunahitaji rehema na neema za Mungu kupitia kwa Yesu. Yesu siyo tu njia ya kwendea kwa Mungu bali pia ni njia pekee ya kwendea kwa Mungu. (Yoh 14:6; 15:5; Matendo 4:12). Njia pekee ya kuifikia mbingu ya Mungu ni kupitia njia ya Mungu.
Ukimkataa Yesu kama Mwana wa Mungu utakuwa umeikataa mbingu: Hata kwa mtu anayeshika dini sana, Farisayo wa kiyahudi, Yesu alisema kuwa kama ukinikataa utakufa kwenye dhambi zako. (Yohana 8:24)
Mungu hutafuta: Mungu hapendi mtu yoyote aangamie (2 Petro 3:9), lakini kama Yeremia alivyowalilia watu wake (Yeremia 13:17; 14:17) na kama Yesu alivyoililia Yerusalem (Luka 19:41-44) na kama Petro alivyowasihi watu waliokuwa wanamsikiliza (Matendo 2:40), Mungu, huwatafuta watu wake kwa haja hiyo hiyo.
Ni mimi Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.
Shalom.
البحث
الأقسام
- BIBLICAL FINANCIAL EDUCATION
- SPIRITUAL EDUCATION
- MASWALI & MAJIBU
- WORLD'S EDUCATION
- MAHUSIANO KIBIBLIA
- Injili Ya Yesu Kristo
- OTHERS
إقرأ المزيد
The difference between an invoice and a bill
‘Invoice’ and ‘bill’ are two terms that are often...
FURAHA YA BWANA NI NGUVU ZAKO.
Mpendwa wangu nina kusalimu katika Jina lipitalo majina yote, Yesu Kristo Mwana wa Mungu Aliye...
KWANINI MUHAMMAD ALIKUWA NA TABIA KAMA ZA WANAWAKE?
1. APAKA WANJA NA PODA KAMA WANAWAKE.2. ACHUCHUMAA WAKATI WA HAJA NDOGO.3. ALIVAA MAGAUNI YA WAKE...
Urithi wa Uislamu kutoka kwenye dini za kipagani za Uarabuni
SEHEMU YA 1
Allah alitokea wapi?
Uislamu unajinadi kwamba Allah ndiye Mungu yuleyule...
HAKIMU ALIYE TOFAUTI NA MAHAKIMU WOTE
Neno la Uzima kutoka kwa Askofu Zachary...