JE, UNAWEZA KUOKOKA BILA YA KUPITIA YESU?

0
5K
Je naweza kuingia mbinguni bila kumkubali Yesu kama Bwana na Mwokozi wangu?
Jibu: Hapana, huwezi kwenda mbinguni kama unakataa kumkubali Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wako. Mambo manne ya kuzingatia kwenye jibu hili.
 
Haki: Mungu ni mwema, Mtakatifu, mwenye haki kwa watu wote (Waebrania 6:10). Mungu huwahukumu watu kwa kuzingatia ufahamu walio nao (Warumi 4:15; 5:13). Abraham hakujua jina la Yesu, lakini alimfuata Mungu na bado aliokolewa kupitia Yesu. (Yohana 8:56, Waebrania 9)
 
Njia moja tu: Hatuwezi kwenda mbinguni kwa kutegemea haki yetu wenyewe; tunahitaji rehema na neema za Mungu kupitia kwa Yesu. Yesu siyo tu njia ya kwendea kwa Mungu bali pia ni njia pekee ya kwendea kwa Mungu. (Yoh 14:6; 15:5; Matendo 4:12). Njia pekee ya kuifikia mbingu ya Mungu ni kupitia njia ya Mungu.
 
Ukimkataa Yesu kama Mwana wa Mungu utakuwa umeikataa mbingu: Hata kwa mtu anayeshika dini sana, Farisayo wa kiyahudi, Yesu alisema kuwa kama ukinikataa utakufa kwenye dhambi zako. (Yohana 8:24)
 
Mungu hutafuta: Mungu hapendi mtu yoyote aangamie (2 Petro 3:9), lakini kama Yeremia alivyowalilia watu wake (Yeremia 13:17; 14:17) na kama Yesu alivyoililia Yerusalem (Luka 19:41-44) na kama Petro alivyowasihi watu waliokuwa wanamsikiliza (Matendo 2:40), Mungu, huwatafuta watu wake kwa haja hiyo hiyo.
 
Ni mimi Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.
Shalom.
Buscar
Categorías
Read More
Injili Ya Yesu Kristo
UBATIZO WA MAJI MENGI.
Na Mch.Madumla ( wa katikati mbele) Bwana Yesu asifiwe… Kwa ufupi; Miaka fulani nilipata...
By GOSPEL PREACHER 2022-03-29 23:44:15 0 6K
MASWALI & MAJIBU
Je! Dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu ni ipi?
SWALI : Dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu ni ipi? JIBU: Tukisoma; Mathayo 12:25-32 ”...
By GOSPEL PREACHER 2022-06-13 00:19:41 0 6K
JOSHUA
Verse by verse explanation of Joshua 9
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 30 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-01-25 07:30:25 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
YESU ALIBADILI MWENENDO WA HISTORIA YOTE
Tembea sehemu yoyote ulimwenguni. Ongea na watu wa dini yoyote. Haijalishi jinsi walivyoshikilia...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 21:16:46 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
KWA NAMNA GANI MTU ANAWEZA KUMZIMISHA ROHO MTAKATIFU?
Roho Mtakatifu ni Mungu, mwenye nguvu zote, maarifa yote, anayepatikana kila mahali. Yeye pia...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-23 12:55:47 2 5K