JE, UNAWEZA KUOKOKA BILA YA KUPITIA YESU?
Posted 2021-12-24 21:01:24
0
5K
Je naweza kuingia mbinguni bila kumkubali Yesu kama Bwana na Mwokozi wangu?
Jibu: Hapana, huwezi kwenda mbinguni kama unakataa kumkubali Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wako. Mambo manne ya kuzingatia kwenye jibu hili.
Haki: Mungu ni mwema, Mtakatifu, mwenye haki kwa watu wote (Waebrania 6:10). Mungu huwahukumu watu kwa kuzingatia ufahamu walio nao (Warumi 4:15; 5:13). Abraham hakujua jina la Yesu, lakini alimfuata Mungu na bado aliokolewa kupitia Yesu. (Yohana 8:56, Waebrania 9)
Njia moja tu: Hatuwezi kwenda mbinguni kwa kutegemea haki yetu wenyewe; tunahitaji rehema na neema za Mungu kupitia kwa Yesu. Yesu siyo tu njia ya kwendea kwa Mungu bali pia ni njia pekee ya kwendea kwa Mungu. (Yoh 14:6; 15:5; Matendo 4:12). Njia pekee ya kuifikia mbingu ya Mungu ni kupitia njia ya Mungu.
Ukimkataa Yesu kama Mwana wa Mungu utakuwa umeikataa mbingu: Hata kwa mtu anayeshika dini sana, Farisayo wa kiyahudi, Yesu alisema kuwa kama ukinikataa utakufa kwenye dhambi zako. (Yohana 8:24)
Mungu hutafuta: Mungu hapendi mtu yoyote aangamie (2 Petro 3:9), lakini kama Yeremia alivyowalilia watu wake (Yeremia 13:17; 14:17) na kama Yesu alivyoililia Yerusalem (Luka 19:41-44) na kama Petro alivyowasihi watu waliokuwa wanamsikiliza (Matendo 2:40), Mungu, huwatafuta watu wake kwa haja hiyo hiyo.
Ni mimi Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.
Shalom.
Zoeken
Categorieën
- BIBLICAL FINANCIAL EDUCATION
- SPIRITUAL EDUCATION
- MASWALI & MAJIBU
- WORLD'S EDUCATION
- MAHUSIANO KIBIBLIA
- Injili Ya Yesu Kristo
- OTHERS
Read More
Verse by verse explanation of Deuteronomy 25
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 19 questions at the...
Book of 1 Samuel Explained
Title: The books of Samuel were originally one book in the Hebrew Canon. The single volume...
Verse by verse explanation of Genesis 39
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 25 questions at the...
Verse by verse explanation of Deuteronomy 32
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 62 questions at the...
ROHO MTAKATIFU
Ndugu msomaji;
Je, unamfahamu Roho Mtakatifu?
Je, Roho Mtakatifu ni nani kwako?
Katika...