JE, UNAWEZA KUOKOKA BILA YA KUPITIA YESU?

0
4Кб
Je naweza kuingia mbinguni bila kumkubali Yesu kama Bwana na Mwokozi wangu?
Jibu: Hapana, huwezi kwenda mbinguni kama unakataa kumkubali Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wako. Mambo manne ya kuzingatia kwenye jibu hili.
 
Haki: Mungu ni mwema, Mtakatifu, mwenye haki kwa watu wote (Waebrania 6:10). Mungu huwahukumu watu kwa kuzingatia ufahamu walio nao (Warumi 4:15; 5:13). Abraham hakujua jina la Yesu, lakini alimfuata Mungu na bado aliokolewa kupitia Yesu. (Yohana 8:56, Waebrania 9)
 
Njia moja tu: Hatuwezi kwenda mbinguni kwa kutegemea haki yetu wenyewe; tunahitaji rehema na neema za Mungu kupitia kwa Yesu. Yesu siyo tu njia ya kwendea kwa Mungu bali pia ni njia pekee ya kwendea kwa Mungu. (Yoh 14:6; 15:5; Matendo 4:12). Njia pekee ya kuifikia mbingu ya Mungu ni kupitia njia ya Mungu.
 
Ukimkataa Yesu kama Mwana wa Mungu utakuwa umeikataa mbingu: Hata kwa mtu anayeshika dini sana, Farisayo wa kiyahudi, Yesu alisema kuwa kama ukinikataa utakufa kwenye dhambi zako. (Yohana 8:24)
 
Mungu hutafuta: Mungu hapendi mtu yoyote aangamie (2 Petro 3:9), lakini kama Yeremia alivyowalilia watu wake (Yeremia 13:17; 14:17) na kama Yesu alivyoililia Yerusalem (Luka 19:41-44) na kama Petro alivyowasihi watu waliokuwa wanamsikiliza (Matendo 2:40), Mungu, huwatafuta watu wake kwa haja hiyo hiyo.
 
Ni mimi Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.
Shalom.
Поиск
Категории
Больше
PSALMS
Verse by verse explanation of Psalm 6
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 31 questions at the...
От THE HOLY BIBLE 2022-04-04 23:12:00 0 5Кб
1 KINGS
Verse by verse explanation of 1 Kings 15
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 39 questions at the...
От THE HOLY BIBLE 2022-02-05 13:56:33 0 5Кб
Injili Ya Yesu Kristo
JIANDAE KUFA KIFO KIZURI.
‘Maadam unaishi, lazima utakufa pia, hata kama hupendi kufa, kifo ni sehemu ya maisha na...
От GOSPEL PREACHER 2021-11-23 12:46:10 0 5Кб
Injili Ya Yesu Kristo
Ukombozi wa Kiroho Unafanywaje kwa Mafanikio?
Ukombozi wa Kiroho, kwa watu wanaomwamini Mungu, ni jambo la maana sana, kwa kuwa wanafikiri...
От PROSPER HABONA 2022-04-16 11:34:22 0 5Кб
2 SAMUEL
Verse by verse explanation of 2 Samuel 18
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 35 questions at the...
От THE HOLY BIBLE 2022-02-05 09:59:42 0 5Кб