JE, UNAWEZA KUOKOKA BILA YA KUPITIA YESU?

0
5KB
Je naweza kuingia mbinguni bila kumkubali Yesu kama Bwana na Mwokozi wangu?
Jibu: Hapana, huwezi kwenda mbinguni kama unakataa kumkubali Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wako. Mambo manne ya kuzingatia kwenye jibu hili.
 
Haki: Mungu ni mwema, Mtakatifu, mwenye haki kwa watu wote (Waebrania 6:10). Mungu huwahukumu watu kwa kuzingatia ufahamu walio nao (Warumi 4:15; 5:13). Abraham hakujua jina la Yesu, lakini alimfuata Mungu na bado aliokolewa kupitia Yesu. (Yohana 8:56, Waebrania 9)
 
Njia moja tu: Hatuwezi kwenda mbinguni kwa kutegemea haki yetu wenyewe; tunahitaji rehema na neema za Mungu kupitia kwa Yesu. Yesu siyo tu njia ya kwendea kwa Mungu bali pia ni njia pekee ya kwendea kwa Mungu. (Yoh 14:6; 15:5; Matendo 4:12). Njia pekee ya kuifikia mbingu ya Mungu ni kupitia njia ya Mungu.
 
Ukimkataa Yesu kama Mwana wa Mungu utakuwa umeikataa mbingu: Hata kwa mtu anayeshika dini sana, Farisayo wa kiyahudi, Yesu alisema kuwa kama ukinikataa utakufa kwenye dhambi zako. (Yohana 8:24)
 
Mungu hutafuta: Mungu hapendi mtu yoyote aangamie (2 Petro 3:9), lakini kama Yeremia alivyowalilia watu wake (Yeremia 13:17; 14:17) na kama Yesu alivyoililia Yerusalem (Luka 19:41-44) na kama Petro alivyowasihi watu waliokuwa wanamsikiliza (Matendo 2:40), Mungu, huwatafuta watu wake kwa haja hiyo hiyo.
 
Ni mimi Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.
Shalom.
Suche
Kategorien
Mehr lesen
OTHERS
UNAJUA KWANINI WAISLAM WANAMSWALIA MUHAMMAD KILA SIKU?
KWASABABU MUHAMMAD ALIKUFA NA DHAMBI NYINGI SANA KULIKO KIUMBE CHOCHOTE KILE.   Katika...
Von MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 21:37:38 0 5KB
2 SAMUEL
Verse by verse explanation of 2 Samuel 7
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 29 questions at the...
Von THE HOLY BIBLE 2022-02-05 09:26:36 0 5KB
Injili Ya Yesu Kristo
KWA NINI TUMEOKOKA?
Bwana YESU atukuzwe ndugu zangu wote. Karibuni tujifunze Neno la MUNGU la uzima wetu sasa na...
Von GOSPEL PREACHER 2021-11-06 09:38:24 0 6KB
EZRA
Book of Ezra Explained
Book of Ezra “Title”: Even though Ezra’s name does not enter the account...
Von THE HOLY BIBLE 2022-04-02 06:01:46 0 6KB
SPIRITUAL EDUCATION
NINI MATARAJIO YA MUNGU KWA VIJANA?
1 Yohana 2:14 “…. Nimewaandikia ninyi,vijana kwa sababu mna nguvu,na neno la Mungu...
Von GOSPEL PREACHER 2021-11-23 07:29:25 0 5KB