WANAWAKE KUMTUMIKIA MUNGU

0
5K
Ni uongo wa Shetani kwamba wanawake hawawezi kuwa Watumishi wa Mungu, wakahubiri, wakafundisha, wakatoa pepo au kumtumikia Mungu kwa namna nyinginezo.  Wanawake kumtumikia Mungu, ni jambo la Ki-Biblia hasa. 
 
Nyakati hizi za mwisho, Roho wa Mungu atamwagwa kwa WOTE, binti watatabiri (kuhubiri ni kutabiri pia) na Roho huyu wa Mungu atamwagwa kwa WATUMISHI WA MUNGU WANAUME NA WANAWAKE (MATENDO 2:17-18).  
 
Nyakati za Kanisa la Kwanza, wanaume na wanawake, wote walikuwa watendakazi, wakilihubiri Neno na kulifundisha (MATENDO 8: 1, 4).  Inatupasa kufuata mfumo huu wa ki-Biblia.  Mara kwa mara, katika Biblia, wanawake, wamekuwa na ujasiri wa kumtumikia Mungu na kuwa wanyenyekevu na watii kwa Yesu Kristo na Neno lake, kuliko wanaume.  Hapa tunaona wanawake waliomfuata Yesu kutoka Galilaya, karibu maili 100 kutoka Yerusalemu, wakija kumtumikia Yesu.  Hapa msalabani, hawakuwako wanafunzi wale kumi na moja wa Yesu kasoro Yohana (YOHANA 19: 25-26).  Wengi walikuwa wanawake waliokuwa wakijipiga vifua na kumwombolezea (LUKA 23:27).  
 
Wanawake walikuwepo msalabani mpaka mwisho na tena walikuwapo kwenye mazishi yake (MST 61) na pia wanawake ndiyo waliokuwa wa kwanza kwenda kulitazama kaburi siku ya kufufuka kwa Yesu (MATHAYO 28:1).  Mwanamke ndiye aliyewapelekea habari za kufufuka kwa Yesu, Petro na Yohana, na kuwatia moyo, NDIPO nao wakachangamka!  Hapo mwanzo, walikuwa wamekata tamaa na kwenda kuvua samaki (YOHANA 20:1-3; 21:1-3).  
 
Mwanamke Priska au Prisila alikuwa tayari kukatwa kichwa kwa ajili ya Injili aliyokuwa anaihubiri Paulo na Mwanamke Fibi aliwasaidia wengi mno (WARUMI 16:1-3).  Shime wanawake, tutende kazi ya Bwana! Wanaume pia tupate changamoto kwa watendakazi wanawake ambao wanatenda kazi ya Mungu kwa bidii pamoja na majukumu mengi ya kifamilia waliyo nayo.
Site içinde arama yapın
Kategoriler
Read More
NUMBERS
Verse by verse explanation of Numbers 30
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 17 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-01-24 15:25:37 0 6K
NDOA KIBIBLIA
SHAMBA LA MTU MVIVU, ASIYE NA AKLI: MAHUSIANO YA NDOA (NA UCHUMBA)
MAHUSIANO: SHAMBA LA MTU MVIVU, ASIYE NA AKLI(Uvivu na Kukosa Akili Kichocheo Cha...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-07 23:23:24 0 5K
NDOA KIBIBLIA
CHANZO CHA MATATIZO KATIKA NDOA
USIMWEKE MBALI NAWEMaisha ya mume na mke ni maisha yasiyokuwa na nafasi katikati inayowaweka...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-07 22:56:29 0 7K
OTHERS
Kwa Nini Niliacha Uislamu na Kumpokea Yesu?
Mutee'a Al-Fadi alikuwa ni Mwislamu mwenye msimamo mkali wa Wahabbi ambao alisomea kule Saudi...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 09:30:32 0 5K
LEVITICUS
Verse by verse explanation of Leviticus 21
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 30 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-01-24 10:27:13 0 5K