WANAWAKE KUMTUMIKIA MUNGU

0
5KB
Ni uongo wa Shetani kwamba wanawake hawawezi kuwa Watumishi wa Mungu, wakahubiri, wakafundisha, wakatoa pepo au kumtumikia Mungu kwa namna nyinginezo.  Wanawake kumtumikia Mungu, ni jambo la Ki-Biblia hasa. 
 
Nyakati hizi za mwisho, Roho wa Mungu atamwagwa kwa WOTE, binti watatabiri (kuhubiri ni kutabiri pia) na Roho huyu wa Mungu atamwagwa kwa WATUMISHI WA MUNGU WANAUME NA WANAWAKE (MATENDO 2:17-18).  
 
Nyakati za Kanisa la Kwanza, wanaume na wanawake, wote walikuwa watendakazi, wakilihubiri Neno na kulifundisha (MATENDO 8: 1, 4).  Inatupasa kufuata mfumo huu wa ki-Biblia.  Mara kwa mara, katika Biblia, wanawake, wamekuwa na ujasiri wa kumtumikia Mungu na kuwa wanyenyekevu na watii kwa Yesu Kristo na Neno lake, kuliko wanaume.  Hapa tunaona wanawake waliomfuata Yesu kutoka Galilaya, karibu maili 100 kutoka Yerusalemu, wakija kumtumikia Yesu.  Hapa msalabani, hawakuwako wanafunzi wale kumi na moja wa Yesu kasoro Yohana (YOHANA 19: 25-26).  Wengi walikuwa wanawake waliokuwa wakijipiga vifua na kumwombolezea (LUKA 23:27).  
 
Wanawake walikuwepo msalabani mpaka mwisho na tena walikuwapo kwenye mazishi yake (MST 61) na pia wanawake ndiyo waliokuwa wa kwanza kwenda kulitazama kaburi siku ya kufufuka kwa Yesu (MATHAYO 28:1).  Mwanamke ndiye aliyewapelekea habari za kufufuka kwa Yesu, Petro na Yohana, na kuwatia moyo, NDIPO nao wakachangamka!  Hapo mwanzo, walikuwa wamekata tamaa na kwenda kuvua samaki (YOHANA 20:1-3; 21:1-3).  
 
Mwanamke Priska au Prisila alikuwa tayari kukatwa kichwa kwa ajili ya Injili aliyokuwa anaihubiri Paulo na Mwanamke Fibi aliwasaidia wengi mno (WARUMI 16:1-3).  Shime wanawake, tutende kazi ya Bwana! Wanaume pia tupate changamoto kwa watendakazi wanawake ambao wanatenda kazi ya Mungu kwa bidii pamoja na majukumu mengi ya kifamilia waliyo nayo.
Suche
Kategorien
Mehr lesen
JUDGES
Verse by verse explanation of Judges 12
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 28 questions at the...
Von THE HOLY BIBLE 2022-01-25 11:01:07 0 5KB
Injili Ya Yesu Kristo
JINSI YA KUISHINDA DHAMBI JUMLA
Kubali Kwamba Umeitenda Hiyo Dhambi, Na Usijaribu Kutafuta ANDIKO LA KUJIHAMI, Au MTU WA...
Von GOSPEL PREACHER 2021-11-19 07:12:46 0 5KB
1 SAMUEL
Verse by verse explanation of 1 Samuel 12
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 33 questions at the...
Von THE HOLY BIBLE 2022-01-26 03:40:06 0 5KB
OTHERS
Kwanini Mkristo anauhakika wa kwenda Paradiso zaidi ya Muislamu?
1. Je, Kurani inatoa uhakika kwa Waislamu? Kurani inatengeneza tu mazingira ya mashaka kuhusiana...
Von MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 06:26:41 0 4KB
GENESIS
Verse by verse explanation of Genesis 22
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 28 questions at the...
Von THE HOLY BIBLE 2022-01-21 05:53:18 0 5KB