WANAWAKE KUMTUMIKIA MUNGU

0
5K
Ni uongo wa Shetani kwamba wanawake hawawezi kuwa Watumishi wa Mungu, wakahubiri, wakafundisha, wakatoa pepo au kumtumikia Mungu kwa namna nyinginezo.  Wanawake kumtumikia Mungu, ni jambo la Ki-Biblia hasa. 
 
Nyakati hizi za mwisho, Roho wa Mungu atamwagwa kwa WOTE, binti watatabiri (kuhubiri ni kutabiri pia) na Roho huyu wa Mungu atamwagwa kwa WATUMISHI WA MUNGU WANAUME NA WANAWAKE (MATENDO 2:17-18).  
 
Nyakati za Kanisa la Kwanza, wanaume na wanawake, wote walikuwa watendakazi, wakilihubiri Neno na kulifundisha (MATENDO 8: 1, 4).  Inatupasa kufuata mfumo huu wa ki-Biblia.  Mara kwa mara, katika Biblia, wanawake, wamekuwa na ujasiri wa kumtumikia Mungu na kuwa wanyenyekevu na watii kwa Yesu Kristo na Neno lake, kuliko wanaume.  Hapa tunaona wanawake waliomfuata Yesu kutoka Galilaya, karibu maili 100 kutoka Yerusalemu, wakija kumtumikia Yesu.  Hapa msalabani, hawakuwako wanafunzi wale kumi na moja wa Yesu kasoro Yohana (YOHANA 19: 25-26).  Wengi walikuwa wanawake waliokuwa wakijipiga vifua na kumwombolezea (LUKA 23:27).  
 
Wanawake walikuwepo msalabani mpaka mwisho na tena walikuwapo kwenye mazishi yake (MST 61) na pia wanawake ndiyo waliokuwa wa kwanza kwenda kulitazama kaburi siku ya kufufuka kwa Yesu (MATHAYO 28:1).  Mwanamke ndiye aliyewapelekea habari za kufufuka kwa Yesu, Petro na Yohana, na kuwatia moyo, NDIPO nao wakachangamka!  Hapo mwanzo, walikuwa wamekata tamaa na kwenda kuvua samaki (YOHANA 20:1-3; 21:1-3).  
 
Mwanamke Priska au Prisila alikuwa tayari kukatwa kichwa kwa ajili ya Injili aliyokuwa anaihubiri Paulo na Mwanamke Fibi aliwasaidia wengi mno (WARUMI 16:1-3).  Shime wanawake, tutende kazi ya Bwana! Wanaume pia tupate changamoto kwa watendakazi wanawake ambao wanatenda kazi ya Mungu kwa bidii pamoja na majukumu mengi ya kifamilia waliyo nayo.
Zoeken
Categorieën
Read More
Injili Ya Yesu Kristo
Je! Mkristo anaweza pagagwa na Mapepo?
Bibilia kwa ukamilifu haitaji kama Mkristo anaweza shikwa na pepo. Ingagwa, kwa vile Mkristo...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 04:05:56 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
HAKIMU ALIYE TOFAUTI NA MAHAKIMU WOTE
Neno la Uzima kutoka kwa  Askofu Zachary...
By GOSPEL PREACHER 2022-01-12 01:34:25 0 5K
CHRISTIAN EDUCATION
JE! NI HAKI WATAKATIFU WALIOKUFA KUTUOMBEA SISI WATAKATIFU TULIO DUNIANI?
JE NI HAKI WATAKATIFU WALIOKUFA KUTUOMBEA SISI WATAKATIFU TULIO DUNIANI?
By Martin Laizer 2024-01-24 10:41:33 3 6K
Injili Ya Yesu Kristo
JINSI YA KUWASHINDA MAPEPO
Mstari wa Msingi  Waefeso 6:12 “Kwa maana kushindana (Struggle NIV,...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-06 00:58:05 0 9K
SPIRITUAL EDUCATION
HAZINA YA MTU
PALIPO NA HAZINA YA MTU NDIPO NA MOYO WAKE UTAKAPOKUWA 
By Martin Laizer 2023-09-25 06:09:55 0 12K