WANAWAKE KUMTUMIKIA MUNGU

0
5χλμ.
Ni uongo wa Shetani kwamba wanawake hawawezi kuwa Watumishi wa Mungu, wakahubiri, wakafundisha, wakatoa pepo au kumtumikia Mungu kwa namna nyinginezo.  Wanawake kumtumikia Mungu, ni jambo la Ki-Biblia hasa. 
 
Nyakati hizi za mwisho, Roho wa Mungu atamwagwa kwa WOTE, binti watatabiri (kuhubiri ni kutabiri pia) na Roho huyu wa Mungu atamwagwa kwa WATUMISHI WA MUNGU WANAUME NA WANAWAKE (MATENDO 2:17-18).  
 
Nyakati za Kanisa la Kwanza, wanaume na wanawake, wote walikuwa watendakazi, wakilihubiri Neno na kulifundisha (MATENDO 8: 1, 4).  Inatupasa kufuata mfumo huu wa ki-Biblia.  Mara kwa mara, katika Biblia, wanawake, wamekuwa na ujasiri wa kumtumikia Mungu na kuwa wanyenyekevu na watii kwa Yesu Kristo na Neno lake, kuliko wanaume.  Hapa tunaona wanawake waliomfuata Yesu kutoka Galilaya, karibu maili 100 kutoka Yerusalemu, wakija kumtumikia Yesu.  Hapa msalabani, hawakuwako wanafunzi wale kumi na moja wa Yesu kasoro Yohana (YOHANA 19: 25-26).  Wengi walikuwa wanawake waliokuwa wakijipiga vifua na kumwombolezea (LUKA 23:27).  
 
Wanawake walikuwepo msalabani mpaka mwisho na tena walikuwapo kwenye mazishi yake (MST 61) na pia wanawake ndiyo waliokuwa wa kwanza kwenda kulitazama kaburi siku ya kufufuka kwa Yesu (MATHAYO 28:1).  Mwanamke ndiye aliyewapelekea habari za kufufuka kwa Yesu, Petro na Yohana, na kuwatia moyo, NDIPO nao wakachangamka!  Hapo mwanzo, walikuwa wamekata tamaa na kwenda kuvua samaki (YOHANA 20:1-3; 21:1-3).  
 
Mwanamke Priska au Prisila alikuwa tayari kukatwa kichwa kwa ajili ya Injili aliyokuwa anaihubiri Paulo na Mwanamke Fibi aliwasaidia wengi mno (WARUMI 16:1-3).  Shime wanawake, tutende kazi ya Bwana! Wanaume pia tupate changamoto kwa watendakazi wanawake ambao wanatenda kazi ya Mungu kwa bidii pamoja na majukumu mengi ya kifamilia waliyo nayo.
Αναζήτηση
Κατηγορίες
Διαβάζω περισσότερα
JUDGES
Book of Judges Explained
Title: The book bears the fitting name “Judges,” which refers to unique leaders...
από THE HOLY BIBLE 2022-01-25 08:58:35 0 5χλμ.
NEHEMIAH
Verse by verse explanation of Nehemiah 9
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 31 questions at the...
από THE HOLY BIBLE 2022-04-02 12:31:44 0 6χλμ.
REVELATION
UFUNUO 12
MAELEZO JUU YA “UFUNUO 12” Ufunuo 12 1 Na ishara kuu ilionekana mbinguni;...
από GOSPEL PREACHER 2021-10-30 11:35:41 0 5χλμ.
Injili Ya Yesu Kristo
Yesu ni Mungu
Je, Yesu Kristo ni Mungu?Hebu tuanzie kutafiti ukweli wa hili swali, Je Yesu ni Mungu, kabla ya...
από MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 10:42:49 0 5χλμ.
1 KINGS
Verse by verse explanation of 1 Kings 4
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 37 questions at the...
από THE HOLY BIBLE 2022-02-05 12:32:39 0 5χλμ.