WANAWAKE KUMTUMIKIA MUNGU

0
5كيلو بايت
Ni uongo wa Shetani kwamba wanawake hawawezi kuwa Watumishi wa Mungu, wakahubiri, wakafundisha, wakatoa pepo au kumtumikia Mungu kwa namna nyinginezo.  Wanawake kumtumikia Mungu, ni jambo la Ki-Biblia hasa. 
 
Nyakati hizi za mwisho, Roho wa Mungu atamwagwa kwa WOTE, binti watatabiri (kuhubiri ni kutabiri pia) na Roho huyu wa Mungu atamwagwa kwa WATUMISHI WA MUNGU WANAUME NA WANAWAKE (MATENDO 2:17-18).  
 
Nyakati za Kanisa la Kwanza, wanaume na wanawake, wote walikuwa watendakazi, wakilihubiri Neno na kulifundisha (MATENDO 8: 1, 4).  Inatupasa kufuata mfumo huu wa ki-Biblia.  Mara kwa mara, katika Biblia, wanawake, wamekuwa na ujasiri wa kumtumikia Mungu na kuwa wanyenyekevu na watii kwa Yesu Kristo na Neno lake, kuliko wanaume.  Hapa tunaona wanawake waliomfuata Yesu kutoka Galilaya, karibu maili 100 kutoka Yerusalemu, wakija kumtumikia Yesu.  Hapa msalabani, hawakuwako wanafunzi wale kumi na moja wa Yesu kasoro Yohana (YOHANA 19: 25-26).  Wengi walikuwa wanawake waliokuwa wakijipiga vifua na kumwombolezea (LUKA 23:27).  
 
Wanawake walikuwepo msalabani mpaka mwisho na tena walikuwapo kwenye mazishi yake (MST 61) na pia wanawake ndiyo waliokuwa wa kwanza kwenda kulitazama kaburi siku ya kufufuka kwa Yesu (MATHAYO 28:1).  Mwanamke ndiye aliyewapelekea habari za kufufuka kwa Yesu, Petro na Yohana, na kuwatia moyo, NDIPO nao wakachangamka!  Hapo mwanzo, walikuwa wamekata tamaa na kwenda kuvua samaki (YOHANA 20:1-3; 21:1-3).  
 
Mwanamke Priska au Prisila alikuwa tayari kukatwa kichwa kwa ajili ya Injili aliyokuwa anaihubiri Paulo na Mwanamke Fibi aliwasaidia wengi mno (WARUMI 16:1-3).  Shime wanawake, tutende kazi ya Bwana! Wanaume pia tupate changamoto kwa watendakazi wanawake ambao wanatenda kazi ya Mungu kwa bidii pamoja na majukumu mengi ya kifamilia waliyo nayo.
البحث
الأقسام
إقرأ المزيد
Injili Ya Yesu Kristo
IPONYE NAFSI YAKO, EPUKA MANABII WA UONGO
Muhubiri/ Mtumishi yeyote aliyerudi nyuma na kusahau kusudi lake tayari anageuka kuwa nabii wa...
بواسطة GOSPEL PREACHER 2023-06-17 23:43:15 0 8كيلو بايت
2 SAMUEL
Verse by verse explanation of 2 Samuel 14
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 27 questions at the...
بواسطة THE HOLY BIBLE 2022-02-05 09:49:47 0 5كيلو بايت
OTHERS
UTATA: NUHU WA QURAN NI TOFAUTI NA NUHU WA BIBLIA
Ndugu Msomaji: Siku zote Waislam huwa mnatutambia kuwa, Quran ni kitabu kilichoeleza kila...
بواسطة MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 03:30:49 0 5كيلو بايت
SPIRITUAL EDUCATION
KONA YA USHAURI
VITU MUHIMU AMBAVYO KILA MSHAURI ANATAKIWA KUVIJUA ILI AWE MSHAURI MZURI.  
بواسطة Martin Laizer 2023-09-30 01:49:06 2 7كيلو بايت
Injili Ya Yesu Kristo
KILA ATAKAYELIITIA JINA LA BWANA ATAOKOKA.
Kwa ufupi.. Bwana Yesu asifiwe… `` Kwa kuwa,kila atakayeliitia Jina la Bwana...
بواسطة GOSPEL PREACHER 2022-03-30 05:01:07 0 5كيلو بايت