WANAWAKE KUMTUMIKIA MUNGU

0
5كيلو بايت
Ni uongo wa Shetani kwamba wanawake hawawezi kuwa Watumishi wa Mungu, wakahubiri, wakafundisha, wakatoa pepo au kumtumikia Mungu kwa namna nyinginezo.  Wanawake kumtumikia Mungu, ni jambo la Ki-Biblia hasa. 
 
Nyakati hizi za mwisho, Roho wa Mungu atamwagwa kwa WOTE, binti watatabiri (kuhubiri ni kutabiri pia) na Roho huyu wa Mungu atamwagwa kwa WATUMISHI WA MUNGU WANAUME NA WANAWAKE (MATENDO 2:17-18).  
 
Nyakati za Kanisa la Kwanza, wanaume na wanawake, wote walikuwa watendakazi, wakilihubiri Neno na kulifundisha (MATENDO 8: 1, 4).  Inatupasa kufuata mfumo huu wa ki-Biblia.  Mara kwa mara, katika Biblia, wanawake, wamekuwa na ujasiri wa kumtumikia Mungu na kuwa wanyenyekevu na watii kwa Yesu Kristo na Neno lake, kuliko wanaume.  Hapa tunaona wanawake waliomfuata Yesu kutoka Galilaya, karibu maili 100 kutoka Yerusalemu, wakija kumtumikia Yesu.  Hapa msalabani, hawakuwako wanafunzi wale kumi na moja wa Yesu kasoro Yohana (YOHANA 19: 25-26).  Wengi walikuwa wanawake waliokuwa wakijipiga vifua na kumwombolezea (LUKA 23:27).  
 
Wanawake walikuwepo msalabani mpaka mwisho na tena walikuwapo kwenye mazishi yake (MST 61) na pia wanawake ndiyo waliokuwa wa kwanza kwenda kulitazama kaburi siku ya kufufuka kwa Yesu (MATHAYO 28:1).  Mwanamke ndiye aliyewapelekea habari za kufufuka kwa Yesu, Petro na Yohana, na kuwatia moyo, NDIPO nao wakachangamka!  Hapo mwanzo, walikuwa wamekata tamaa na kwenda kuvua samaki (YOHANA 20:1-3; 21:1-3).  
 
Mwanamke Priska au Prisila alikuwa tayari kukatwa kichwa kwa ajili ya Injili aliyokuwa anaihubiri Paulo na Mwanamke Fibi aliwasaidia wengi mno (WARUMI 16:1-3).  Shime wanawake, tutende kazi ya Bwana! Wanaume pia tupate changamoto kwa watendakazi wanawake ambao wanatenda kazi ya Mungu kwa bidii pamoja na majukumu mengi ya kifamilia waliyo nayo.
البحث
الأقسام
إقرأ المزيد
2 CHRONICLES
Verse by verse explanation of 2 Chronicles 26
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 30 questions at the...
بواسطة THE HOLY BIBLE 2022-04-02 02:05:08 0 6كيلو بايت
OTHERS
KWANINI MUNGU HUBARIKI MATAIFA YANAYOIBARIKI ISRAELI?
Taifa la Israeli pamoja na mji wake mtakatifu wa Yerusalemu, kimsingi ndio unaoshika funguo za...
بواسطة MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 22:37:50 0 5كيلو بايت
1 CHRONICLES
Book of 1 Chronicles Explained
Book of 1 Chronicles The books of Chronicles were originally one book in the Hebrew text. They...
بواسطة THE HOLY BIBLE 2022-03-20 04:24:31 0 6كيلو بايت
Injili Ya Yesu Kristo
JIHADHARI USIMKATAE MUNGU KATIKA FAHAMU ZAKO
Shalom, leo nipe muda nikuonyeshe jambo muhimu sana katika safari yetu ya wokovu hapa dunia...
بواسطة GOSPEL PREACHER 2021-11-23 13:02:56 0 5كيلو بايت
OTHERS
NIFANYE NINI ILI KUSHINDA TAMAA ZA MWILI?
JE, NINAWEZA KUISHINDA DHAMBI? Sasa je, tunaweza kweli kuishi humu duniani bila dhambi?  ...
بواسطة MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 22:18:48 0 5كيلو بايت