WANAWAKE KUMTUMIKIA MUNGU

0
5KB
Ni uongo wa Shetani kwamba wanawake hawawezi kuwa Watumishi wa Mungu, wakahubiri, wakafundisha, wakatoa pepo au kumtumikia Mungu kwa namna nyinginezo.  Wanawake kumtumikia Mungu, ni jambo la Ki-Biblia hasa. 
 
Nyakati hizi za mwisho, Roho wa Mungu atamwagwa kwa WOTE, binti watatabiri (kuhubiri ni kutabiri pia) na Roho huyu wa Mungu atamwagwa kwa WATUMISHI WA MUNGU WANAUME NA WANAWAKE (MATENDO 2:17-18).  
 
Nyakati za Kanisa la Kwanza, wanaume na wanawake, wote walikuwa watendakazi, wakilihubiri Neno na kulifundisha (MATENDO 8: 1, 4).  Inatupasa kufuata mfumo huu wa ki-Biblia.  Mara kwa mara, katika Biblia, wanawake, wamekuwa na ujasiri wa kumtumikia Mungu na kuwa wanyenyekevu na watii kwa Yesu Kristo na Neno lake, kuliko wanaume.  Hapa tunaona wanawake waliomfuata Yesu kutoka Galilaya, karibu maili 100 kutoka Yerusalemu, wakija kumtumikia Yesu.  Hapa msalabani, hawakuwako wanafunzi wale kumi na moja wa Yesu kasoro Yohana (YOHANA 19: 25-26).  Wengi walikuwa wanawake waliokuwa wakijipiga vifua na kumwombolezea (LUKA 23:27).  
 
Wanawake walikuwepo msalabani mpaka mwisho na tena walikuwapo kwenye mazishi yake (MST 61) na pia wanawake ndiyo waliokuwa wa kwanza kwenda kulitazama kaburi siku ya kufufuka kwa Yesu (MATHAYO 28:1).  Mwanamke ndiye aliyewapelekea habari za kufufuka kwa Yesu, Petro na Yohana, na kuwatia moyo, NDIPO nao wakachangamka!  Hapo mwanzo, walikuwa wamekata tamaa na kwenda kuvua samaki (YOHANA 20:1-3; 21:1-3).  
 
Mwanamke Priska au Prisila alikuwa tayari kukatwa kichwa kwa ajili ya Injili aliyokuwa anaihubiri Paulo na Mwanamke Fibi aliwasaidia wengi mno (WARUMI 16:1-3).  Shime wanawake, tutende kazi ya Bwana! Wanaume pia tupate changamoto kwa watendakazi wanawake ambao wanatenda kazi ya Mungu kwa bidii pamoja na majukumu mengi ya kifamilia waliyo nayo.
Rechercher
Catégories
Lire la suite
Injili Ya Yesu Kristo
IMENIPASA KUWAMO KATIKA NYUMBA YA BABA YANGU
Neno la Uzima kutoka kwa  Askofu Zachary Kakobe        ...
Par GOSPEL PREACHER 2022-01-12 01:49:42 0 6KB
SPIRITUAL EDUCATION
PAULO ALIMAANISHA NINI KATIKA WARAKA KWA WAKOLOSAI 2:16-17
NI NINI HASA PAULO ALIKUWA ANAMAANISHA KATIKA WARAKA WAKE KWA WAKOLOSAI 2:16-17. NAOMBA USOME...
Par Martin Laizer 2023-11-02 11:42:03 0 6KB
Injili Ya Yesu Kristo
ISHARA ZA ZAMANI HIZI
Neno la Uzima kutoka kwa Askofu Zachary Kakobe Tovuti : http://www.bishopzacharykakobe.org...
Par GOSPEL PREACHER 2022-01-12 01:55:23 4 6KB
Injili Ya Yesu Kristo
NINI MAANA YA KUUMBWA KWA MFANO WA MUNGU?
Mungu ni Roho. Je wewe ni nani?Katika somo hili la uumbaji wa binadamu, nitajibu hoja na maswali...
Par MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 08:12:32 0 6KB
DEUTERONOMY
Verse by verse explanation of Deuteronomy 12
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 28 questions at the...
Par THE HOLY BIBLE 2022-01-25 06:04:38 0 5KB