WANAWAKE KUMTUMIKIA MUNGU

0
5KB
Ni uongo wa Shetani kwamba wanawake hawawezi kuwa Watumishi wa Mungu, wakahubiri, wakafundisha, wakatoa pepo au kumtumikia Mungu kwa namna nyinginezo.  Wanawake kumtumikia Mungu, ni jambo la Ki-Biblia hasa. 
 
Nyakati hizi za mwisho, Roho wa Mungu atamwagwa kwa WOTE, binti watatabiri (kuhubiri ni kutabiri pia) na Roho huyu wa Mungu atamwagwa kwa WATUMISHI WA MUNGU WANAUME NA WANAWAKE (MATENDO 2:17-18).  
 
Nyakati za Kanisa la Kwanza, wanaume na wanawake, wote walikuwa watendakazi, wakilihubiri Neno na kulifundisha (MATENDO 8: 1, 4).  Inatupasa kufuata mfumo huu wa ki-Biblia.  Mara kwa mara, katika Biblia, wanawake, wamekuwa na ujasiri wa kumtumikia Mungu na kuwa wanyenyekevu na watii kwa Yesu Kristo na Neno lake, kuliko wanaume.  Hapa tunaona wanawake waliomfuata Yesu kutoka Galilaya, karibu maili 100 kutoka Yerusalemu, wakija kumtumikia Yesu.  Hapa msalabani, hawakuwako wanafunzi wale kumi na moja wa Yesu kasoro Yohana (YOHANA 19: 25-26).  Wengi walikuwa wanawake waliokuwa wakijipiga vifua na kumwombolezea (LUKA 23:27).  
 
Wanawake walikuwepo msalabani mpaka mwisho na tena walikuwapo kwenye mazishi yake (MST 61) na pia wanawake ndiyo waliokuwa wa kwanza kwenda kulitazama kaburi siku ya kufufuka kwa Yesu (MATHAYO 28:1).  Mwanamke ndiye aliyewapelekea habari za kufufuka kwa Yesu, Petro na Yohana, na kuwatia moyo, NDIPO nao wakachangamka!  Hapo mwanzo, walikuwa wamekata tamaa na kwenda kuvua samaki (YOHANA 20:1-3; 21:1-3).  
 
Mwanamke Priska au Prisila alikuwa tayari kukatwa kichwa kwa ajili ya Injili aliyokuwa anaihubiri Paulo na Mwanamke Fibi aliwasaidia wengi mno (WARUMI 16:1-3).  Shime wanawake, tutende kazi ya Bwana! Wanaume pia tupate changamoto kwa watendakazi wanawake ambao wanatenda kazi ya Mungu kwa bidii pamoja na majukumu mengi ya kifamilia waliyo nayo.
Rechercher
Catégories
Lire la suite
JOB
Verse by verse explanation of Job 4
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 29 questions at the...
Par THE HOLY BIBLE 2022-04-02 13:31:42 0 5KB
MASWALI & MAJIBU
Kuna Ufufuo Wa Aina Ngapi?
JIBU: Biblia inasema kuna ufufuo wa aina mbili, Ufufuo wa kwanza, umejumuisha wale...
Par GOSPEL PREACHER 2022-06-13 08:16:59 0 5KB
FORM 3
FORM 3
List of all subjects for the form 3 class AGRICULTURE BASIC MATHEMETICS BIOLOGY BOOK-KEEPING...
Par PROSHABO ONLINE SCHOOLS 2021-10-09 10:24:10 0 5KB
SPIRITUAL EDUCATION
What Does The Holy Spirit Do?
In this study, we’re going to cover four things the Holy Spirit does: 1) The Holy Spirit...
Par MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 06:30:45 0 5KB
REVELATION
UFUNUO 21
Bwana YESU KRISTO atukuzwe, Karibu katika mafunzo ya kitabu cha Ufunuo, leo tukiwa katika ile...
Par GOSPEL PREACHER 2021-10-30 12:58:19 0 7KB