WANAWAKE KUMTUMIKIA MUNGU

0
5KB
Ni uongo wa Shetani kwamba wanawake hawawezi kuwa Watumishi wa Mungu, wakahubiri, wakafundisha, wakatoa pepo au kumtumikia Mungu kwa namna nyinginezo.  Wanawake kumtumikia Mungu, ni jambo la Ki-Biblia hasa. 
 
Nyakati hizi za mwisho, Roho wa Mungu atamwagwa kwa WOTE, binti watatabiri (kuhubiri ni kutabiri pia) na Roho huyu wa Mungu atamwagwa kwa WATUMISHI WA MUNGU WANAUME NA WANAWAKE (MATENDO 2:17-18).  
 
Nyakati za Kanisa la Kwanza, wanaume na wanawake, wote walikuwa watendakazi, wakilihubiri Neno na kulifundisha (MATENDO 8: 1, 4).  Inatupasa kufuata mfumo huu wa ki-Biblia.  Mara kwa mara, katika Biblia, wanawake, wamekuwa na ujasiri wa kumtumikia Mungu na kuwa wanyenyekevu na watii kwa Yesu Kristo na Neno lake, kuliko wanaume.  Hapa tunaona wanawake waliomfuata Yesu kutoka Galilaya, karibu maili 100 kutoka Yerusalemu, wakija kumtumikia Yesu.  Hapa msalabani, hawakuwako wanafunzi wale kumi na moja wa Yesu kasoro Yohana (YOHANA 19: 25-26).  Wengi walikuwa wanawake waliokuwa wakijipiga vifua na kumwombolezea (LUKA 23:27).  
 
Wanawake walikuwepo msalabani mpaka mwisho na tena walikuwapo kwenye mazishi yake (MST 61) na pia wanawake ndiyo waliokuwa wa kwanza kwenda kulitazama kaburi siku ya kufufuka kwa Yesu (MATHAYO 28:1).  Mwanamke ndiye aliyewapelekea habari za kufufuka kwa Yesu, Petro na Yohana, na kuwatia moyo, NDIPO nao wakachangamka!  Hapo mwanzo, walikuwa wamekata tamaa na kwenda kuvua samaki (YOHANA 20:1-3; 21:1-3).  
 
Mwanamke Priska au Prisila alikuwa tayari kukatwa kichwa kwa ajili ya Injili aliyokuwa anaihubiri Paulo na Mwanamke Fibi aliwasaidia wengi mno (WARUMI 16:1-3).  Shime wanawake, tutende kazi ya Bwana! Wanaume pia tupate changamoto kwa watendakazi wanawake ambao wanatenda kazi ya Mungu kwa bidii pamoja na majukumu mengi ya kifamilia waliyo nayo.
Rechercher
Catégories
Lire la suite
PSALMS
Verse by verse explanation of Psalm 16
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 19 questions at the...
Par THE HOLY BIBLE 2022-05-20 11:58:21 0 8KB
RUTH
Book of Ruth Explained
Title: Ancient versions and modern translations consistently entitle this book after Ruth...
Par THE HOLY BIBLE 2022-01-25 11:24:39 0 7KB
LEVITICUS
Verse by verse explanation of Leviticus 18
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 54 questions at the...
Par THE HOLY BIBLE 2022-01-24 10:20:48 0 6KB
OTHERS
JE, YESU ALITUMWA KWA ISRAEL PEKE YAKE?
Waislamu “wanahubiri” kuwa Yesu  hakuja kwa ajili ya ulimwengu wote bali...
Par MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 05:11:00 0 5KB
MAHUSIANO KIBIBLIA
NIFANYE NINI ILI KUSHINDA TAMAA ZA MWILI?
Septemba mwaka 2011, Mwanafunzi mmoja wa shule ya Sekondari alinitembelea nyumbani kwangu hapa...
Par GOSPEL PREACHER 2021-11-23 12:16:15 0 6KB