WANAWAKE KUMTUMIKIA MUNGU

0
5K
Ni uongo wa Shetani kwamba wanawake hawawezi kuwa Watumishi wa Mungu, wakahubiri, wakafundisha, wakatoa pepo au kumtumikia Mungu kwa namna nyinginezo.  Wanawake kumtumikia Mungu, ni jambo la Ki-Biblia hasa. 
 
Nyakati hizi za mwisho, Roho wa Mungu atamwagwa kwa WOTE, binti watatabiri (kuhubiri ni kutabiri pia) na Roho huyu wa Mungu atamwagwa kwa WATUMISHI WA MUNGU WANAUME NA WANAWAKE (MATENDO 2:17-18).  
 
Nyakati za Kanisa la Kwanza, wanaume na wanawake, wote walikuwa watendakazi, wakilihubiri Neno na kulifundisha (MATENDO 8: 1, 4).  Inatupasa kufuata mfumo huu wa ki-Biblia.  Mara kwa mara, katika Biblia, wanawake, wamekuwa na ujasiri wa kumtumikia Mungu na kuwa wanyenyekevu na watii kwa Yesu Kristo na Neno lake, kuliko wanaume.  Hapa tunaona wanawake waliomfuata Yesu kutoka Galilaya, karibu maili 100 kutoka Yerusalemu, wakija kumtumikia Yesu.  Hapa msalabani, hawakuwako wanafunzi wale kumi na moja wa Yesu kasoro Yohana (YOHANA 19: 25-26).  Wengi walikuwa wanawake waliokuwa wakijipiga vifua na kumwombolezea (LUKA 23:27).  
 
Wanawake walikuwepo msalabani mpaka mwisho na tena walikuwapo kwenye mazishi yake (MST 61) na pia wanawake ndiyo waliokuwa wa kwanza kwenda kulitazama kaburi siku ya kufufuka kwa Yesu (MATHAYO 28:1).  Mwanamke ndiye aliyewapelekea habari za kufufuka kwa Yesu, Petro na Yohana, na kuwatia moyo, NDIPO nao wakachangamka!  Hapo mwanzo, walikuwa wamekata tamaa na kwenda kuvua samaki (YOHANA 20:1-3; 21:1-3).  
 
Mwanamke Priska au Prisila alikuwa tayari kukatwa kichwa kwa ajili ya Injili aliyokuwa anaihubiri Paulo na Mwanamke Fibi aliwasaidia wengi mno (WARUMI 16:1-3).  Shime wanawake, tutende kazi ya Bwana! Wanaume pia tupate changamoto kwa watendakazi wanawake ambao wanatenda kazi ya Mungu kwa bidii pamoja na majukumu mengi ya kifamilia waliyo nayo.
Buscar
Categorías
Read More
Injili Ya Yesu Kristo
KUJA KWA YESU KRISTO MARA YA PILI DUNIANI NA VITA YA HAR-MAGEDONI
Neno la Uzima kutoka kwa  Askofu Zachary Kakobe        ...
By GOSPEL PREACHER 2022-01-12 00:33:56 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
MAZINGIRA HATARAISHI YA KUEPUKA KATIKA KUFANYA KAZI NA ROHO MTAKATIFU
Roho Mtakatifu, kwa nafsi na nafasi yake ameletwa ili AKAE nasi...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-23 12:53:48 0 5K
SPIRITUAL EDUCATION
If there is a God, why is there evil?
Agnostics ask: If God is all-powerful and all loving, then why does He permit evil and suffering...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 06:16:47 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
JIHADHARI USIANGUKE TENA ILI USITENGWE NA MUNGU
Na: Patrick & Bernada Sanga Shalom, neema na iwe kwenu na amani zitokazo kwa Mungu Baba yetu...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-23 12:36:12 0 5K
NDOA KIBIBLIA
UNYETI NA UZITO WA NDOA
Shalom mpendwa,Leo ktk kona yetu hii nataka tuangalie unyeti na uzito wa ndoa kutokea ktk...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-06 13:10:52 0 5K