ALIVYOOKOKA SHEIKH ALHAJI RASHID ABUBAKAR WA MSIKITI WA MTAA WA MWANZA ILALA DAR ES SALAAM
نشر بتاريخ 2021-12-24 21:24:13
0
8كيلو بايت
1. AKIRI KULA NYAMA ZA WATU
2. AKIRI KUNYWA DAMU ZA WATU
3. AKIRI KUMEZA MAJINI 360
4. ASEMA UISLAM NI DINI YA WACHAWI
Ndugu msomaji,
Soma huu ushuhuda wa kusisimua kutoka kwa Sheikh Alhaji Rashid Tahtashajara Abubakar aliye kunywa damu za watu, kuhamisha nyota za watu, na kumeza majini 360.
Mwenyekiti wa waislamu waliookoka, Afrika Mashariki na Kati!
Alitokea kwenye familia ya kichawi, mama yake alijiita ni Mungu na kufanya miujiza mbalimbali ikiwemo ya kunyesha mvua. Sheikh Alhaji Rashid Tatashajara Abubakar, aliwahi kufanya shughuli za kisheikh katika msikiti wa Ilala mtaa wa Mwanza ambapo pia alikua mwanafunzi wa sheikh Yahaya Hussein ambaye ni marehemu kwa sasa.
Alianza kujifunza madrasa, akapanda vyeo na kusomea vyuo vya kichawi baada ya kuhitimu majaribio mbalimbali ikiwemo kufukua makaburi, kunywa damu za watu, kuhamisha nyota za watu, na kumeza majini 360 na kufanikiwa kuchaguliwa kuwa mwenyekiti mkuu wa wachawi Afrika mashariki na kati!
Anasema katika mambo hayo yote, alikua akitumwa kushambulia watumishi wa Mungu mbalimbali, aliwahi kujaribu kwa Moses Kulola, Emmanuel Lazaro na Askofu Mwanisongole. Lakini alishindwa na kupata mieleka iliyompelekea kuumwa sana.
“Siku Moja mtaa wa Salender Bridge kama mliwahi kusikia kisa cha dada aliyeota manyoya, alifikishwa kwangu nikamuombea kwa Jina la Yesu naye akapokea uponyaji. Kwa sasa yuko Marekani! nimemuona Mungu kwa jinsi ya tofauti kule nilikotoka nilikua namtumikia shetani, kwa sasa namtumikia Bwana Yesu, na kila ulimi utakiri kwamba Yesu ndiye Mungu”
Alhaji Rashid Abubakary kwa sasa ni mwenyekiti wa waislamu waliookoka Afrika mashariki na kati. Mungu amekua akimtumia kwa jinsi ya tofauti na amealikwa makanisa mbalimbali na kueleza shuhuda nyingi ambazo Bwana Yesu amefanya na kufanya kwenye maisha ya watu wengine. Ameonekana kwenye Televisheni ya kikristo ATN, ushuhuda huu kwa ufupi ameutoa tarehe 26 Agosti 2011, Kanisa la City Christian Centre.
البحث
الأقسام
- BIBLICAL FINANCIAL EDUCATION
- SPIRITUAL EDUCATION
- MASWALI & MAJIBU
- WORLD'S EDUCATION
- MAHUSIANO KIBIBLIA
- Injili Ya Yesu Kristo
- OTHERS
إقرأ المزيد
Verse by verse explanation of Job 5
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 28 questions at the...
Ukijibu Kabla Haujasikia, Ni Upumbavu Na Aibu Kwako.
Maelezo ya Mithali 18:13 Yeye ajibuye kabla hajasikia, Ni upumbavu na aibu kwake.
Hekima...
UFUNUO 11
Karibu katika mwendelezo wa kitabu cha Ufunuo, biblia inasema “Heri asomaye na wao...
NINI MAANA YA KUUMBWA KWA MFANO WA MUNGU?
Mungu ni Roho. Je wewe ni nani?Katika somo hili la uumbaji wa binadamu, nitajibu hoja na maswali...
URAIA WA MBINGUNI.
Bwana Yesu asifiwe…
Kwa ufupi;
Ni vyema tukajifunza kuhusu uraia lakini uraia wa mbinguni...