ALIVYOOKOKA SHEIKH ALHAJI RASHID ABUBAKAR WA MSIKITI WA MTAA WA MWANZA ILALA DAR ES SALAAM
Veröffentlicht 2021-12-24 21:24:13
0
8KB
1. AKIRI KULA NYAMA ZA WATU
2. AKIRI KUNYWA DAMU ZA WATU
3. AKIRI KUMEZA MAJINI 360
4. ASEMA UISLAM NI DINI YA WACHAWI
Ndugu msomaji,
Soma huu ushuhuda wa kusisimua kutoka kwa Sheikh Alhaji Rashid Tahtashajara Abubakar aliye kunywa damu za watu, kuhamisha nyota za watu, na kumeza majini 360.
Mwenyekiti wa waislamu waliookoka, Afrika Mashariki na Kati!
Alitokea kwenye familia ya kichawi, mama yake alijiita ni Mungu na kufanya miujiza mbalimbali ikiwemo ya kunyesha mvua. Sheikh Alhaji Rashid Tatashajara Abubakar, aliwahi kufanya shughuli za kisheikh katika msikiti wa Ilala mtaa wa Mwanza ambapo pia alikua mwanafunzi wa sheikh Yahaya Hussein ambaye ni marehemu kwa sasa.
Alianza kujifunza madrasa, akapanda vyeo na kusomea vyuo vya kichawi baada ya kuhitimu majaribio mbalimbali ikiwemo kufukua makaburi, kunywa damu za watu, kuhamisha nyota za watu, na kumeza majini 360 na kufanikiwa kuchaguliwa kuwa mwenyekiti mkuu wa wachawi Afrika mashariki na kati!
Anasema katika mambo hayo yote, alikua akitumwa kushambulia watumishi wa Mungu mbalimbali, aliwahi kujaribu kwa Moses Kulola, Emmanuel Lazaro na Askofu Mwanisongole. Lakini alishindwa na kupata mieleka iliyompelekea kuumwa sana.
“Siku Moja mtaa wa Salender Bridge kama mliwahi kusikia kisa cha dada aliyeota manyoya, alifikishwa kwangu nikamuombea kwa Jina la Yesu naye akapokea uponyaji. Kwa sasa yuko Marekani! nimemuona Mungu kwa jinsi ya tofauti kule nilikotoka nilikua namtumikia shetani, kwa sasa namtumikia Bwana Yesu, na kila ulimi utakiri kwamba Yesu ndiye Mungu”
Alhaji Rashid Abubakary kwa sasa ni mwenyekiti wa waislamu waliookoka Afrika mashariki na kati. Mungu amekua akimtumia kwa jinsi ya tofauti na amealikwa makanisa mbalimbali na kueleza shuhuda nyingi ambazo Bwana Yesu amefanya na kufanya kwenye maisha ya watu wengine. Ameonekana kwenye Televisheni ya kikristo ATN, ushuhuda huu kwa ufupi ameutoa tarehe 26 Agosti 2011, Kanisa la City Christian Centre.
Suche
Kategorien
- BIBLICAL FINANCIAL EDUCATION
- SPIRITUAL EDUCATION
- MASWALI & MAJIBU
- WORLD'S EDUCATION
- MAHUSIANO KIBIBLIA
- Injili Ya Yesu Kristo
- OTHERS
Mehr lesen
Kati Ya Unyakuo, Dhiki Kuu, Utawala Wa Miaka 1000 Kipi Kinaanza?
SWALI:Naomba kuuliza kati ya Unyakuo wa watakatifu, Dhiki kuu, Vita vya har-magedoni, Utawala wa...
UTHIBITISHO 10 KUWA YESU NI MUNGU
“Wahubiri wa injili” wa Kiislamu huwa wanapinga kuwa Yesu ni Mungu na unapowakatalia...
Verse by verse explanation of Psalm 3
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 38 questions at the...
Verse by verse explanation of Judges 2
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 30 questions at the...
TAFADHALI JIHADHARI USIUKUBALI UONGO HUU WA ADUI.
Bwana Yesu asifiwe mwana wa Mungu, nakusalimu kwa jina la Kristo Yesu, ni matumaini yangu...