ALIVYOOKOKA SHEIKH ALHAJI RASHID ABUBAKAR WA MSIKITI WA MTAA WA MWANZA ILALA DAR ES SALAAM

0
8KB


1. AKIRI KULA NYAMA ZA WATU
2. AKIRI KUNYWA DAMU ZA WATU
3. AKIRI KUMEZA MAJINI 360
4. ASEMA UISLAM NI DINI YA WACHAWI

Ndugu msomaji,

Soma huu ushuhuda wa kusisimua kutoka kwa Sheikh Alhaji Rashid Tahtashajara Abubakar aliye kunywa damu za watu, kuhamisha nyota za watu, na kumeza majini 360. 

Mwenyekiti wa waislamu waliookoka, Afrika Mashariki na Kati!

Alitokea kwenye familia ya kichawi, mama yake alijiita ni Mungu na kufanya miujiza mbalimbali ikiwemo ya kunyesha mvua. Sheikh Alhaji Rashid Tatashajara Abubakar, aliwahi kufanya shughuli za kisheikh katika msikiti wa Ilala mtaa wa Mwanza ambapo pia alikua mwanafunzi wa sheikh Yahaya Hussein ambaye ni marehemu kwa sasa.

Alianza kujifunza madrasa, akapanda vyeo na kusomea vyuo vya kichawi baada ya kuhitimu majaribio mbalimbali ikiwemo kufukua makaburi, kunywa damu za watu, kuhamisha nyota za watu, na kumeza majini 360 na kufanikiwa kuchaguliwa kuwa mwenyekiti mkuu wa wachawi Afrika mashariki na kati!
Anasema katika mambo hayo yote, alikua akitumwa kushambulia watumishi wa Mungu mbalimbali, aliwahi kujaribu kwa Moses Kulola, Emmanuel Lazaro na Askofu Mwanisongole. Lakini alishindwa na kupata mieleka iliyompelekea kuumwa sana.
 
Akielezea ushuhuda wake kwa ufupi, Jinsi alivyompokea Bwana Yesu, ilikuwa sababu ya mke wake wa pili kupita kwenye mkutano wa Injili na kuponywa tumbo lililomsumbua kwa muda mrefu bila mafanikio ya kupona “mke wangu alikuwa akirudi nyumbani na kuimba nyimbo za makafiri, baadaye anaenda kanisani, sasa adhabu ya mtu anayekiuka sheria ni viboko 40, nilipotaka kumchapa mkono ukaganda, ndio mke wangu akasema piga magoti chini, akaniombea na mkono ukarudi mahala pake, baada ya hapo mengi yalitokea kukatisha story Mungu alianza kunifundisha na kunitumia”

“Siku Moja mtaa wa Salender Bridge kama mliwahi kusikia kisa cha dada aliyeota manyoya, alifikishwa kwangu nikamuombea kwa Jina la Yesu naye akapokea uponyaji. Kwa sasa yuko Marekani! nimemuona Mungu kwa jinsi ya tofauti kule nilikotoka nilikua namtumikia shetani, kwa sasa namtumikia Bwana Yesu, na kila ulimi utakiri kwamba Yesu ndiye Mungu”

Alhaji Rashid Abubakary kwa sasa ni mwenyekiti wa waislamu waliookoka Afrika mashariki na kati. Mungu amekua akimtumia kwa jinsi ya tofauti na amealikwa makanisa mbalimbali na kueleza shuhuda nyingi ambazo Bwana Yesu amefanya na kufanya kwenye maisha ya watu wengine. Ameonekana kwenye Televisheni ya kikristo ATN, ushuhuda huu kwa ufupi ameutoa tarehe 26 Agosti 2011, Kanisa la City Christian Centre.
Rechercher
Catégories
Lire la suite
Injili Ya Yesu Kristo
DINI YA KIISLAM ILIANZISHWA SIKU YA JUMATATU MWEZI WA 17, SAWA SAWA NA TAREHE 27 DESEMBA MKWA 610 B.K.
KUMBE UISLAM NI DINI YA KUTENGEZA TU, TENA CHANGA SANA NA HAIKUWEPO KABLA YA MUHAMMAD  ...
Par MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 22:13:31 0 5KB
2 SAMUEL
Verse by verse explanation of 2 Samuel 19
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 40 questions at the...
Par THE HOLY BIBLE 2022-02-05 10:01:28 0 6KB
Religion
USHUHUDA WA MAONO YA JEHANAMU NA YERUSALEMU MPYA WA NYISAKI CHAULA
  UTANGULIZI: Sura ya 1: Kuitwa Sura ya 2: Jehanamu sehemu ya kwanza na Mangojeo ya Wafu....
Par GOSPEL PREACHER 2022-01-12 00:21:26 0 6KB
NDOA KIBIBLIA
MTOFAUTISHE NA WENGINE
KWELI KUU: Mwenzi wako wa ndoa hafanani na yeyote yule, anafanana na wewe, na wala halingani...
Par GOSPEL PREACHER 2021-11-08 00:22:40 0 6KB
MASWALI & MAJIBU
Ubatizo Wa Moto Ni Upi?
JIBU: Ni kweli Yohana alibatiza kwa maji na alisema Bwana YESU atakapokuja atatubatiza kwa...
Par GOSPEL PREACHER 2022-06-13 09:44:22 0 6KB