ALIVYOOKOKA SHEIKH ALHAJI RASHID ABUBAKAR WA MSIKITI WA MTAA WA MWANZA ILALA DAR ES SALAAM

0
8KB


1. AKIRI KULA NYAMA ZA WATU
2. AKIRI KUNYWA DAMU ZA WATU
3. AKIRI KUMEZA MAJINI 360
4. ASEMA UISLAM NI DINI YA WACHAWI

Ndugu msomaji,

Soma huu ushuhuda wa kusisimua kutoka kwa Sheikh Alhaji Rashid Tahtashajara Abubakar aliye kunywa damu za watu, kuhamisha nyota za watu, na kumeza majini 360. 

Mwenyekiti wa waislamu waliookoka, Afrika Mashariki na Kati!

Alitokea kwenye familia ya kichawi, mama yake alijiita ni Mungu na kufanya miujiza mbalimbali ikiwemo ya kunyesha mvua. Sheikh Alhaji Rashid Tatashajara Abubakar, aliwahi kufanya shughuli za kisheikh katika msikiti wa Ilala mtaa wa Mwanza ambapo pia alikua mwanafunzi wa sheikh Yahaya Hussein ambaye ni marehemu kwa sasa.

Alianza kujifunza madrasa, akapanda vyeo na kusomea vyuo vya kichawi baada ya kuhitimu majaribio mbalimbali ikiwemo kufukua makaburi, kunywa damu za watu, kuhamisha nyota za watu, na kumeza majini 360 na kufanikiwa kuchaguliwa kuwa mwenyekiti mkuu wa wachawi Afrika mashariki na kati!
Anasema katika mambo hayo yote, alikua akitumwa kushambulia watumishi wa Mungu mbalimbali, aliwahi kujaribu kwa Moses Kulola, Emmanuel Lazaro na Askofu Mwanisongole. Lakini alishindwa na kupata mieleka iliyompelekea kuumwa sana.
 
Akielezea ushuhuda wake kwa ufupi, Jinsi alivyompokea Bwana Yesu, ilikuwa sababu ya mke wake wa pili kupita kwenye mkutano wa Injili na kuponywa tumbo lililomsumbua kwa muda mrefu bila mafanikio ya kupona “mke wangu alikuwa akirudi nyumbani na kuimba nyimbo za makafiri, baadaye anaenda kanisani, sasa adhabu ya mtu anayekiuka sheria ni viboko 40, nilipotaka kumchapa mkono ukaganda, ndio mke wangu akasema piga magoti chini, akaniombea na mkono ukarudi mahala pake, baada ya hapo mengi yalitokea kukatisha story Mungu alianza kunifundisha na kunitumia”

“Siku Moja mtaa wa Salender Bridge kama mliwahi kusikia kisa cha dada aliyeota manyoya, alifikishwa kwangu nikamuombea kwa Jina la Yesu naye akapokea uponyaji. Kwa sasa yuko Marekani! nimemuona Mungu kwa jinsi ya tofauti kule nilikotoka nilikua namtumikia shetani, kwa sasa namtumikia Bwana Yesu, na kila ulimi utakiri kwamba Yesu ndiye Mungu”

Alhaji Rashid Abubakary kwa sasa ni mwenyekiti wa waislamu waliookoka Afrika mashariki na kati. Mungu amekua akimtumia kwa jinsi ya tofauti na amealikwa makanisa mbalimbali na kueleza shuhuda nyingi ambazo Bwana Yesu amefanya na kufanya kwenye maisha ya watu wengine. Ameonekana kwenye Televisheni ya kikristo ATN, ushuhuda huu kwa ufupi ameutoa tarehe 26 Agosti 2011, Kanisa la City Christian Centre.
Pesquisar
Categorias
Leia mais
Religion
HOW TO BECOME A CHRISTIAN?
This question is very important, and not all human beings know its answer. But it is very simple...
Por GOSPEL PREACHER 2021-08-25 10:01:32 0 5KB
Injili Ya Yesu Kristo
TAJI KWA WATAKATIFU NA HARUSI YA MWANAKONDOO
Neno la Uzima kutoka kwa  Askofu Zachary Kakobe        ...
Por GOSPEL PREACHER 2022-01-12 00:35:38 2 5KB
OTHERS
YEHOVA KWA KIARABU NI YAHUH ( يهوه ) NA SIO ALLAH
Ndugu msomaji, Ninaendelea kuweka ukweli kuhusu Allah ambaye sio Yehova na wala hajawai sema yeye...
Por MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 21:09:27 0 5KB
PSALMS
Verse by verse explanation of Psalm 7
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 25 questions at the...
Por THE HOLY BIBLE 2022-04-04 23:14:19 0 5KB
JOSHUA
Verse by verse explanation of Joshua 19
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 33 questions at the...
Por THE HOLY BIBLE 2022-01-25 08:25:49 0 5KB