Kuna Ufufuo Wa Aina Ngapi?

0
5Кб

JIBU: Biblia inasema kuna ufufuo wa aina mbili,

Ufufuo wa kwanza, umejumuisha wale watakatifu waliofufuka na Bwana Yesu ukisoma (Mathayo 27:52) utaona..,pamoja na watakatifu watakao fufuka katika unyakuo, na watakao fufuliwa wakati wa kuingia kwenye ule utawala wa miaka 1000 (Ufunuo 20:4) haya ni makundi matatu yanayotengeneza aina ya kwanza ya ufufuo.  

Ufunuo 20:6 “….Heri na mtakatifu ni yeye aliye na sehemu katika ufufuo wa kwanza, juu ya hao mauti ya pili haina nguvu…”  

Na ufufuo wa pili utakuja mara tu baada ya utawala wa miaka 1000 kuisha..ambapo wafu wote ambao hawakuwepo katika ufufuo wa kwanza watafufuliwa na kuhukumiwa na Kristo mwenyewe katika hukumu ya kile kiti cheupe cha Enzi cha Yesu Kristo tukisoma  

Ufunuo 20:11 “Kisha nikaona kiti cha enzi, kikubwa, cheupe, na yeye aketiye juu yake; ambaye nchi na mbingu zikakimbia uso wake, na mahali pao hapakuonekana. 12 Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao. 13 Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake. 14 Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto. 15 Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto.”

Kwahiyo ndugu biblia inasema wana heri wale watakaokuwepo katika ule ufufuo wa kwanza. kwasababu mauti ya pili haitakuwa na nguvu juu yao. Na mauti ya pili ni ziwa la moto. Hivyo tujitahidi hata kama Bwana atakupokuja akatukuta tumelala(tumekufa), basi tuwe na nafasi katika ule ufufuo wa kwanza.

Ubarikiwe sana.

Поиск
Категории
Больше
SPIRITUAL EDUCATION
What Is The Purpose Of Life?
Everybody has wondered at one time or another why they exist. What is my purpose in life? Is...
От GOSPEL PREACHER 2023-09-29 09:50:42 0 6Кб
Religion
KUMTUMAINI MUNGU
HEKIMA NI KUMTUMAINI MUNGU TU: Huu ndio ukweli hata Kama wapo watakaopinga, lakini ukweli...
От tabitha Prosper 2021-08-31 06:48:51 0 6Кб
BIBLICAL FINANCIAL EDUCATION
Biblical Personal Finance: Earning for God's Glory
To paraphrase a question often asked by a popular financial advisor, imagine what the people...
От BIBLICAL FINANCES 2021-12-29 15:33:09 0 8Кб
Religion
UFAHAMU KUHUSU DHAMBI YA KUMKUFURU ROHO MTAKATIFU
VIPENGELE VYA SOMO(1). NI MAANA YA KUKUFURU?(2). DHAMBI YA KUMKUFURU ROHO MTAKATIFU IKOJEE?(3)....
От GOSPEL PREACHER 2021-08-24 12:44:21 4 9Кб
REVELATION
UFUNUO 8
Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe.Karibu katika mwendelezo wa kitabu cha Ufunuo, leo kwa...
От GOSPEL PREACHER 2021-10-30 10:32:32 0 6Кб