Kuna Ufufuo Wa Aina Ngapi?

0
5كيلو بايت

JIBU: Biblia inasema kuna ufufuo wa aina mbili,

Ufufuo wa kwanza, umejumuisha wale watakatifu waliofufuka na Bwana Yesu ukisoma (Mathayo 27:52) utaona..,pamoja na watakatifu watakao fufuka katika unyakuo, na watakao fufuliwa wakati wa kuingia kwenye ule utawala wa miaka 1000 (Ufunuo 20:4) haya ni makundi matatu yanayotengeneza aina ya kwanza ya ufufuo.  

Ufunuo 20:6 “….Heri na mtakatifu ni yeye aliye na sehemu katika ufufuo wa kwanza, juu ya hao mauti ya pili haina nguvu…”  

Na ufufuo wa pili utakuja mara tu baada ya utawala wa miaka 1000 kuisha..ambapo wafu wote ambao hawakuwepo katika ufufuo wa kwanza watafufuliwa na kuhukumiwa na Kristo mwenyewe katika hukumu ya kile kiti cheupe cha Enzi cha Yesu Kristo tukisoma  

Ufunuo 20:11 “Kisha nikaona kiti cha enzi, kikubwa, cheupe, na yeye aketiye juu yake; ambaye nchi na mbingu zikakimbia uso wake, na mahali pao hapakuonekana. 12 Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao. 13 Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake. 14 Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto. 15 Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto.”

Kwahiyo ndugu biblia inasema wana heri wale watakaokuwepo katika ule ufufuo wa kwanza. kwasababu mauti ya pili haitakuwa na nguvu juu yao. Na mauti ya pili ni ziwa la moto. Hivyo tujitahidi hata kama Bwana atakupokuja akatukuta tumelala(tumekufa), basi tuwe na nafasi katika ule ufufuo wa kwanza.

Ubarikiwe sana.

البحث
الأقسام
إقرأ المزيد
OTHERS
Je, Biblia inasema nini juu ya Ushoga (ndoa za wanaume kwa wanaume)? Je, Ushoga ni dhambi?
Biblia inasisitiza kila mara kwamba ushoga ni dhambi (mwanzo 19:1-13; mambo ya walawi 18: 22;...
بواسطة MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 04:09:44 0 5كيلو بايت
DEUTERONOMY
Verse by verse explanation of Deuteronomy 23
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 29 questions at the...
بواسطة THE HOLY BIBLE 2022-01-25 06:36:17 0 5كيلو بايت
1 SAMUEL
Verse by verse explanation of 1 Samuel 20
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 52 questions at the...
بواسطة THE HOLY BIBLE 2022-01-26 03:56:56 0 5كيلو بايت
Injili Ya Yesu Kristo
Je, Yesu anawezaje kuwa Mungu na mwanadamu kwa wakati mmoja?
Ni nini maana ya muungano wa kimwili na Uungu?Hili ni swali linalo ulizwa mara nyingi sana, ni...
بواسطة MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 21:14:28 0 5كيلو بايت
Injili Ya Yesu Kristo
ALIVYOOKOKA SHEIKH ALHAJI RASHID ABUBAKAR WA MSIKITI WA MTAA WA MWANZA ILALA DAR ES SALAAM
1. AKIRI KULA NYAMA ZA WATU2. AKIRI KUNYWA DAMU ZA WATU3. AKIRI KUMEZA MAJINI 3604. ASEMA UISLAM...
بواسطة MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 21:24:13 0 8كيلو بايت