Kuna Ufufuo Wa Aina Ngapi?

0
5K

JIBU: Biblia inasema kuna ufufuo wa aina mbili,

Ufufuo wa kwanza, umejumuisha wale watakatifu waliofufuka na Bwana Yesu ukisoma (Mathayo 27:52) utaona..,pamoja na watakatifu watakao fufuka katika unyakuo, na watakao fufuliwa wakati wa kuingia kwenye ule utawala wa miaka 1000 (Ufunuo 20:4) haya ni makundi matatu yanayotengeneza aina ya kwanza ya ufufuo.  

Ufunuo 20:6 “….Heri na mtakatifu ni yeye aliye na sehemu katika ufufuo wa kwanza, juu ya hao mauti ya pili haina nguvu…”  

Na ufufuo wa pili utakuja mara tu baada ya utawala wa miaka 1000 kuisha..ambapo wafu wote ambao hawakuwepo katika ufufuo wa kwanza watafufuliwa na kuhukumiwa na Kristo mwenyewe katika hukumu ya kile kiti cheupe cha Enzi cha Yesu Kristo tukisoma  

Ufunuo 20:11 “Kisha nikaona kiti cha enzi, kikubwa, cheupe, na yeye aketiye juu yake; ambaye nchi na mbingu zikakimbia uso wake, na mahali pao hapakuonekana. 12 Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao. 13 Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake. 14 Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto. 15 Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto.”

Kwahiyo ndugu biblia inasema wana heri wale watakaokuwepo katika ule ufufuo wa kwanza. kwasababu mauti ya pili haitakuwa na nguvu juu yao. Na mauti ya pili ni ziwa la moto. Hivyo tujitahidi hata kama Bwana atakupokuja akatukuta tumelala(tumekufa), basi tuwe na nafasi katika ule ufufuo wa kwanza.

Ubarikiwe sana.

Site içinde arama yapın
Kategoriler
Read More
GENESIS
THE BOOK OF GENESIS EXPLAINED
  BOOK OF GENESIS Genesis is the book of beginnings. It records the beginning of time, life,...
By GOSPEL PREACHER 2021-08-25 14:23:57 0 5K
1 KINGS
Verse by verse explanation of 1 Kings 15
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 39 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-02-05 13:56:33 0 5K
REVELATION
MAJIRA YA KANISA LA SMIRNA
Majira haya ya kanisa la Smirna tutayaona katika {UFUNUO 2:8 -11} ambapo kama...
By GOSPEL PREACHER 2021-09-24 08:49:32 0 6K
2 SAMUEL
Verse by verse explanation of 2 Samuel 6
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 34 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-02-05 09:25:13 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
Jesus Saves
Jesus saves from what and from who? Jesus is the most important figure in all of human...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 05:36:34 0 5K