Kuna Ufufuo Wa Aina Ngapi?

0
5χλμ.

JIBU: Biblia inasema kuna ufufuo wa aina mbili,

Ufufuo wa kwanza, umejumuisha wale watakatifu waliofufuka na Bwana Yesu ukisoma (Mathayo 27:52) utaona..,pamoja na watakatifu watakao fufuka katika unyakuo, na watakao fufuliwa wakati wa kuingia kwenye ule utawala wa miaka 1000 (Ufunuo 20:4) haya ni makundi matatu yanayotengeneza aina ya kwanza ya ufufuo.  

Ufunuo 20:6 “….Heri na mtakatifu ni yeye aliye na sehemu katika ufufuo wa kwanza, juu ya hao mauti ya pili haina nguvu…”  

Na ufufuo wa pili utakuja mara tu baada ya utawala wa miaka 1000 kuisha..ambapo wafu wote ambao hawakuwepo katika ufufuo wa kwanza watafufuliwa na kuhukumiwa na Kristo mwenyewe katika hukumu ya kile kiti cheupe cha Enzi cha Yesu Kristo tukisoma  

Ufunuo 20:11 “Kisha nikaona kiti cha enzi, kikubwa, cheupe, na yeye aketiye juu yake; ambaye nchi na mbingu zikakimbia uso wake, na mahali pao hapakuonekana. 12 Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao. 13 Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake. 14 Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto. 15 Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto.”

Kwahiyo ndugu biblia inasema wana heri wale watakaokuwepo katika ule ufufuo wa kwanza. kwasababu mauti ya pili haitakuwa na nguvu juu yao. Na mauti ya pili ni ziwa la moto. Hivyo tujitahidi hata kama Bwana atakupokuja akatukuta tumelala(tumekufa), basi tuwe na nafasi katika ule ufufuo wa kwanza.

Ubarikiwe sana.

Αναζήτηση
Κατηγορίες
Διαβάζω περισσότερα
Injili Ya Yesu Kristo
Ushuhuda wa Victoria Juu ya Kuzimu
Huu ni ufupisho wa ushuhuda wa Victoria Nehale Nilizaliwa na kuishi Namibia maisha yangu yote;...
από MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 02:40:22 0 5χλμ.
MAHUSIANO KIBIBLIA
NIFANYE NINI ILI KUSHINDA TAMAA ZA MWILI?
Septemba mwaka 2011, Mwanafunzi mmoja wa shule ya Sekondari alinitembelea nyumbani kwangu hapa...
από GOSPEL PREACHER 2021-11-23 12:16:15 0 6χλμ.
JOB
Verse by verse explanation of Job 20
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 20 questions at the...
από THE HOLY BIBLE 2022-04-03 03:50:13 0 5χλμ.
NDOA KIBIBLIA
MWANAMUME HAPASWI KUWA MBINAFSI, MCHOYO
Bwana Yesu asifiwe, Amani iwe nawe.Leo napenda tuanze kuangalia mfululizo wa somo hili la,...
από GOSPEL PREACHER 2021-11-06 13:35:45 0 5χλμ.
DEUTERONOMY
Verse by verse explanation of Joshua 10
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 49 questions at the...
από THE HOLY BIBLE 2022-01-25 07:40:06 0 6χλμ.