Kuna Ufufuo Wa Aina Ngapi?

0
5Кб

JIBU: Biblia inasema kuna ufufuo wa aina mbili,

Ufufuo wa kwanza, umejumuisha wale watakatifu waliofufuka na Bwana Yesu ukisoma (Mathayo 27:52) utaona..,pamoja na watakatifu watakao fufuka katika unyakuo, na watakao fufuliwa wakati wa kuingia kwenye ule utawala wa miaka 1000 (Ufunuo 20:4) haya ni makundi matatu yanayotengeneza aina ya kwanza ya ufufuo.  

Ufunuo 20:6 “….Heri na mtakatifu ni yeye aliye na sehemu katika ufufuo wa kwanza, juu ya hao mauti ya pili haina nguvu…”  

Na ufufuo wa pili utakuja mara tu baada ya utawala wa miaka 1000 kuisha..ambapo wafu wote ambao hawakuwepo katika ufufuo wa kwanza watafufuliwa na kuhukumiwa na Kristo mwenyewe katika hukumu ya kile kiti cheupe cha Enzi cha Yesu Kristo tukisoma  

Ufunuo 20:11 “Kisha nikaona kiti cha enzi, kikubwa, cheupe, na yeye aketiye juu yake; ambaye nchi na mbingu zikakimbia uso wake, na mahali pao hapakuonekana. 12 Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao. 13 Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake. 14 Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto. 15 Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto.”

Kwahiyo ndugu biblia inasema wana heri wale watakaokuwepo katika ule ufufuo wa kwanza. kwasababu mauti ya pili haitakuwa na nguvu juu yao. Na mauti ya pili ni ziwa la moto. Hivyo tujitahidi hata kama Bwana atakupokuja akatukuta tumelala(tumekufa), basi tuwe na nafasi katika ule ufufuo wa kwanza.

Ubarikiwe sana.

Поиск
Категории
Больше
OTHERS
ALLAH ANAAPA KWA ALIYE UMBA KIUME NA KIKE
JE, NANI KAUMBA KIUME NA KIKE?QURAN 92 1-3 Naapa kwa usiku ufunikapo, 2 kwa mchana uingiapo, 3....
От MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 08:39:34 0 5Кб
Injili Ya Yesu Kristo
SOMA KITABU HIKI: ZIJUE SIRI KUBWA ZA SHETANI, ILI UWEZE KUMSHINDA
TOLEO LA 16 ISBN 978 9987 9717-7-0 UTANGULIZI Nawasalimu watu wote wa mataifa yote kwa jina la...
От GOSPEL PREACHER 2021-11-19 05:59:01 0 7Кб
Injili Ya Yesu Kristo
UFALME WA MUNGU
BWANA ASIFIWE, unaweza kupakua (download) somo hili kwa kubonyeza hapa. Au unaweza...
От MOCARECI CHURCH 2021-10-31 00:10:46 0 7Кб
OTHERS
KWANINI MUHAMMAD ALITAKA KUJINYONGA “COMMIT SUICIDE”?
1. MUHAMMAD ALITAKATA KUJINYONGA2. MUHAMMAD ALIPANDA MLIMANI NA KUJARIBU KUJIRUSHA ILI AFE3....
От MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 22:55:32 0 5Кб
Injili Ya Yesu Kristo
NAMNA YA KUITAMBUA SAUTI YA MUNGU INAPOZUNGUMZA NA WEWE
Imekuwa ni ngumu kwa watu wengi kuisikia sauti ya Mungu ikizungumza maishani mwao, hii ni...
От GOSPEL PREACHER 2022-07-10 04:09:01 0 6Кб