Kuna Ufufuo Wa Aina Ngapi?

0
5KB

JIBU: Biblia inasema kuna ufufuo wa aina mbili,

Ufufuo wa kwanza, umejumuisha wale watakatifu waliofufuka na Bwana Yesu ukisoma (Mathayo 27:52) utaona..,pamoja na watakatifu watakao fufuka katika unyakuo, na watakao fufuliwa wakati wa kuingia kwenye ule utawala wa miaka 1000 (Ufunuo 20:4) haya ni makundi matatu yanayotengeneza aina ya kwanza ya ufufuo.  

Ufunuo 20:6 “….Heri na mtakatifu ni yeye aliye na sehemu katika ufufuo wa kwanza, juu ya hao mauti ya pili haina nguvu…”  

Na ufufuo wa pili utakuja mara tu baada ya utawala wa miaka 1000 kuisha..ambapo wafu wote ambao hawakuwepo katika ufufuo wa kwanza watafufuliwa na kuhukumiwa na Kristo mwenyewe katika hukumu ya kile kiti cheupe cha Enzi cha Yesu Kristo tukisoma  

Ufunuo 20:11 “Kisha nikaona kiti cha enzi, kikubwa, cheupe, na yeye aketiye juu yake; ambaye nchi na mbingu zikakimbia uso wake, na mahali pao hapakuonekana. 12 Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao. 13 Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake. 14 Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto. 15 Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto.”

Kwahiyo ndugu biblia inasema wana heri wale watakaokuwepo katika ule ufufuo wa kwanza. kwasababu mauti ya pili haitakuwa na nguvu juu yao. Na mauti ya pili ni ziwa la moto. Hivyo tujitahidi hata kama Bwana atakupokuja akatukuta tumelala(tumekufa), basi tuwe na nafasi katika ule ufufuo wa kwanza.

Ubarikiwe sana.

Suche
Kategorien
Mehr lesen
BIBLICAL FINANCIAL EDUCATION
Should Christians desire wealth?
For the Christian, wealth requires extreme caution. While wealth is not evil or bad in and of...
Von BIBLICAL FINANCES 2021-12-29 15:23:39 0 7KB
REVELATION
UFUNUO 21
Bwana YESU KRISTO atukuzwe, Karibu katika mafunzo ya kitabu cha Ufunuo, leo tukiwa katika ile...
Von GOSPEL PREACHER 2021-10-30 12:58:19 0 7KB
HOLY BIBLE
Will more people go to heaven or to hell?
The question of whether there are more people in heaven or hell is answered by Jesus Himself in...
Von MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 04:21:07 0 5KB
REVELATION
MAJIRA YA KANISA LA THIATIRA
(1) MLENGWA WA KANISA{UFUNUO 2:18}Na kwa malaika wa kanisa lililoko Thiatira andika; Haya ndiyo...
Von GOSPEL PREACHER 2021-09-24 09:47:12 2 7KB
JOB
Verse by verse explanation of Job 19
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 23 questions at the...
Von THE HOLY BIBLE 2022-04-03 03:34:43 0 5KB