Kujichua/punyeto – je, ni dhambi kulingana na Biblia?

0
6كيلو بايت
Biblia haitaji kujichua wala kwamba kujichua ni dhambi. Hakuna swali juu ya kuwa kitendo kinachoelekeza mtu katika kujichua ni dhambi pia. Kujichua ni kitendo cha mwisho katika kuwasilisha ujumbe wa tamaa mbaya, inayotokana na msisimko wa hisia za ngono ama kutazama kanda za video za ngono. Haya ndiyo matatizo ambayo ni tuyatatue. Ikiwa dhambi ya tamaa na kuangalia picha za ngono itaachwa na kushindwa –shida ya kujichua itaisha.
 
Biblia inatuagiza kuepuka hata hali ya kutazama matendo machafu ya ngono (waefeso 5:3). Sioni kuwa kujichua kutashinda mtihani huu. Mara nyingi kitu ambacho unaaibika nacho huwa ni dhambi. Na hata hivyo kwa kuwa hatuwezi kumuomba Mungu akibariki kitendo cha kujichua ili akitumie kwa wema wa jina lake inaonyesha wazi kwamba ni dhambi. Hatuwezi kujisikia tumshukuru Mungu kwa kutuwezesha kufanya kitendo hicho cha kujichua.
 
Biblia inatufundisha, “kwa hivyo mkila au mkinywa chochote mkifanyacho, kifanyeni kwa utukufu wa Mungu” (wakorintho wa kwanza 10:31). Kama hakuna uhakika wa kumpendeza Mungu basi heri kukiacha kitendo hicho. Kitendo cha kujichua ni cha kuonewa shaka. “kwa kuwa chochote ambacho si cha imani ni dhambi” (warumi 14:23). Lazima tujue ya kwamba miili yetu pamoja na roho zetu zimekombolewa na ni za Mungu. “Nini? Hamjui ya kuwa miili yenu ni hekalu la Roho Mtakatifu akaaye ndani yenu kwa ajili ya Mungu na ninyi si mali yenu wenyewe? Kwa kuwa mmenunuliwa kwa thamani; kwa hivyo mtukuzeni Mungu kwa miili yenu na katika roho zenu ambavyo vyote ni vya Mungu” (wakorintho wa kwanza 6:19 -20). Ukweli huu lazima uwe na mizizi ndani ya maisha yetu kokote tuendako na chochote tufanyacho. Kwa sababu ya haya yote ninasema kujichua ni dhambi kwa mujibu wa Biblia. Siamini kujichua kunaweza kumpendeza Mungu, kwa kuwa kunaepuka mipaka ya heshima na sheria ya Mungu juu ya miili yetu.
البحث
الأقسام
إقرأ المزيد
Injili Ya Yesu Kristo
YESU ANASEMA: MSIDHANI NALIKUJA KULETA AMANI DUNIANI, LAAA! BALI UPANGA!
Leo nitajibu haya madai ya Upanga. Waumini wa dini ya Kiislam katika Mihadhara mbalimbali ya...
بواسطة MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 09:16:31 0 6كيلو بايت
SPIRITUAL EDUCATION
KWA MAANA KUJIZOEZA KUPATA NGUVU ZA MWILI KUNAFAA BALI ZA KIROHO ZAIDI SANA
KWA MAANA KUJIZOEZA KUPATA NGUVU ZA MWILI KUNAFAA BALI ZA KIROHO ZAIDI SANA  
بواسطة Martin Laizer 2023-10-10 20:38:59 4 6كيلو بايت
OTHERS
If Jesus was God, why did He say 'No one is good but God alone'?
It is often claimed by those who reject the deity of Christ that inMark 10:17-22Jesus denies His...
بواسطة MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 09:46:29 0 5كيلو بايت
SPIRITUAL EDUCATION
HATARI YA KUHUBIRI WENGINE LAKINI KUWA MKATALIWA – FUNGUO LA YOHANA 4:23
Andiko Kuu: Yohana 4:23 – “Lakini wakati unakuja, na upo sasa, hapo...
بواسطة GOSPEL PREACHER 2026-05-31 05:52:53 0 3كيلو بايت
FORM 4
FORM 4
List of all subjects for the form 4 class AGRICULTURE BASIC MATHEMETICS BIOLOGY BOOK-KEEPING...
بواسطة PROSHABO ONLINE SCHOOLS 2021-10-09 10:25:06 0 6كيلو بايت