Kujichua/punyeto – je, ni dhambi kulingana na Biblia?

0
5K
Biblia haitaji kujichua wala kwamba kujichua ni dhambi. Hakuna swali juu ya kuwa kitendo kinachoelekeza mtu katika kujichua ni dhambi pia. Kujichua ni kitendo cha mwisho katika kuwasilisha ujumbe wa tamaa mbaya, inayotokana na msisimko wa hisia za ngono ama kutazama kanda za video za ngono. Haya ndiyo matatizo ambayo ni tuyatatue. Ikiwa dhambi ya tamaa na kuangalia picha za ngono itaachwa na kushindwa –shida ya kujichua itaisha.
 
Biblia inatuagiza kuepuka hata hali ya kutazama matendo machafu ya ngono (waefeso 5:3). Sioni kuwa kujichua kutashinda mtihani huu. Mara nyingi kitu ambacho unaaibika nacho huwa ni dhambi. Na hata hivyo kwa kuwa hatuwezi kumuomba Mungu akibariki kitendo cha kujichua ili akitumie kwa wema wa jina lake inaonyesha wazi kwamba ni dhambi. Hatuwezi kujisikia tumshukuru Mungu kwa kutuwezesha kufanya kitendo hicho cha kujichua.
 
Biblia inatufundisha, “kwa hivyo mkila au mkinywa chochote mkifanyacho, kifanyeni kwa utukufu wa Mungu” (wakorintho wa kwanza 10:31). Kama hakuna uhakika wa kumpendeza Mungu basi heri kukiacha kitendo hicho. Kitendo cha kujichua ni cha kuonewa shaka. “kwa kuwa chochote ambacho si cha imani ni dhambi” (warumi 14:23). Lazima tujue ya kwamba miili yetu pamoja na roho zetu zimekombolewa na ni za Mungu. “Nini? Hamjui ya kuwa miili yenu ni hekalu la Roho Mtakatifu akaaye ndani yenu kwa ajili ya Mungu na ninyi si mali yenu wenyewe? Kwa kuwa mmenunuliwa kwa thamani; kwa hivyo mtukuzeni Mungu kwa miili yenu na katika roho zenu ambavyo vyote ni vya Mungu” (wakorintho wa kwanza 6:19 -20). Ukweli huu lazima uwe na mizizi ndani ya maisha yetu kokote tuendako na chochote tufanyacho. Kwa sababu ya haya yote ninasema kujichua ni dhambi kwa mujibu wa Biblia. Siamini kujichua kunaweza kumpendeza Mungu, kwa kuwa kunaepuka mipaka ya heshima na sheria ya Mungu juu ya miili yetu.
Site içinde arama yapın
Kategoriler
Read More
SPIRITUAL EDUCATION
Spirit, Soul, and Body
The Christian doctrine of immortality cannot be understood apart from the right conception of...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 05:38:37 0 5K
JONAH
YONA 4
Bwana wetu YESU KRISTO atukuzwe. Tunamshukuru Mungu kwa kutupa neema hii mpya ya kujifunza...
By GOSPEL PREACHER 2022-01-20 03:14:39 0 5K
1 KINGS
Verse by verse explanation of 1 Kings 19
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 32 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-02-05 15:55:21 0 6K
Other
IGVault Fast Way to Make Money in Burning Crusade Classic 2022
As you are making your way through World of Warcraft: The Burning Crusade, you are going to...
By Wowgold Igvault 2022-05-12 02:02:10 0 9K
OTHERS
UTATA: NUHU WA QURAN NI TOFAUTI NA NUHU WA BIBLIA
Ndugu Msomaji: Siku zote Waislam huwa mnatutambia kuwa, Quran ni kitabu kilichoeleza kila...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 03:30:49 0 5K