Kujichua/punyeto – je, ni dhambi kulingana na Biblia?

0
6K
Biblia haitaji kujichua wala kwamba kujichua ni dhambi. Hakuna swali juu ya kuwa kitendo kinachoelekeza mtu katika kujichua ni dhambi pia. Kujichua ni kitendo cha mwisho katika kuwasilisha ujumbe wa tamaa mbaya, inayotokana na msisimko wa hisia za ngono ama kutazama kanda za video za ngono. Haya ndiyo matatizo ambayo ni tuyatatue. Ikiwa dhambi ya tamaa na kuangalia picha za ngono itaachwa na kushindwa –shida ya kujichua itaisha.
 
Biblia inatuagiza kuepuka hata hali ya kutazama matendo machafu ya ngono (waefeso 5:3). Sioni kuwa kujichua kutashinda mtihani huu. Mara nyingi kitu ambacho unaaibika nacho huwa ni dhambi. Na hata hivyo kwa kuwa hatuwezi kumuomba Mungu akibariki kitendo cha kujichua ili akitumie kwa wema wa jina lake inaonyesha wazi kwamba ni dhambi. Hatuwezi kujisikia tumshukuru Mungu kwa kutuwezesha kufanya kitendo hicho cha kujichua.
 
Biblia inatufundisha, “kwa hivyo mkila au mkinywa chochote mkifanyacho, kifanyeni kwa utukufu wa Mungu” (wakorintho wa kwanza 10:31). Kama hakuna uhakika wa kumpendeza Mungu basi heri kukiacha kitendo hicho. Kitendo cha kujichua ni cha kuonewa shaka. “kwa kuwa chochote ambacho si cha imani ni dhambi” (warumi 14:23). Lazima tujue ya kwamba miili yetu pamoja na roho zetu zimekombolewa na ni za Mungu. “Nini? Hamjui ya kuwa miili yenu ni hekalu la Roho Mtakatifu akaaye ndani yenu kwa ajili ya Mungu na ninyi si mali yenu wenyewe? Kwa kuwa mmenunuliwa kwa thamani; kwa hivyo mtukuzeni Mungu kwa miili yenu na katika roho zenu ambavyo vyote ni vya Mungu” (wakorintho wa kwanza 6:19 -20). Ukweli huu lazima uwe na mizizi ndani ya maisha yetu kokote tuendako na chochote tufanyacho. Kwa sababu ya haya yote ninasema kujichua ni dhambi kwa mujibu wa Biblia. Siamini kujichua kunaweza kumpendeza Mungu, kwa kuwa kunaepuka mipaka ya heshima na sheria ya Mungu juu ya miili yetu.
Căutare
Categorii
Citeste mai mult
FORM 1
GEOGRAPHY : FORM 1
List of all topics in Geography for the form 1 class: CLICK HERE TO DOWNLOAD. CONCEPT OF...
By PROSHABO ONLINE SCHOOLS 2021-10-31 17:05:31 0 7K
TANZANIA
WELCOME TO PROSHABO ONLINE SCHOOLS
Our online system can be accessed by CLICKING HERE, if you have any problem in clicking this...
By PROSHABO ONLINE SCHOOLS 2021-10-30 07:08:06 0 8K
2 CHRONICLES
Verse by verse explanation of 2 Chronicles 26
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 30 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-04-02 02:05:08 0 6K
Injili Ya Yesu Kristo
EPUKA UONGO UKIENDELEA KUTENDA DHAMBI BAADA YA KUOKOKA, HUENDI MBINGUNI KAMWE / IF YOU CONTINUE TO SIN AFTER BEING SAVED, YOU WILL NOT GO TO HEAVEN
SWAHILI: Bwana Yesu (ambaye ni Mungu mkuu na mwokozi wetu, Tito 2:13)  asifiweeee! Lengo la...
By PROSPER HABONA 2022-01-16 14:16:25 0 6K
Injili Ya Yesu Kristo
HISTORIA FUPI YA IBADA YA KISHETANI YA ROZARI.
UTANGULIZI Katika Biblia hakuna mahali popote pale panapofundisha kuwa tusali rozali, na hata...
By GOSPEL PREACHER 2021-12-22 01:04:26 0 7K