Kujichua/punyeto – je, ni dhambi kulingana na Biblia?

0
5KB
Biblia haitaji kujichua wala kwamba kujichua ni dhambi. Hakuna swali juu ya kuwa kitendo kinachoelekeza mtu katika kujichua ni dhambi pia. Kujichua ni kitendo cha mwisho katika kuwasilisha ujumbe wa tamaa mbaya, inayotokana na msisimko wa hisia za ngono ama kutazama kanda za video za ngono. Haya ndiyo matatizo ambayo ni tuyatatue. Ikiwa dhambi ya tamaa na kuangalia picha za ngono itaachwa na kushindwa –shida ya kujichua itaisha.
 
Biblia inatuagiza kuepuka hata hali ya kutazama matendo machafu ya ngono (waefeso 5:3). Sioni kuwa kujichua kutashinda mtihani huu. Mara nyingi kitu ambacho unaaibika nacho huwa ni dhambi. Na hata hivyo kwa kuwa hatuwezi kumuomba Mungu akibariki kitendo cha kujichua ili akitumie kwa wema wa jina lake inaonyesha wazi kwamba ni dhambi. Hatuwezi kujisikia tumshukuru Mungu kwa kutuwezesha kufanya kitendo hicho cha kujichua.
 
Biblia inatufundisha, “kwa hivyo mkila au mkinywa chochote mkifanyacho, kifanyeni kwa utukufu wa Mungu” (wakorintho wa kwanza 10:31). Kama hakuna uhakika wa kumpendeza Mungu basi heri kukiacha kitendo hicho. Kitendo cha kujichua ni cha kuonewa shaka. “kwa kuwa chochote ambacho si cha imani ni dhambi” (warumi 14:23). Lazima tujue ya kwamba miili yetu pamoja na roho zetu zimekombolewa na ni za Mungu. “Nini? Hamjui ya kuwa miili yenu ni hekalu la Roho Mtakatifu akaaye ndani yenu kwa ajili ya Mungu na ninyi si mali yenu wenyewe? Kwa kuwa mmenunuliwa kwa thamani; kwa hivyo mtukuzeni Mungu kwa miili yenu na katika roho zenu ambavyo vyote ni vya Mungu” (wakorintho wa kwanza 6:19 -20). Ukweli huu lazima uwe na mizizi ndani ya maisha yetu kokote tuendako na chochote tufanyacho. Kwa sababu ya haya yote ninasema kujichua ni dhambi kwa mujibu wa Biblia. Siamini kujichua kunaweza kumpendeza Mungu, kwa kuwa kunaepuka mipaka ya heshima na sheria ya Mungu juu ya miili yetu.
Rechercher
Catégories
Lire la suite
DEUTERONOMY
Verse by verse explanation of Deuteronomy 1
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 62 questions at the...
Par THE HOLY BIBLE 2022-01-24 19:17:34 0 5KB
SPIRITUAL EDUCATION
WANYAMA SABA 7 KATIKA KITABU CHA DANIEL
1.Tafsiri ya unabii wa hicho kitabu cha Daniel 2.Kuhusu kanisa la Leo.Hivyo sisi kanisa la Leo...
Par Martin Laizer 2023-09-22 07:26:51 4 32KB
Injili Ya Yesu Kristo
JE! MUNGU ANAZUNGUMZA NA SISI TULIO HAI KUPITIA WAFU?
Ndugu zangu Bwana Yesu asifiwe.Katika kujifunza neno la Mungu nilikutana na maandiko kwenye...
Par GOSPEL PREACHER 2022-04-06 00:48:09 1 6KB
Injili Ya Yesu Kristo
JIFUNZE KUENENDA KWA ROHO ILI USIMHUZUNISHE ROHO MTAKATIFU
Shalom, hakuna namna mwamini anaweza kuishi maisha ya kumpendeza Mungu hapa duniani bila kuenenda...
Par GOSPEL PREACHER 2021-11-23 12:54:38 0 6KB
OTHERS
Je, Biblia inasema nini juu ya Ushoga (ndoa za wanaume kwa wanaume)? Je, Ushoga ni dhambi?
Biblia inasisitiza kila mara kwamba ushoga ni dhambi (mwanzo 19:1-13; mambo ya walawi 18: 22;...
Par MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 04:09:44 0 5KB