Kujichua/punyeto – je, ni dhambi kulingana na Biblia?

0
5KB
Biblia haitaji kujichua wala kwamba kujichua ni dhambi. Hakuna swali juu ya kuwa kitendo kinachoelekeza mtu katika kujichua ni dhambi pia. Kujichua ni kitendo cha mwisho katika kuwasilisha ujumbe wa tamaa mbaya, inayotokana na msisimko wa hisia za ngono ama kutazama kanda za video za ngono. Haya ndiyo matatizo ambayo ni tuyatatue. Ikiwa dhambi ya tamaa na kuangalia picha za ngono itaachwa na kushindwa –shida ya kujichua itaisha.
 
Biblia inatuagiza kuepuka hata hali ya kutazama matendo machafu ya ngono (waefeso 5:3). Sioni kuwa kujichua kutashinda mtihani huu. Mara nyingi kitu ambacho unaaibika nacho huwa ni dhambi. Na hata hivyo kwa kuwa hatuwezi kumuomba Mungu akibariki kitendo cha kujichua ili akitumie kwa wema wa jina lake inaonyesha wazi kwamba ni dhambi. Hatuwezi kujisikia tumshukuru Mungu kwa kutuwezesha kufanya kitendo hicho cha kujichua.
 
Biblia inatufundisha, “kwa hivyo mkila au mkinywa chochote mkifanyacho, kifanyeni kwa utukufu wa Mungu” (wakorintho wa kwanza 10:31). Kama hakuna uhakika wa kumpendeza Mungu basi heri kukiacha kitendo hicho. Kitendo cha kujichua ni cha kuonewa shaka. “kwa kuwa chochote ambacho si cha imani ni dhambi” (warumi 14:23). Lazima tujue ya kwamba miili yetu pamoja na roho zetu zimekombolewa na ni za Mungu. “Nini? Hamjui ya kuwa miili yenu ni hekalu la Roho Mtakatifu akaaye ndani yenu kwa ajili ya Mungu na ninyi si mali yenu wenyewe? Kwa kuwa mmenunuliwa kwa thamani; kwa hivyo mtukuzeni Mungu kwa miili yenu na katika roho zenu ambavyo vyote ni vya Mungu” (wakorintho wa kwanza 6:19 -20). Ukweli huu lazima uwe na mizizi ndani ya maisha yetu kokote tuendako na chochote tufanyacho. Kwa sababu ya haya yote ninasema kujichua ni dhambi kwa mujibu wa Biblia. Siamini kujichua kunaweza kumpendeza Mungu, kwa kuwa kunaepuka mipaka ya heshima na sheria ya Mungu juu ya miili yetu.
Suche
Kategorien
Mehr lesen
Injili Ya Yesu Kristo
JIPANGE KABLA YA NDOA!
Bwana Yesu asifiwe… Kwa ufupi; Moja ya tatizo kubwa linalowasumbua  vijana ni...
Von GOSPEL PREACHER 2022-03-30 05:16:16 0 5KB
SPIRITUAL EDUCATION
IT IS NOT FOR THE ANOINTED
This message was given to me on the evening of  March 29, 2014 in Njombe Region after...
Von GOSPEL PREACHER 2021-11-23 07:40:43 0 5KB
NDOA KIBIBLIA
MWANAUME: SIO MKE WAKO NI WEWE
Mchungaji wangu Emmanuel Nhyama Manwele ambaye ni mwalimu wangu wa kwanza wa ndoa na maswala...
Von GOSPEL PREACHER 2021-11-08 00:15:02 0 6KB
CERTIFICATE
CERTIFICATE
List of all subjects for the students who are taking certificate courses.
Von PROSHABO ONLINE SCHOOLS 2021-10-09 10:45:31 0 5KB
OTHERS
WAZAZI WA MUHAMMAD WALIKUWA MAKAFIRI NA WALIKUFA MAKAFIRI
Ndugu msomaji, KUMBE MAMA YAKE NABII MUHAMMAD ALIKUFA KAFIRI Bi Amina mamake na Muhammad kafa...
Von MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 21:28:03 0 5KB