Kujichua/punyeto – je, ni dhambi kulingana na Biblia?

0
5K
Biblia haitaji kujichua wala kwamba kujichua ni dhambi. Hakuna swali juu ya kuwa kitendo kinachoelekeza mtu katika kujichua ni dhambi pia. Kujichua ni kitendo cha mwisho katika kuwasilisha ujumbe wa tamaa mbaya, inayotokana na msisimko wa hisia za ngono ama kutazama kanda za video za ngono. Haya ndiyo matatizo ambayo ni tuyatatue. Ikiwa dhambi ya tamaa na kuangalia picha za ngono itaachwa na kushindwa –shida ya kujichua itaisha.
 
Biblia inatuagiza kuepuka hata hali ya kutazama matendo machafu ya ngono (waefeso 5:3). Sioni kuwa kujichua kutashinda mtihani huu. Mara nyingi kitu ambacho unaaibika nacho huwa ni dhambi. Na hata hivyo kwa kuwa hatuwezi kumuomba Mungu akibariki kitendo cha kujichua ili akitumie kwa wema wa jina lake inaonyesha wazi kwamba ni dhambi. Hatuwezi kujisikia tumshukuru Mungu kwa kutuwezesha kufanya kitendo hicho cha kujichua.
 
Biblia inatufundisha, “kwa hivyo mkila au mkinywa chochote mkifanyacho, kifanyeni kwa utukufu wa Mungu” (wakorintho wa kwanza 10:31). Kama hakuna uhakika wa kumpendeza Mungu basi heri kukiacha kitendo hicho. Kitendo cha kujichua ni cha kuonewa shaka. “kwa kuwa chochote ambacho si cha imani ni dhambi” (warumi 14:23). Lazima tujue ya kwamba miili yetu pamoja na roho zetu zimekombolewa na ni za Mungu. “Nini? Hamjui ya kuwa miili yenu ni hekalu la Roho Mtakatifu akaaye ndani yenu kwa ajili ya Mungu na ninyi si mali yenu wenyewe? Kwa kuwa mmenunuliwa kwa thamani; kwa hivyo mtukuzeni Mungu kwa miili yenu na katika roho zenu ambavyo vyote ni vya Mungu” (wakorintho wa kwanza 6:19 -20). Ukweli huu lazima uwe na mizizi ndani ya maisha yetu kokote tuendako na chochote tufanyacho. Kwa sababu ya haya yote ninasema kujichua ni dhambi kwa mujibu wa Biblia. Siamini kujichua kunaweza kumpendeza Mungu, kwa kuwa kunaepuka mipaka ya heshima na sheria ya Mungu juu ya miili yetu.
Pesquisar
Categorias
Leia Mais
Injili Ya Yesu Kristo
Jinsi ya kuzidi kuwa Hodari.
Utangulizi: Tunasoma Katika maandiko ya kwamba watu wengi wanaotajwa kama mashujaa wa Imani...
Por GOSPEL PREACHER 2022-03-31 14:49:05 0 7K
Injili Ya Yesu Kristo
HABARI ZA MWANA MPOTEVU
(A) MWANA MPOTEVU (MTOTO MDOGO)  LUKA 15;11-24 "Kulikuwa na mtu mmoja mwenye wana...
Por GOSPEL PREACHER 2022-01-15 22:14:25 0 6K
HOLY BIBLE
Responding to the Jehovah’s Witness attacks on the deity of Christ
If Jesus is God, why did he pray to the Father in John 17? Jesus prayed to the Father because as...
Por MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 06:00:07 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
NJIA YA WOKOVU NDANI YA KITABU CHA WARUMI.*
NJIA YA WOKOVU NDANI YA KITABU CHA WARUMI.*  
Por Martin Laizer 2023-10-18 04:00:33 0 6K
Injili Ya Yesu Kristo
HAKIKA ALIKUWA MWANA WA MUNGU
Neno la Uzima kutoka kwa  Askofu Zachary...
Por GOSPEL PREACHER 2022-01-12 01:29:16 0 5K