YESU ANASEMA: MSIDHANI NALIKUJA KULETA AMANI DUNIANI, LAAA! BALI UPANGA!

0
6χλμ.

Leo nitajibu haya madai ya Upanga.

Waumini wa dini ya Kiislam katika Mihadhara mbalimbali ya kidini wamekuwa na tabia ya kutumia aya YA UPANGA iliyopo katika Mathayo 10: 34 inayo sema ''MSIDHANI NALIKUJA KULETA AMANI DUNIANI, LAAA! BALI UPANGA! Waislam wanadai kuwa, katika aya hii, Yesu alikuja kuleta UPANGA na si Habari Njema kama tufundishavyo sisi Wakristo.

Kwa kuwa Waislam kazi yao ni kutoa kashfa na kuutukana Ukristo, wahadhiri hao wa Dini ya Uislamu hufundisha jamii kwa kutumia Qurani na Biblia na kusema kuwa eti Yesu alikuja kuleta UPANGA  na Hivyo Basi Ukristo ni dini ya UPANGA. Fundisho hili la "MSIDHANI NALIKUJA KULETA AMANI DUNIANI, LAAA! BALI UPANGA! " wanalieneza kwa kupitia Mitandao mbalimbali kama ya  Radio, Vijarida, Mihadhara, vitabu na Kanda (cassettes) za Video na Audio. Na hivyo kuwafanya baadhi ya Wakristo kuingiwa na wasiwasi kutokana na jinsi hawa Wahadhiri wa Dini ya Uislamu wanavyo toa kashfa chafu kwa Yesu Kristo ambaye ni Masiah. Na baadhi ya Wakristo wengine ingawa hawajabadili dini wanaamini hivyo. Swali la muhimu la kujiuliza kwa kila Mkristo, je, ni kweli Yesu alikuja kuleta UPANGA? Nakusihi fuatilia somo hili kwa makini ili kujua Ukweli wa aya hii:

 

Ngoja niiweke hiyo aya:

Mathayo 10:34''MSIDHANI NALIKUJA KULETA AMANI DUNIANI, LAAA! BALI UPANGA!

Ukitazama na kusikiliza kwa haraka haraka namna wahadhiri hao wa Dini ya Uislamu wanavyoifunda hii aya ya Biblia unaweza ukashawishika kuamini hicho wanachokifundisha, lakini ni vyema tukajifundisha kwa undani kadiri maneno ya Yesu kuwa "MSIDHANI NALIKUJA KULETA AMANI DUNIANI, LAAA! BALI UPANGA!" kisha tuone kama kuna ukweli juu ya hayo mafundisho yao, ya kusema kuwa Yesu alikuja kuleta Upanga na si kutangaza Habari Njema kwa Mataifa yote. 

Haya tuanze utafiti wetu.

Kwanza tujiuluize, Je, Yesu analeta Upanga wa ainga gani? Yesu anazungumzi Upanga ambao ni “Neno la Mungu”.  Neno la Mungu linagawanya na au kukata Mabaya na kuacha mazuri.  Hebu kwanza tuyasome maagizo yake kwa wanafuzi. Mathayo 10 aya 16: Inasema: Sasa, mimi nawatuma ninyi kama kondoo kati ya mbwa mwitu. Muwe na busara kama nyoka, na wapole kama njiwa. Katika hii AYA, Yesu anawaambia Wanafunzi wake wawe na Busara na Wapole, Hatusomi katia hii aya kuwa anawaambia wabebe Upanga. Je, Yesu alipo sema Upanga, alimaanisha nini? Hebu tuendelee na somo letu.

Sasa tuangalie aya ya 1 inasema:  “Yesu aliwaita wanafunzi wake kumi na wawili, akawapa uwezo wa kutoa pepo wachafu na kuponya magonjwa na maradhi yote”. Upanga unao zungumziwa hapa ni uwezo ambao Yesu aliwapa Wanafunzi wake. Unaweza kuniuliza uwezo huo ni nini?

Hebu tusome Kitabu cha Waefeso ili tuweze kuelewa nini hasa maana ya Upanga na Uwezo wa kutoa Pepo na Kuponya kama alivyo wapa Wanafunzi wake.


Waefeso 6:17

17 Vaeni wokovu kama kofia ya vita vichwani na chukueni UPANGA wa Roho ambao ni neno la Mungu.

Kutokana na ayah hii ya Waefeso, tumeweza kufunguliwa macho yetu ya Kiroho na kuelewa kuwa UPANGA NI NENO LA MUNGU.

Kwasabau Waislam wanakubali kuwa Yesu kaleta Upanga ambao sasa tunaelewa nini maana yake kutoka na Ushaidi wa Waefeso. Basi leo hii hawa Waislam hawatakuwa na jinsi ya kujitetea bali kukubali kuwa Upanga ambao ni Neno la Mungu ni wa kufuatwa kama alivyo sema Yesu katika Mathayo 10: 34.

Ni matumaini yangu kuwa leo hii umeweza kujua kwa undani maana ya "MSIDHANI NALIKUJA KULETA AMANI DUNIANI, LAAA! BALI (UPANGA) NENO LA MUNGU!" na Yesu alipo sema hayo alikuwa anatufahamisha kuwa neon La Mungu ni Sawa na Upanga Mkali unao tenganisha na au toa Mabaya yote kwa Binadamu.

Mungu awabariki sana

Αναζήτηση
Κατηγορίες
Διαβάζω περισσότερα
Injili Ya Yesu Kristo
NIMEKUTANA NA YESU KRISTO.
Mwaka 2012 mwezi Novemba, Nilikuwa mgonjwa sana na wazazi wangu wakanichukua na kunipeleka...
από GOSPEL PREACHER 2022-07-10 05:31:42 0 7χλμ.
HOLY BIBLE
Will more people go to heaven or to hell?
The question of whether there are more people in heaven or hell is answered by Jesus Himself in...
από MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 04:21:07 0 5χλμ.
SPIRITUAL EDUCATION
What will happen to those who die without hearing anything of Christ Jesus?
The Holy Bible makes it conspicuous and crystal clear that while there are might be people in the...
από MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 06:15:50 0 6χλμ.
SPIRITUAL EDUCATION
AINA ZA MAGONJWA
AINA ZA MAGONJWA NA DAWA YAKE
από Martin Laizer 2023-09-26 06:41:50 8 18χλμ.
NUMBERS
Verse by verse explanation of Numbers 25
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 26 questions at the...
από THE HOLY BIBLE 2022-01-24 15:12:57 0 6χλμ.