Je, Biblia inasema nini juu ya Ushoga (ndoa za wanaume kwa wanaume)? Je, Ushoga ni dhambi?

0
5χλμ.
Biblia inasisitiza kila mara kwamba ushoga ni dhambi (mwanzo 19:1-13; mambo ya walawi 18: 22; warumi 1:26-27; wakorintho wa kwanza 6:9). Warumi 1:26-27 inatufundisha ya kwamba ushoga ni njia mojawapo ya kumkana na kutomtii Mungu. Mtu anapodumu katika dhambi na kutokuamini biblia inatuambia ya kwamba “Mungu huwaachilia” kutenda maovu zaidi ili wapate kujua ubatili wa maisha bila Uwepo wa Mungu. Wakorintho wa kwanza 6:9 inasema kuwa mashoga hawataurithi ufalme wa Mungu.
 
Mungu haumbi mwanadamu mwenye tamaa ya ushoga. Biblia inatuambia mtu huwa shoga kwa sababu ya dhambi. (warumi 1:24-27), na pia kwa sababu ya uamuzi wake mwenyewe. Mtu anaweza kuzaliwa na msukumo juu ya ushoga kama vile watu pia huzaliwa na msukumo juu ya fujo na dhambi nyinginezo. Hili halihalalishi dhambi yoyote inayofanywa na wanadamu. Je, mtu akizaliwa na msukumo wa hasira mbaya, ni halali aendeleze hasira zake mbaya? La, hasha. Hata kwa ushoga pia si halali.
 
Hata hivyo Biblia haiitaji dhambi ya ushoga kuwa ndiyo kubwa zaidi. Kila dhambi ni chukizo kwa Mungu. Ushoga ni mojawapo ya mambo yaliyoorodheshwa katika wakorintho wa kwanza 6:9-10 yatakayozuia mtu asiingie katika ufalme wa Mungu. Kulingana na Biblia msamaha wa Mungu juu ya shoga upo sawa na wa mzinzi, muabudu sanamu, muuaji, mwizi na kadhalika. Mungu tena aahidi uwezo juu ya kushinda dhambi, pamoja na ushoga, kwa wale wote watakao mwaminiYesu kristo kwa wokovu wao (wakorintho wa kwanza 6:11; wakorintho wa pili 5:17).
Αναζήτηση
Κατηγορίες
Διαβάζω περισσότερα
SPIRITUAL EDUCATION
MZABIBU WA KWELI
                 YOHANE 15:5-10 ...
από Martin Laizer 2025-03-11 02:07:19 0 2χλμ.
Injili Ya Yesu Kristo
SIRI ZA KIROHO ZILIZOPO NDANI YA SIKUU 7 ZA KIYAHUDI
Baada ya wana wa Israeli kutoka Misri na kuingia katika nchi yao ya ahadi Mungu aliwaagiza...
από GOSPEL PREACHER 2023-07-16 00:04:43 2 8χλμ.
2 SAMUEL
Verse by verse explanation of 2 Samuel 13
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 32 questions at the...
από THE HOLY BIBLE 2022-02-05 09:44:30 0 6χλμ.
1 SAMUEL
Verse by verse explanation of 1 Samuel 7
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 27 questions at the...
από THE HOLY BIBLE 2022-01-26 03:28:24 0 5χλμ.
OTHERS
NIFANYE NINI ILI KUSHINDA TAMAA ZA MWILI?
JE, NINAWEZA KUISHINDA DHAMBI? Sasa je, tunaweza kweli kuishi humu duniani bila dhambi?  ...
από MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 22:18:48 0 6χλμ.