Je, Biblia inasema nini juu ya Ushoga (ndoa za wanaume kwa wanaume)? Je, Ushoga ni dhambi?

0
5χλμ.
Biblia inasisitiza kila mara kwamba ushoga ni dhambi (mwanzo 19:1-13; mambo ya walawi 18: 22; warumi 1:26-27; wakorintho wa kwanza 6:9). Warumi 1:26-27 inatufundisha ya kwamba ushoga ni njia mojawapo ya kumkana na kutomtii Mungu. Mtu anapodumu katika dhambi na kutokuamini biblia inatuambia ya kwamba “Mungu huwaachilia” kutenda maovu zaidi ili wapate kujua ubatili wa maisha bila Uwepo wa Mungu. Wakorintho wa kwanza 6:9 inasema kuwa mashoga hawataurithi ufalme wa Mungu.
 
Mungu haumbi mwanadamu mwenye tamaa ya ushoga. Biblia inatuambia mtu huwa shoga kwa sababu ya dhambi. (warumi 1:24-27), na pia kwa sababu ya uamuzi wake mwenyewe. Mtu anaweza kuzaliwa na msukumo juu ya ushoga kama vile watu pia huzaliwa na msukumo juu ya fujo na dhambi nyinginezo. Hili halihalalishi dhambi yoyote inayofanywa na wanadamu. Je, mtu akizaliwa na msukumo wa hasira mbaya, ni halali aendeleze hasira zake mbaya? La, hasha. Hata kwa ushoga pia si halali.
 
Hata hivyo Biblia haiitaji dhambi ya ushoga kuwa ndiyo kubwa zaidi. Kila dhambi ni chukizo kwa Mungu. Ushoga ni mojawapo ya mambo yaliyoorodheshwa katika wakorintho wa kwanza 6:9-10 yatakayozuia mtu asiingie katika ufalme wa Mungu. Kulingana na Biblia msamaha wa Mungu juu ya shoga upo sawa na wa mzinzi, muabudu sanamu, muuaji, mwizi na kadhalika. Mungu tena aahidi uwezo juu ya kushinda dhambi, pamoja na ushoga, kwa wale wote watakao mwaminiYesu kristo kwa wokovu wao (wakorintho wa kwanza 6:11; wakorintho wa pili 5:17).
Αναζήτηση
Κατηγορίες
Διαβάζω περισσότερα
MASWALI & MAJIBU
Nini Maana Ya Kusali Kwa Kupayuka Payuka?
Swali linaendelea…..Na Je, nisali kwa namna gani ili maombi yangu yasionekane kuwa ni ya...
από GOSPEL PREACHER 2022-06-13 08:11:49 0 5χλμ.
2 CHRONICLES
Verse by verse explanation of 2 Chronicles 18
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 30 questions at the...
από THE HOLY BIBLE 2022-04-02 01:40:16 0 5χλμ.
Injili Ya Yesu Kristo
UNATEKELEZA WAZO LA NANI UNAPOKUWA NDANI YA JARIBU?
Andiko la msingi ni Matahayo 27:11-20.  Mpenzi msomaji ninakusalimu katika jina la Bwana...
από GOSPEL PREACHER 2021-11-23 12:22:26 0 5χλμ.
NEHEMIAH
Verse by verse explanation of Nehemiah 13
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 29 questions at the...
από THE HOLY BIBLE 2022-04-02 12:36:58 0 6χλμ.
OTHERS
Waislam Wauliza Wakristo
  Swali la 1: Kwa nini mnaliamini Agano la Kale? Jibu: Maandiko na elimukale...
από MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 05:40:11 0 5χλμ.