Je, Biblia inasema nini juu ya Ushoga (ndoa za wanaume kwa wanaume)? Je, Ushoga ni dhambi?

0
5KB
Biblia inasisitiza kila mara kwamba ushoga ni dhambi (mwanzo 19:1-13; mambo ya walawi 18: 22; warumi 1:26-27; wakorintho wa kwanza 6:9). Warumi 1:26-27 inatufundisha ya kwamba ushoga ni njia mojawapo ya kumkana na kutomtii Mungu. Mtu anapodumu katika dhambi na kutokuamini biblia inatuambia ya kwamba “Mungu huwaachilia” kutenda maovu zaidi ili wapate kujua ubatili wa maisha bila Uwepo wa Mungu. Wakorintho wa kwanza 6:9 inasema kuwa mashoga hawataurithi ufalme wa Mungu.
 
Mungu haumbi mwanadamu mwenye tamaa ya ushoga. Biblia inatuambia mtu huwa shoga kwa sababu ya dhambi. (warumi 1:24-27), na pia kwa sababu ya uamuzi wake mwenyewe. Mtu anaweza kuzaliwa na msukumo juu ya ushoga kama vile watu pia huzaliwa na msukumo juu ya fujo na dhambi nyinginezo. Hili halihalalishi dhambi yoyote inayofanywa na wanadamu. Je, mtu akizaliwa na msukumo wa hasira mbaya, ni halali aendeleze hasira zake mbaya? La, hasha. Hata kwa ushoga pia si halali.
 
Hata hivyo Biblia haiitaji dhambi ya ushoga kuwa ndiyo kubwa zaidi. Kila dhambi ni chukizo kwa Mungu. Ushoga ni mojawapo ya mambo yaliyoorodheshwa katika wakorintho wa kwanza 6:9-10 yatakayozuia mtu asiingie katika ufalme wa Mungu. Kulingana na Biblia msamaha wa Mungu juu ya shoga upo sawa na wa mzinzi, muabudu sanamu, muuaji, mwizi na kadhalika. Mungu tena aahidi uwezo juu ya kushinda dhambi, pamoja na ushoga, kwa wale wote watakao mwaminiYesu kristo kwa wokovu wao (wakorintho wa kwanza 6:11; wakorintho wa pili 5:17).
Suche
Kategorien
Mehr lesen
DARASA LA 6
DARASA LA 6
Orodha ya masomo yote ya darasa la 6
Von PROSHABO ONLINE SCHOOLS 2021-10-09 10:17:05 0 5KB
2 KINGS
Verse by verse explanation of 2 Kings 5
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 30 questions at the...
Von THE HOLY BIBLE 2022-03-19 19:29:47 0 5KB
OTHERS
KUMBE QURAN IMEJAA SHAKA NA HAIPO WAZIWAZI
Je, madai ya kuwa Quran imekalika na ipo waziwazi ni ya kweli? Allah ateremsha aya na kudai kuwa,...
Von MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 19:34:25 0 5KB
OTHERS
Do you think Kadhi’s courts should be part of the new Tanzanian Constitution?
The current debate is about whether or not these “Kadhi” courts should be entrenched...
Von MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 20:32:21 0 5KB
SPIRITUAL EDUCATION
VITA INAYOENDELEA JUU MBINGUNI
Zipo vita mbili kuu zinazowahusu shetani na Malaika watakatifu. Vita ya kwanza: Ni ile...
Von GOSPEL PREACHER 2021-10-30 11:35:03 0 6KB