Je, Biblia inasema nini juu ya Ushoga (ndoa za wanaume kwa wanaume)? Je, Ushoga ni dhambi?

0
5KB
Biblia inasisitiza kila mara kwamba ushoga ni dhambi (mwanzo 19:1-13; mambo ya walawi 18: 22; warumi 1:26-27; wakorintho wa kwanza 6:9). Warumi 1:26-27 inatufundisha ya kwamba ushoga ni njia mojawapo ya kumkana na kutomtii Mungu. Mtu anapodumu katika dhambi na kutokuamini biblia inatuambia ya kwamba “Mungu huwaachilia” kutenda maovu zaidi ili wapate kujua ubatili wa maisha bila Uwepo wa Mungu. Wakorintho wa kwanza 6:9 inasema kuwa mashoga hawataurithi ufalme wa Mungu.
 
Mungu haumbi mwanadamu mwenye tamaa ya ushoga. Biblia inatuambia mtu huwa shoga kwa sababu ya dhambi. (warumi 1:24-27), na pia kwa sababu ya uamuzi wake mwenyewe. Mtu anaweza kuzaliwa na msukumo juu ya ushoga kama vile watu pia huzaliwa na msukumo juu ya fujo na dhambi nyinginezo. Hili halihalalishi dhambi yoyote inayofanywa na wanadamu. Je, mtu akizaliwa na msukumo wa hasira mbaya, ni halali aendeleze hasira zake mbaya? La, hasha. Hata kwa ushoga pia si halali.
 
Hata hivyo Biblia haiitaji dhambi ya ushoga kuwa ndiyo kubwa zaidi. Kila dhambi ni chukizo kwa Mungu. Ushoga ni mojawapo ya mambo yaliyoorodheshwa katika wakorintho wa kwanza 6:9-10 yatakayozuia mtu asiingie katika ufalme wa Mungu. Kulingana na Biblia msamaha wa Mungu juu ya shoga upo sawa na wa mzinzi, muabudu sanamu, muuaji, mwizi na kadhalika. Mungu tena aahidi uwezo juu ya kushinda dhambi, pamoja na ushoga, kwa wale wote watakao mwaminiYesu kristo kwa wokovu wao (wakorintho wa kwanza 6:11; wakorintho wa pili 5:17).
Suche
Kategorien
Mehr lesen
1 SAMUEL
Verse by verse explanation of 1 Samuel 31
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 25 questions at the...
Von THE HOLY BIBLE 2022-01-26 05:17:22 0 6KB
EZRA
Verse by verse explanation of Ezra 8
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 24 questions at the...
Von THE HOLY BIBLE 2022-04-02 06:23:21 0 6KB
1 SAMUEL
Verse by verse explanation of 1 Samuel 23
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 33 questions at the...
Von THE HOLY BIBLE 2022-01-26 04:15:25 0 6KB
BIBLICAL FINANCIAL EDUCATION
test
Jeremiah Chapter 48 Verses 1-47: The Moabites were descendants of Lot who lived east of the...
Von PROSHABO NETWORK 2021-12-31 18:31:29 0 8KB
NUMBERS
Verse by verse explanation of Numbers 12
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 26 questions at the...
Von THE HOLY BIBLE 2022-01-24 14:36:34 0 5KB