Je, Biblia inasema nini juu ya Ushoga (ndoa za wanaume kwa wanaume)? Je, Ushoga ni dhambi?

0
5KB
Biblia inasisitiza kila mara kwamba ushoga ni dhambi (mwanzo 19:1-13; mambo ya walawi 18: 22; warumi 1:26-27; wakorintho wa kwanza 6:9). Warumi 1:26-27 inatufundisha ya kwamba ushoga ni njia mojawapo ya kumkana na kutomtii Mungu. Mtu anapodumu katika dhambi na kutokuamini biblia inatuambia ya kwamba “Mungu huwaachilia” kutenda maovu zaidi ili wapate kujua ubatili wa maisha bila Uwepo wa Mungu. Wakorintho wa kwanza 6:9 inasema kuwa mashoga hawataurithi ufalme wa Mungu.
 
Mungu haumbi mwanadamu mwenye tamaa ya ushoga. Biblia inatuambia mtu huwa shoga kwa sababu ya dhambi. (warumi 1:24-27), na pia kwa sababu ya uamuzi wake mwenyewe. Mtu anaweza kuzaliwa na msukumo juu ya ushoga kama vile watu pia huzaliwa na msukumo juu ya fujo na dhambi nyinginezo. Hili halihalalishi dhambi yoyote inayofanywa na wanadamu. Je, mtu akizaliwa na msukumo wa hasira mbaya, ni halali aendeleze hasira zake mbaya? La, hasha. Hata kwa ushoga pia si halali.
 
Hata hivyo Biblia haiitaji dhambi ya ushoga kuwa ndiyo kubwa zaidi. Kila dhambi ni chukizo kwa Mungu. Ushoga ni mojawapo ya mambo yaliyoorodheshwa katika wakorintho wa kwanza 6:9-10 yatakayozuia mtu asiingie katika ufalme wa Mungu. Kulingana na Biblia msamaha wa Mungu juu ya shoga upo sawa na wa mzinzi, muabudu sanamu, muuaji, mwizi na kadhalika. Mungu tena aahidi uwezo juu ya kushinda dhambi, pamoja na ushoga, kwa wale wote watakao mwaminiYesu kristo kwa wokovu wao (wakorintho wa kwanza 6:11; wakorintho wa pili 5:17).
Rechercher
Catégories
Lire la suite
OTHERS
Isaac (Christian) or Ishmael (Islam)
Bible = Genesis 17:18,19 “And Abraham said unto God, O that Ishmael might live before thee!...
Par MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 06:23:35 0 5KB
NDOA KIBIBLIA
NDOA YA MKE MMOJA NA MUME MMOJA NI AGIZO NA NI SHERIA YA MUNGU
UTANGULIZI:Kumekuwepo na mkanganyiko mkubwa katika swala la ndoa kati ya ndoa ya mke...
Par GOSPEL PREACHER 2021-11-08 00:04:02 0 8KB
SPIRITUAL EDUCATION
MIKATABA YA DAMU
Na Mchungaji Kiongozi: Josephat Gwajima.    UTANGULIZI: Katika mfululizo wa masomo haya...
Par MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 02:31:46 0 5KB
EXODUS
Verse by verse explanation of Exodus 26
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 35 questions at the...
Par THE HOLY BIBLE 2022-01-22 18:15:15 0 5KB
DANIEL
DANELI 8
Jina la YESU KRISTO, BWANA wetu libarikiwe. Karibu katika mwendelezo wa kitabu cha Danieli,...
Par GOSPEL PREACHER 2021-11-05 23:59:52 0 8KB