Je, Biblia inasema nini juu ya Ushoga (ndoa za wanaume kwa wanaume)? Je, Ushoga ni dhambi?

0
5KB
Biblia inasisitiza kila mara kwamba ushoga ni dhambi (mwanzo 19:1-13; mambo ya walawi 18: 22; warumi 1:26-27; wakorintho wa kwanza 6:9). Warumi 1:26-27 inatufundisha ya kwamba ushoga ni njia mojawapo ya kumkana na kutomtii Mungu. Mtu anapodumu katika dhambi na kutokuamini biblia inatuambia ya kwamba “Mungu huwaachilia” kutenda maovu zaidi ili wapate kujua ubatili wa maisha bila Uwepo wa Mungu. Wakorintho wa kwanza 6:9 inasema kuwa mashoga hawataurithi ufalme wa Mungu.
 
Mungu haumbi mwanadamu mwenye tamaa ya ushoga. Biblia inatuambia mtu huwa shoga kwa sababu ya dhambi. (warumi 1:24-27), na pia kwa sababu ya uamuzi wake mwenyewe. Mtu anaweza kuzaliwa na msukumo juu ya ushoga kama vile watu pia huzaliwa na msukumo juu ya fujo na dhambi nyinginezo. Hili halihalalishi dhambi yoyote inayofanywa na wanadamu. Je, mtu akizaliwa na msukumo wa hasira mbaya, ni halali aendeleze hasira zake mbaya? La, hasha. Hata kwa ushoga pia si halali.
 
Hata hivyo Biblia haiitaji dhambi ya ushoga kuwa ndiyo kubwa zaidi. Kila dhambi ni chukizo kwa Mungu. Ushoga ni mojawapo ya mambo yaliyoorodheshwa katika wakorintho wa kwanza 6:9-10 yatakayozuia mtu asiingie katika ufalme wa Mungu. Kulingana na Biblia msamaha wa Mungu juu ya shoga upo sawa na wa mzinzi, muabudu sanamu, muuaji, mwizi na kadhalika. Mungu tena aahidi uwezo juu ya kushinda dhambi, pamoja na ushoga, kwa wale wote watakao mwaminiYesu kristo kwa wokovu wao (wakorintho wa kwanza 6:11; wakorintho wa pili 5:17).
Rechercher
Catégories
Lire la suite
Injili Ya Yesu Kristo
YESU ALIISHI KABLA YA DUNIA KUUMBWA
1. Yesu asema kabla ya Abraham kuwepo yeye aliishi2. Yesu aendelea kusema kuwa kabla ya dunia...
Par MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 03:40:41 0 5KB
Injili Ya Yesu Kristo
BIBLIA INAWEZA KUAMINIWA NA KUTEGEMEWA
Kimsingi mwanadamu anaweza kumfikiria Mungu kwa njia kuu mbili: Njia ya kwanza ni ile ya...
Par MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 04:11:59 0 5KB
DEUTERONOMY
Verse by verse explanation of Deuteronomy 12
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 28 questions at the...
Par THE HOLY BIBLE 2022-01-25 06:04:38 0 5KB
SPIRITUAL EDUCATION
WANYAMA SABA 7 KATIKA KITABU CHA DANIEL
1.Tafsiri ya unabii wa hicho kitabu cha Daniel 2.Kuhusu kanisa la Leo.Hivyo sisi kanisa la Leo...
Par Martin Laizer 2023-09-22 07:26:51 4 31KB
SPIRITUAL EDUCATION
Looking at the false doctrine of ‘once saved, always saved’
The false doctrine of “once saved, always saved” teaches that it is not possible for...
Par PROSPER HABONA 2022-01-16 14:43:41 0 5KB