Je, Biblia inasema nini juu ya Ushoga (ndoa za wanaume kwa wanaume)? Je, Ushoga ni dhambi?

0
6KB
Biblia inasisitiza kila mara kwamba ushoga ni dhambi (mwanzo 19:1-13; mambo ya walawi 18: 22; warumi 1:26-27; wakorintho wa kwanza 6:9). Warumi 1:26-27 inatufundisha ya kwamba ushoga ni njia mojawapo ya kumkana na kutomtii Mungu. Mtu anapodumu katika dhambi na kutokuamini biblia inatuambia ya kwamba “Mungu huwaachilia” kutenda maovu zaidi ili wapate kujua ubatili wa maisha bila Uwepo wa Mungu. Wakorintho wa kwanza 6:9 inasema kuwa mashoga hawataurithi ufalme wa Mungu.
 
Mungu haumbi mwanadamu mwenye tamaa ya ushoga. Biblia inatuambia mtu huwa shoga kwa sababu ya dhambi. (warumi 1:24-27), na pia kwa sababu ya uamuzi wake mwenyewe. Mtu anaweza kuzaliwa na msukumo juu ya ushoga kama vile watu pia huzaliwa na msukumo juu ya fujo na dhambi nyinginezo. Hili halihalalishi dhambi yoyote inayofanywa na wanadamu. Je, mtu akizaliwa na msukumo wa hasira mbaya, ni halali aendeleze hasira zake mbaya? La, hasha. Hata kwa ushoga pia si halali.
 
Hata hivyo Biblia haiitaji dhambi ya ushoga kuwa ndiyo kubwa zaidi. Kila dhambi ni chukizo kwa Mungu. Ushoga ni mojawapo ya mambo yaliyoorodheshwa katika wakorintho wa kwanza 6:9-10 yatakayozuia mtu asiingie katika ufalme wa Mungu. Kulingana na Biblia msamaha wa Mungu juu ya shoga upo sawa na wa mzinzi, muabudu sanamu, muuaji, mwizi na kadhalika. Mungu tena aahidi uwezo juu ya kushinda dhambi, pamoja na ushoga, kwa wale wote watakao mwaminiYesu kristo kwa wokovu wao (wakorintho wa kwanza 6:11; wakorintho wa pili 5:17).
Rechercher
Catégories
Lire la suite
OTHERS
UTHIBITISHO 12 KUWA ALLAH SIO MUNGU
  Leo nitawapa Sababu 12 kwanini allah sio mungu. 1. ALLAH NI MUNGU ASIYE NA JINA...
Par MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 03:12:48 0 5KB
HOLY BIBLE
What did Jesus come to do?
To reveal the Father (Matt. 11:27) "All things have been committed to me by my Father. No...
Par MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 05:54:43 0 6KB
NUMBERS
Verse by verse explanation of Numbers 36
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 15 questions at the...
Par THE HOLY BIBLE 2022-01-24 15:40:17 0 6KB
Injili Ya Yesu Kristo
HAKIKA YA KUJIBIWA MAOMBI
Neno la Uzima kutoka kwa  Askofu Zachary Kakobe        ...
Par GOSPEL PREACHER 2022-01-12 01:33:21 0 5KB
SPIRITUAL EDUCATION
AINA 10 ZA WANAWAKE AMBAO BIBLIA INAKUONYA UWAEPUKE
​Ikiwa wewe ni mwanamume mwenye maono, hatima (destiny), na kusudi, huwezi kuruhusu...
Par GOSPEL PREACHER 2026-04-11 21:41:10 0 226